KATASAN'KAZA
JF-Expert Member
- Jul 24, 2013
- 3,097
- 1,356
Jamani, mnijuzeni mwenzenu mpenzi wangu tulikuwa tumeamua kuishi pamoja kabla ya kuhalalisha kwa watumishi wa Mungu.
Wakati huo tunasubiria tukawa tunamega taratibu tunda la mti wa katikati, ghafla mwenzangu mara kavimbiwa, kichefuchefu mara woohh....(katapika) alipoenda kupima akakuta amenasa.
Sasa shida ananichukia vibaya mno na sasa hivi yuko na kisirani na kiburi, ananiangalia kwa jicho la dharau sana!
Na mimi nimeona isiwe shida nimehama zangu nikarudi makazi yangu ya mwanzo, analalamika nirudi na mimi nimegoma.
Anataka nikajitambulishe kwao na mimi nikifikiria anavyonichukia nimemwambia kamwe siendi na pia ana kitabia cha kunishurutisha mara kwa mara kwa kunitumatuma ovyo..." Sielewi kapatwa na nini?
Ushauri jamani.
Wakati huo tunasubiria tukawa tunamega taratibu tunda la mti wa katikati, ghafla mwenzangu mara kavimbiwa, kichefuchefu mara woohh....(katapika) alipoenda kupima akakuta amenasa.
Sasa shida ananichukia vibaya mno na sasa hivi yuko na kisirani na kiburi, ananiangalia kwa jicho la dharau sana!
Na mimi nimeona isiwe shida nimehama zangu nikarudi makazi yangu ya mwanzo, analalamika nirudi na mimi nimegoma.
Anataka nikajitambulishe kwao na mimi nikifikiria anavyonichukia nimemwambia kamwe siendi na pia ana kitabia cha kunishurutisha mara kwa mara kwa kunitumatuma ovyo..." Sielewi kapatwa na nini?
Ushauri jamani.