Nimemkatalia lakini ananisumbua nifanyaje?

Nimemkatalia lakini ananisumbua nifanyaje?

kuchangumu

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2014
Posts
724
Reaction score
290
Kama kuna kitu huyu mwanamke hatambui na hataki kutambua ni Ukweli nilipomwambia "Hapana"maana yake ni hiyo.
Kuna msichana ananikwaza sana kwani kwa muda mrefu nimekuwa ninamkatalia mahusiano na mimi na ni mpenzi wa jamaa yangu wa mtaa.

Siwezi kuwa na mahusiano naye period. Lakini yeye haamini anafikiria namringia au nitabadili mawazo nimeshasema "hapana"HIvi hadi mtu aseme kwa ukali na kumtukana mtu ndio ajue kuwa hatakiwi.Au mpaka nimchane mshikaji live.
Ningekuwa na uwezo wa kumkwepa ningemkwepa lakini ndiyo hivyo.

Hakosekani mtaani na wote tumejenga tena majirani hatujapanga kwa hiyo kuhama inakuwa ngumu sana.Hata ninapokuwa mbali nje ya mtaani haachi kusumbua kwenye mitandao ndio kabisaa,kila saa nimesema "hapana"we kiziwii,unanitafutia balaa kwa jamaa tena ukijuwa wazi ni mbeba vyuma
 
Umaanishe,sio huku unajidai mkali huko PM unamchekea chekea tu

Hata PM namrarua mbaya ila anashupalia ni king'ana'anizi kama luba sasa najiuliza ningekuwa nimemwonjesha asali si ndio ingekuwa balaaa
 
Sasa Mkuu kama anakutafuta fb kule si unaweza kumblock tu asikusumbue tena.. Na kama hapa JF amejuaje id hii kama ni ya kwako wewe..? Na vile vile unaweza ukamuweka kwenye ignore list vile vile..!

Inawezekana sitaki ni kiroho papo hapo..? Au a fictitious story pengine..?
 
Sasa Mkuu kama anakutafuta fb kule si unaweza kumblock tu asikusumbue tena.. Na kama hapa JF amejuaje id hii kama ni ya kwako wewe..? Na vile vile unaweza ukamuweka kwenye ignore list vile vile..!

Inawezekana sitaki ni kiroho papo hapo..? Au a fictitious story pengine..?

Id yake ya JF naijuwa na yeye anaijuwa yangu
So hata nikimfungia hutafuta kila njia kurudi tena.
 
Back
Top Bottom