Mpenzi wangu ni nesi,
aliniaga anakwenda semina ya kikazi, tangu juzi jana nikapigiwa simu na
jamaa kuwa mpenzi wangu kaonekana nyumba flani ambapo wanaishi watu
mbalimbali, na jamaa alinijuza kuwa alikua akinisaliti.
Nilimuliza mpenzi wangu akakataa katu na kuapa kwa mungu na
kunikaripia vikali kwa kusikiliza maneno ya watu. nilidhani ni ukweli
jinsi alivyokuwa serious kujitetea na kulia kwa uchungu.
Leo jamaa kaniita kanambia njoo shuhudia mwenyewe, nimeenda nikakaa
nyumbani kwa jamaa huku nikisikilizia sauti zilizokuwa zinatoka chumba
jirani kwa kuwa nyumba haina sing body.
Gafla mlango wa kile chumba ulifunguliwa na wakatoka nje kuelekea
msalani, na mimi nikatoka nikasimama mlangoni waliporudi alistuka na
sikufanya lolote.
Nimekuja mbio hadi nyumbani natetemeka mwili mzima sijui cha kufanya.
Jamaa aliye nae simfahamu ila nimeona namweza kabisa. Mpenzi wangu ana
ujauzito wa mieiz 2 wa kwangu.
NISHAURINI TAFADHALI