Nimekutana na Maswali ya Kunisumbua

Nimekutana na Maswali ya Kunisumbua

ukitaka kula lazima nawe uliwe hata kidogo.
sasa wewe unataka kula bila kuliwa? Haiwezekani.

sina maana hiyo.

mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake.
 
acha longo longo. mwaga hadharani wtz wajue.usingeandika basi

Ndugu Peter, kuandika hapa haikua na lengo la kutoa habari. Badala ya kutaka tu kujua ni nani au ni kampuni gani, hebu jipe muda kidogo wa kutafakari uone ni nini mwaandishi ametaka kukifikisha kwenye hadhira. Usiiangalie tu kama habari
 
Pole sana mkuu.
Inasikitisha sana lakini hiyo ndiyo hali halisi waTZ tulipofika. Umenikumbusha nyuma kidogo: Niliwahi kuondolewa kwenye position fulani kisa "SIIDHINISHI MALIPO YA UONGO". Mimi ndiye nilikuwa na-certify payments, uadilifu wangu ukaniponza! Nikaambiwa the whole TZ is rotten so I alone can't change it.
 
...Kwa kuendelea kuficha Ugonjwa na 'Wagonjwa' kama ulivyofanya hapa, Hujasaidia Lolote na Ndio maana Rushwa Imetushinda Kuipiga Vita na Sasa Imekuwa Kama Taasisi!:A S 39:
 
...Kwa kuendelea kuficha Ugonjwa na 'Wagonjwa' kama ulivyofanya hapa, Hujasaidia Lolote na Ndio maana Rushwa Imetushinda Kuipiga Vita na Sasa Imekuwa Kama Taasisi!:A S 39:

Baba Desi

Hivi ni kweli ameficha rushwa? hebu jaribuni kumuelewa huyu jamaa. .
 
Hivi umri huo bwana mathewmndeme unaogopa kutaja jina la kampuni kisa umeacha id yako... weka wazi tukusaidie....
 
Last edited by a moderator:
Hivi umri huo bwana mathewmndeme unaogopa kutaja jina la kampuni kisa umeacha id yako... weka wazi tukusaidie....

Mkuu kabanga MR. mathewmndeme anahofia kucha na meno yake. Hata hivyo yeye bado anahitaji watoto wake wakue. Yasije yakamtokea kama ya Prof. Mwaikusa et al..moreover, ni rahisi sana hao jamaa kumtrace na hata kumdhuru maana wanataarifa zake zote.
 
...Kwa kuendelea kuficha Ugonjwa na 'Wagonjwa' kama ulivyofanya hapa, Hujasaidia Lolote na Ndio maana Rushwa Imetushinda Kuipiga Vita na Sasa Imekuwa Kama Taasisi!:A S 39:

Inawezekana kwa upande mmoja lakini katika muktadha mtoa mada alioonyesha ni ngumu kutaja Jina la kampuni husika maana ameacha taarifa zake kwenye ofisi husika!Try to put yourself in his shoes!
 
Pole sana mwl wangu,mathewmndeme. Umenikumbusha kisa cha jamaa yangu aliyehamishiwa mkoani kutoka hapa mjini kisa alikuwa anakataa kupokea hongo ili kuidhinisha fedha ambazo alikuwa anaagizwa na wakubwa wake kwenye Ofisi ya serikali!

Lakini hii mizizi ya rushwa ni vigumu sana kufutika, labda tu kupungua!
 
Mbona umeficha jina la hiyo kampuni?,hujatusaidia bado mkuu funguka.
 
Inawezekana kwa upande mmoja lakini katika muktadha mtoa mada alioonyesha ni ngumu kutaja Jina la kampuni husika maana ameacha taarifa zake kwenye ofisi husika!Try to put yourself in his shoes!

..Woga Wetu ndio Mauti Yetu Mkuu na Kama kuna Watu Waoga na Kondoo Duniani Basi watu Hao ni Watanzania, Ndio Maana Mafisadi Wanatamba.
Mkuu ametuambia kuwa ameingia kwenye ofisi hiyo na akakuta imejaa wateja kibao na yeye ndio akavutwa chemba kidogo. Amesema pia kuwa mazingira ya watu kuombwa Rushwa yalikuwa yametamalaki:

Sasa basi, anajuaje kwamba ni yeye pekee aliyekataa kutoa rushwa kiasi cha kwamba atajulikana kwa kutaja jina la Kampuni husika Humu?
Ana Uhakika gani kwamba hao wala rushwa wataweza kuunganisha jina lake alilotumia ofisini hapo na jina lake analotumia humu JF??
Anajuaje kwamba katika hiyo siku husika Hakukuwa na wana JF ama Wakristo wengine wengi tu ambao pia waliombwa Rushwa na Kukataa???

Mkuu anaweza kutoa Visingizio vyovyote humu ili kuhalalisha kwake kuogopa kutaja majina ya ofisi husika na wahusika waomba rushwa.
Hatuwezi Kumlaumu.
Ndio asili yetu Watanzania ya Ukondoo na Kuogopa watu tuliowaajiri wenyewe. Na ndio maana wanaendelea kutugeuza wanavyotaka mpaka tu pale tutakapokuwa na Ujasiri wa kusema HAPANA na pia kuacha Ubinafsi wa kila mmoja wetu Kujipenda mwenyewe na familia yake tu!!!

:A S 39:
 
Kwa kweli rushwa ni kitu kinanikera sana Tanzania. Rushwa ndiyo inayorudisha nyuma maendeleo ya nchi. Kwa kiasi kikubwa sana makampuni binafsi yamesaidia kuondoa kero kwa wananchi wa hali ya chini japokuwa yamechochea rushwa serikalini kwani yanashiriki sana katika kuwahonga watuminshi wa serikali na wanasiasa.

Kwa maoni yangu ni vyema tukianika vitendo vyote vya rushwa kila vinapotokea ijapokuwa ni vyema kufanya hivyo bila kuhatarisha maisha yako. Mwalimu Mndeme angeweza kuanika uozo wa hiyo kampuni kwa kutumia njia mbalimbali.
 
Ndugu yangu, dhana ya uandishi kwenye public pamoja na mambo mengine imejikita katika thinking inayomuongoza mwandishi. Kwamba aandike nini na asiandike nini, inatokana na lengo la alichokiandika ana anachotaka kukifikisha kwenye hadhira.

Mimi lengo langu la kuandika hapa halikua kutaja jina la mtu wala kampuni,..ningetaka kufanya hivyo ningefanya tu hata kama sio kwa kutumia jina langu kama ambavyo wewe BabaDesi umefanya hapa kwa kushindwa kutumia jina lako halisi kwenye forum hii. Nadhani huniafahamu vema hivyo usikimbilie kuniita muoga kwa kutaka tu kutimiza kiu yako ya kujua majina. Ungependa ungekwend ambele zaidi kutaka kuona nilitaka kutoa ujumbe gani...nilichoandika hapa siyo news wala udaku..soma vizuri na kutafakari hasa maswahili niliyoyaibua.

Pamoja na hayo, naelewa tofuati ambazo tunaweza kuwa nazo katika mitazamo, priorities na jinsi tunavyochulia mambo..na kwa hiyo sio lazima nikidhi mahitaji yako

...Na hili ndilo ambalo Wabongo tuko katika Viwango vya Juu kabisa vya Ubora...Maneno Meengi, Vitendo Haba.
Bado tuna Safari Ndefu ya Kwenda ili Kutoka hapa pa Kila Mtu kuwaza Madhara yatakayompata Yeye Binafsi na Familia Yake iwapo atataja majina ya Wala Rushwa na Wauza Madawa badala ya Kuwaza Madhara yanayolipata Taifa kwa Ujumla Wake.
Mwalimu, Ili ule Omelette ni Lazima Mayai mawili matatu yalazimike Kuvunjwa.
Ni Lazima baadhi Yetu Watajikuta Watalazimika Kujitoa Mhanga ili Rushwa kwa Vizazi vyetu Vijavyo iwe ni Kama Simulizi za Kusisimua tu.
Kudra na mazingira yakikuchagua Wewe kuwa Mhanga, Usiogope.
Ndivyo Wenzetu Walivyofanikiwa katika Kupiga Vita Rushwa.



 
Back
Top Bottom