Nimekusamehe lakini sitasahau

Nimekusamehe lakini sitasahau

Benny

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2014
Posts
3,275
Reaction score
5,414
Habari ndugu zangu wa Jf,

Hili ni jambo ambalo linanitatiza kidogo hivi kumsamehe mtu maana yake ni nini hasa? Na ukimsamehe mtu lile jambo alilokutenda ni lazima ulisahau? Na vipi umemsamehe lakini bado unalikumbuka na linakuumiza si msamaha huo?

Naombeni expirience yenu mliowahi kuwasamehe watu waliowaumiza kama ni kweli unasamehe na kusahau? Binafsi nasamehe sana ila sisahau nilichotendwa.

Naombeni msaada kama na mimi ninaweza kusamehe na kusahau au kutokusahau lililoumiza ni tatizo la kila mtu nami niendelee kusamehe na nisisahau
.
 
Unasamehe but huezi kusahau, cha msingi tu ku ignore tu maumivu as long as umesamehe, na uliemsamehe he/she shud do u good fr a lngtym kidgo hii inaweza kusaidia kusahau na kuona mybe alitereza kidgo kuliko uliemsamehe kukuletea mkosa mwingne, Huo sass ndio tunauita MSALA
 
Kusahau labda upoteze kumbukumbu. Lakin HAIWEZEKANI, kusamehe kupo lakini
 
Kusamalehe na kusahau ni kama kidonda kugeuka kovu. Unaweza samehe na roho isikuume ukikumbuka, hapo ni sawa na kidonda kugeuka kovu, unaliona kovu ila halikuumi tena maana liliisha pita. Ukubwa wa kovu hutegemea na kidonda kilikuwaje..
 
mtu asiye na akili timamu labda ndo anayeweza kusamehe na kusahau...tunasamehe tu ila hatusahau

Taahira tu na mwenye mtindio wa ubongo ndio anaweza kusamehe na asisahau. Mwenye akili timamu husamehe na kusahau au kutokusamehe na kutokusahau. Umesamehe alafu husahau ya nini umesamehe.

Hilo neno tunasamehe hatusahau wewe na nani? Kama wewe unasamehe ila husahau sema wewe sio kujumlisha watu wote. Wengine tuna akili timamu na hatuma matatizo ya mtindio wa ubongo.
 
Taahira tu na mwenye mtindio wa ubongo ndio anaweza kusamehe na asisahau. Mwenye akili timamu husamehe na kusahau au kutokusamehe na kutokusahau. Umesamehe alafu husahau ya nini umesamehe.

Hilo neno tunasamehe hatusahau wewe na nani? Kama wewe unasamehe ila husahau sema wewe sio kujumlisha watu wote. Wengine tuna akili timamu na hatuma matatizo ya mtindio wa ubongo.

mmh kusahau na kusamehe vinauhusiano gani?

Hivi kusamehe ni kujisahaulisha unacho kumbuka?
 
Good idea mkuu! Pia inategemea kosa na kosa mengne ni madodgodog na ni rahs kusamehe vlevle kusahau kabisa
Kusamalehe na kusahau ni kama kidonda kugeuka kovu. Unaweza samehe na roho isikuume ukikumbuka, hapo ni sawa na kidonda kugeuka kovu, unaliona kovu ila halikuumi tena maana liliisha pita. Ukubwa wa kovu hutegemea na kidonda kilikuwaje..
 
Tunasamehe ili tuweze kusonga mbele na tusiwe watumwa kwa kile kilichotutokea. Kusahau kabisa??? Binafsi sijafanikiwa bado. Nakubaliana na na mtoa hoja aliefananisha na kidonda ambacho kinaishia kuwa kovu; unakumbuka lakini huumiii tena?
 
As long as sitampasua nikikutana naye huko ni kumsamehe, ila swala la kusahau halipo, reference muhimu kuwa nazo ili ujue wabaya wako
 
Wewe nikukute unafanya mapenzi ma mke wangu, naweza kukusamehe ila sitaweza sahau kuwa niliwahi kukuta umelala na mke wangu... labda ufe
 
mmh kusahau na kusamehe vinauhusiano gani?

Hivi kusamehe ni kujisahaulisha unacho kumbuka?

Nimetumia logic ya kidini, Mungu anasema anasamehe na kusahau alafu anatutaka sasa tufanye hivyo. Angekua anasamehe na hasahau hakuna maana ya kusamehe.

Jifunzeni kutoka kwangu maana mimi ni mnyenyekevu na mpole, nadhani umenipata.

Kusamehe na kutosahau vina uhusiano gani?
Kwani kusamehe ni kujikumbusha unachokikumbuka?
 
Kusamehe ni somo kubwa sana na inabidi ujifunze kusamehe. Kusamehe kunaendana na kusahau kwa sababu msamaha wa kweli ni kuyaacha yaliyopita na kuanza upya ukiwa mweupe (clean) moyoni. Ukikumbuka makosa uliyofanyiwa utaumia na hapo utamchukia aliyekukosea na msamaha utakuwa haujafanya kazi.

Binafsi kuna mtu alinikosea sana na nilipitia situation kama yako ila kuna vitabu nilivisoma na kusikiliza kama why forgive (audio book), when forgiveness seems impossible ( discovery series) n.k ambavyo vilinisaidia kusamehe na kusahau.

Kusamehe kunaendana na kusahau na kusamehe bila kusahau basi si msamaha wa kweli kwa kuwa bado utateseka na kosa ulilofanyiwa na mwisho wake ni chuki kwa aliyetenda kosa.
 
Kusamehe ni karama ambayo wachache sana wamejaliwa...
Binafsi sidhani kama naweza kumsamehe mtu kirahisi hivyo...
 
Habari ndugu zangu wa Jf,

Hili ni jambo ambalo linanitatiza kidogo hivi kumsamehe mtu maana yake ni nini hasa? Na ukimsamehe mtu lile jambo alilokutenda ni lazima ulisahau? Na vipi umemsamehe lakini bado unalikumbuka na linakuumiza si msamaha huo?

Naombeni expirience yenu mliowahi kuwasamehe watu waliowaumiza kama ni kweli unasamehe na kusahau? Binafsi nasamehe sana ila sisahau nilichotendwa.

Naombeni msaada kama na mimi ninaweza kusamehe na kusahau au kutokusahau lililoumiza ni tatizo la kila mtu nami niendelee kusamehe na nisisahau
.

ni kumuomba Mungu akusaidie uachilie, once you really forgive with Gods help, u just forget it, inakuwa nyuma kabisa ya akili yako, yani hata ukijaribu kukumbuka it just doesnt work, niamini!unaweza kusamehe na kusahau, naongea from experience...unaweza kumbuka ila haikupi tatizo, haikuletei hasira...yani ni kama kitu kingine tu kisicho na maana ambacho kitakupotezea mda ukikipa mda
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom