Nimekumbuka zamani

Myangu

JF-Expert Member
Dec 15, 2012
7,172
9,697
Haikuwa kitu rahisi Mimi kukubali kuhamia boarding / hostel kwa umri ume na stori za kipindi hicho kuhusu huko boarding. Kwa bahati mbaya mama yangu akapata nafasi ya kuongeza kisomo ktk chuo fulani kikongwe ktk mambo ya uongozi.

Fasta bimkubwa yule kaenda wizarani nikapata nafasi ya kutoka day kuja hostel.Maisha ya ratiba ndiyo kwanza nayaanza duuh ilikuwa mfecane war sana kwangu.Menyu nilikuwa shida kitu cha maharage na bondo jioni niliona balaa. Jumba bovu liangukia miye.Ntafanyaje maisha mapya nimeyaanza.

Likizo ya mwezi wa sita naleta matokeo nyumbani hesabu nimelamba D, bi mkubwa wangu akashtuka kweli viiipii wewe mbona shule ya msingi uliweza sana hili soma.Nikampa makavu live kule kingreza Mimi sijakimaster bado.Duuuhh bi mkubwa akasema isiwe kesi, ukifungua ulizia tution uanze. Hapo ukizingatia shule bado sijaimaster vizuri maana miye nilihamia mwezi wa pili mwishoni.

Tulipofungua nikapewa vitu vyangu vyoote sabauni,blue band,mangopiko,sukari ,maziwa ya unga.Na posho ya tution kwa mwezi huo hata haikuwa pesa ndefu sh 300 tuu.Nilipofika zangu hostel nikajichana ila nikawa naogopa kuomba ruhusa ya kwenda tution jumamosi / jumapili maana jumamosi tulikuwa na inspection ya kufa mtu, mitundiko,viatu hujapanga, locka liwe safi, space inasuguliwa na sabuni.Yaani ile saa 4 ikipita inspection roho juuu juu.Hadi mpasishwe ndiyo roho inatulia. Kwa woga wangu siku zikapita bi mkubwa anajua miye nimeanza tution kitambo ili nimuonyeshe surprise kwenye exams. Na nilivyo kimeo nikampa na timetable kabisa.

Jumamosi moja bi mkubwa katinga anga zangu mpk kwa ticha anauliza nina mtt wangu ........... Ameniambia wewe ndiyo mwalimu wake wa maths anakaa hostel bweni ........Mhhh yule ticha akasema tuu mwanao sijawahi muona na hajawahi kuingia humu. Bi mkubwa wangu akapandisha mpk hostel na mazaga zaga yake nikatafuta nikapatikana nikaulizwa kwanini hujaenda tution leo nikajibu nilikuwa nafyeka ploti sikupata muda.

Wakati namsindikiza ili aondoke akanipa makavu wewe huendi tuion wala nini pesa yangu unakula tuuu.Sasa nimemwambia maagizo ticha akufuatilie kila siku na pesa yooote ya miezi sita nimeona.Duuh jioni wakati naenda dinning ticha namuona ananisubiri uwanjani.Weee kuja hapa kwanini huingii class kwangu wkt unapewa pesa kwa wazazi wako, nikamwambia miye naogopa kuomba ruhusa ya kuja shule jumamosi. Akasema kuanzia sasa ntamwambia walimu wawe wanakuruhusu.

Namshukuru mama yangu kwa kusimmama kidete mpk nikawa kupanga nzuri wa maths. Hadi chuo sikupata tabu sana ya course niliyosomea.

Asante mama kwa kuona mbali.
 
Haikuwa kitu rahisi Mimi kukubali kuhamia boarding / hostel kwa umri ume na stori za kipindi hicho kuhusu huko boarding. Kwa bahati mbaya mama yangu akapata nafasi ya kuongeza kisomo ktk chuo fulani kikongwe ktk mambo ya uongozi.

Fasta bimkubwa yule kaenda wizarani nikapata nafasi ya kutoka day kuja hostel.Maisha ya ratiba ndiyo kwanza nayaanza duuh ilikuwa mfecane war sana kwangu.Menyu nilikuwa shida kitu cha maharage na bondo jioni niliona balaa. Jumba bovu liangukia miye.Ntafanyaje maisha mapya nimeyaanza.

Likizo ya mwezi wa sita naleta matokeo nyumbani hesabu nimelamba D, bi mkubwa wangu akashtuka kweli viiipii wewe mbona shule ya msingi uliweza sana hili soma.Nikampa makavu live kule kingreza Mimi sijakimaster bado.Duuuhh bi mkubwa akasema isiwe kesi, ukifungua ulizia tution uanze. Hapo ukizingatia shule bado sijaimaster vizuri maana miye nilihamia mwezi wa pili mwishoni.

Tulipofungua nikapewa vitu vyangu vyoote sabauni,blue band,mangopiko,sukari ,maziwa ya unga.Na posho ya tution kwa mwezi huo hata haikuwa pesa ndefu sh 300 tuu.Nilipofika zangu hostel nikajichana ila nikawa naogopa kuomba ruhusa ya kwenda tution jumamosi / jumapili maana jumamosi tulikuwa na inspection ya kufa mtu, mitundiko,viatu hujapanga, locka liwe safi, space inasuguliwa na sabuni.Yaani ile saa 4 ikipita inspection roho juuu juu.Hadi mpasishwe ndiyo roho inatulia. Kwa woga wangu siku zikapita bi mkubwa anajua miye nimeanza tution kitambo ili nimuonyeshe surprise kwenye exams. Na nilivyo kimeo nikampa na timetable kabisa.

Jumamosi moja bi mkubwa katinga anga zangu mpk kwa ticha anauliza nina mtt wangu ........... Ameniambia wewe ndiyo mwalimu wake wa maths anakaa hostel bweni ........Mhhh yule ticha akasema tuu mwanao sijawahi muona na hajawahi kuingia humu. Bi mkubwa wangu akapandisha mpk hostel na mazaga zaga yake nikatafuta nikapatikana nikaulizwa kwanini hujaenda tution leo nikajibu nilikuwa nafyeka ploti sikupata muda.

Wakati namsindikiza ili aondoke akanipa makavu wewe huendi tuion wala nini pesa yangu unakula tuuu.Sasa nimemwambia maagizo ticha akufuatilie kila siku na pesa yooote ya miezi sita nimeona.Duuh jioni wakati naenda dinning ticha namuona ananisubiri uwanjani.Weee kuja hapa kwanini huingii class kwangu wkt unapewa pesa kwa wazazi wako, nikamwambia miye naogopa kuomba ruhusa ya kuja shule jumamosi. Akasema kuanzia sasa ntamwambia walimu wawe wanakuruhusu.

Namshukuru mama yangu kwa kusimmama kidete mpk nikawa kupanga nzuri wa maths. Hadi chuo sikupata tabu sana ya course niliyosomea.

Asante mama kwa kuona mbali.
lakini mbona hujui kuandika?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom