Nimekukumbuka Mchungaji Mtikila

hasan124

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
716
128
Mchungaji Christopher Mtikila mwenyekiti wa DP nimekukumbuka mzazi wangu.
Nimekukumbuka kwa suala moja tu, nalo Ni UTANGANYIKA. Nakukumbuka sana na gari Lako lile ukipeperusha Bendera ya Tanganyika hakika Ni wachache tulikuelewa.
Nimekukumbuka sana kipindi hiki hasa baada ya kuona namna ambavyo ndugu zetu wa Zanzibar wanavyotubagua na kudai nchi Yao kana kwamba Watanganyika tumewapora.
Nimetembelea mtandao wa kijamii wa Mzalendo.net ambao Ni wa wenzetu hawa na kukutana na kura zinazoendeshwa za AMA kuuunga AMA kupinga muungano. 87% Wanasema Uvunjwe na only 13% Wanasema Usivunjwe. Hii inaashiria nini? Binafsi inaniambia kwamba Sisi si wamoja, kuna Wao Wazanzibar na Sisi Watanganyika.
Ukisikiliza coment za Watanganyika wengi wanaunga MKONO Muungano lakini Ni kinyume kwa wenzetu hawa.
Mhe. HAMAD Rashid Mbunge wa WAWI Cuf, kafukuzwa kwa kuhoji tu upendeleo unaonyeshwa na viongozi wa chama CHAKE kwa upande wa Visiwani.
Inashangaza kuona kwamba Ni juzi tu, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Cuf MHE. Ismail Jusa amesikika Alizungumzia kushindwa kwao katika uchaguzi mdogo JIMBO la Uzini eti kisa Ni Ukristo na Ubara uliokithiri eneo lile.
Nijuavyo mimi, kuna Wazanzibar Karibu million moja wote kwa ujumla na nina hakika KATI Yao zaidi ya laki moja wanaishi bara na wamewekeza na kuendesha shughuli zao za kujipatia riziki Kama walivyo Wamakua, Wamakonde,Waha,Wakurya na makabila mengine mengi tu yaliyopo nchini mwetu.
Nachelea kufikiri wangekuwa wapi pasipo Muungano? AMA ndio ile DHAMBI ALIYOKUWA ANAIHUBIRI MWALIMU JULIUS NYERERE?
Nimekukumbuka Mchungaji kwa kusimamia Utanganyika wetu, hakika uko sahihi katika hili.
Hebu Watanganyika tuifanyieni kazi hii Katiba mpya.
 
Muungano ndo kosa kubwa alotutendea baba wa Taifa kwa kutuunganisha na watu wasiopenda mahusiano na bara,
 
Nadhani hali ya kutawaliwa inawanukia hao wala urojo na wanaipenda. Nachelea kuwa ujasiri walionao umeegemea kwa "wajomba" walioko nyuma yao. Watalia hawa mtaniambia nasema!
 
Muungano ndo kosa kubwa alotutendea baba wa Taifa kwa kutuunganisha na watu wasiopenda mahusiano na bara,

ubinafsi na ubaguzi wao ndio utawamaliza....naamini kuna umuhimu mkubwa sana na sisi watanganyika tukajitazama upya, tukatazama utanganyika wetu na kujipanga kama watanganyika. Binafsi sioni sababu ya kubembeleza watu wasiojua umuhimu wa kuwa nasi. Hawa ni wabaguzi na hata kama nami nitaonekana nawabagua basi sawa naridhia kuwabagua kwanni hatukuanza sisi ni wao ndio wameanzisha yote haya. kuna mambo mengi sana kwa kupitia huu muungano wanabenefit hawa wenzetu lakini inasikitisha viongozi wao hawawaelezi ukweli. wanawaficha hivyo inaonekana bara tunawanyonya.
 
Hawa waponjoro ni washe -------------i tu!! kwa nini wasihoji mantiki ya akina Jussa kudai watu milioni 41[wabara] wanalelewa na population ya watu million moja[wazanzibar]? hivi zanzibar ina kipato gani cha kutulisha wabara millioni 41 hadi wajivune kuwa tunawanyonya?
 
Hawa waponjoro ni washe -------------i tu!! kwa nini wasihoji mantiki ya akina Jussa kudai watu milioni 41[wabara] wanalelewa na population ya watu million moja[wazanzibar]? hivi zanzibar ina kipato gani cha kutulisha wabara millioni 41 hadi wajivune kuwa tunawanyonya?

Inashangaza kuona sababu Kama hizo wanazotoa ilhali kwa uhalisia huhitaji elimu Kubwa sana kujua nani ananufaika zaidi na muungano huu. Hawa wenzetu wanachukua almost Kila kitu kutoka bara, kuanzia umeme, vyakula vyote kwa ujumla wake....sidhani Kama kuna mkandamizo huo wanaouzungumzia napa.....
Fursa ZANZ kimaisha Zanzibar haziwezi kuwa sawa na bara, tuna demand Kubwa ya bidhaa mbalimbali kutokana na iddi yetu kuwa Kubwa. Sijui Sijui, hebu ninyi viongozi mnaochochea kuuvunja huu muungano, jitazameni.
 
Hawa waponjoro ni washe -------------i tu!! kwa nini wasihoji mantiki ya akina Jussa kudai watu milioni 41[wabara] wanalelewa na population ya watu million moja[wazanzibar]? hivi zanzibar ina kipato gani cha kutulisha wabara millioni 41 hadi wajivune kuwa tunawanyonya?

Inashangaza kuona sababu Kama hizo wanazotoa ilhali kwa uhalisia huhitaji elimu Kubwa sana kujua nani ananufaika zaidi na muungano huu. Hawa wenzetu wanachukua almost Kila kitu kutoka bara, kuanzia umeme, vyakula vyote kwa ujumla wake....sidhani Kama kuna mkandamizo huo wanaouzungumzia napa.....
Fursa ZANZ kimaisha Zanzibar haziwezi kuwa sawa na bara, tuna demand Kubwa ya bidhaa mbalimbali kutokana na iddi yetu kuwa Kubwa. Sijui Sijui, hebu ninyi viongozi mnaochochea kuuvunja huu muungano, jitazameni.
 
wanaodekeza hawa wazenj ni ccm tu! yaani wazenj wanaina Tanganyika kama wamerishishwa na mama zao!
 
MA*********, WAMEMKOLIMBA. hizi ni semi alizoziibua mtanganyika huyu machachali bingwa wa kesi , sijamsikia siku nyingi kweli yuko kimya muda mrefu sasa au ndo wameisha mfiksi......?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom