Nimekubali MUHONGO ni muongo

Nimekubali MUHONGO ni muongo

manning

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2013
Posts
5,093
Reaction score
11,948
Nakumbuka mara baada ya kumwapisha anaeyeitwa Prof Muhongo na Katibu wake mkuu Maswi walitamba sana kwamba KWA SASA MGAO UTAKUWA NI HISTORIA. Kwa sasa niko hapa Mwanza kikazi. Tangu nifike hapa Mwanza ni karibu masaa 70 lakini sijauona umeme wa TANESCO hapa tangu nifike hapa . Niliporejea Tangazo la Tanesco la mgao wala Mwanza haimo lakini hali ndo hii na hakuna taarifa nyingine zaidi ya tangazo lao katika magazeti. Tahadhari kwa wanaozaa bado muwe waangalifu kuchagulia watoto wenu majina , unaweza kumpa mototo jina likaja kuendena na matendo yake.
 
Mkuu KILL nakuunga mkono hii Serikali ya CCM imeshachoka kabisa na kujisahau pia, hakuna Waziri anaefanya kazi kikamilifu, Anayejaribu kujitutumua anakutana na rungu la Waziri mkuu.
 
Huyu Muhongo kavunja rekodi , masaa zaidi ya sabini bila tone la umeme !!!???!!
 
Bungeni walishasema sasa mlitaka kujua zaidi? Ilifaa awajibike wakati alipodanganya bungeni!
 
Namshauri mkuu wa kaya avunje baraza la Mawaziri, Kama hata CCM wenyewe wanalalamika hawa mawaziri wanamtumikia nani?
 
Nakumbuka mara baada ya kumwapisha anaeyeitwa Prof Muhongo na Katibu wake mkuu Maswi walitamba sana kwamba KWA SASA MGAO UTAKUWA NI HISTORIA. Kwa sasa niko hapa Mwanza kikazi. Tangu nifike hapa Mwanza ni karibu masaa 70 lakini sijauona umeme wa TANESCO hapa tangu nifike hapa . Niliporejea Tangazo la Tanesco la mgao wala Mwanza haimo lakini hali ndo hii na hakuna taarifa nyingine zaidi ya tangazo lao katika magazeti. Tahadhari kwa wanaozaa bado muwe waangalifu kuchagulia watoto wenu majina , unaweza kumpa mototo jina likaja kuendena na matendo yake.

Muhongo kasema wabongo ni wavivu wa kufikiri na kusoma. Hoja zako zinainyesha wewe ni mmoja wao. Ni mfano mzuri wa wavivu wa kufikiri
 
Back
Top Bottom