Fahari ya kusini
JF-Expert Member
- Nov 26, 2022
- 427
- 1,668
Chumba kimoja ninachoishi kimenikumbuka kuwa napoteza muda na maisha ya mjini; heri nirudi kijijini.
Haiwezekani nina miaka 35 halafu bado naishi kwenye chumba kimoja.
Ukiachilia mbali majirani kuniona 'mhuni' niliyegoma kukua, kuna sababu nyingine nyingi zimenilazimisha nihame.
1. Haiwezekani hadi leo nalala chumba kimoja na magudulia ya maji. Naweka viatu uvunguni. Napikia chumbani. Miaka 35?
2. Kila siku nawatembelea jamaa makwao, nakwepa waje kwangu kwa sababu sebuleni nd'o chumbani. Si jambo jema kila mgeni kuona ninapolala.
3. Nikipata mgeni wa maana, tunakutana barabarani, kwa sababu naona haya kumkaribisha kwangu. Wanaona siko 'serious' na maisha yangu.
4. Miaka 35 bado namletea michezo ya kombolela mwenye nyumba. Kodi ikiisha nawahi kuamka na kuchelewa kulala, alimradi kumkwepa tu. Miaka 35 bado nashindwa kulipa kodi ya 35,000? Yaani kila mwaka nilioishi duniani thamani yake ni buku, lakini bado ndefu. Huu ni utani, watu wa rika langu wana nyumba za kupangisha, mimi bado nakimbizana na kodi. Najitambua kweli?
Heri nirudi nyumbani kijijini, huko nitajenga kibanda katika shamba kubwa la urithi. Mwembe wa nje utakuwa sebule; hapo ndipo nitakapofanyia vikao na wageni wangu. Madumu nitayaweka nje kwa kuwa kule kijijini hatuibiani.
Haya maisha ya kuishi mjini kwenye chumba kimoja ilhali mali pekee ya thamani ninayomiliki ni king'amuzi, si maisha. Au niseme, yana ukomo. Si maisha ya sisi 35+.
Nimekubali kushindwa vita. Narudi kijijini...
Naenda kuandaa mikorosho na ufuta
Haiwezekani nina miaka 35 halafu bado naishi kwenye chumba kimoja.
Ukiachilia mbali majirani kuniona 'mhuni' niliyegoma kukua, kuna sababu nyingine nyingi zimenilazimisha nihame.
1. Haiwezekani hadi leo nalala chumba kimoja na magudulia ya maji. Naweka viatu uvunguni. Napikia chumbani. Miaka 35?
2. Kila siku nawatembelea jamaa makwao, nakwepa waje kwangu kwa sababu sebuleni nd'o chumbani. Si jambo jema kila mgeni kuona ninapolala.
3. Nikipata mgeni wa maana, tunakutana barabarani, kwa sababu naona haya kumkaribisha kwangu. Wanaona siko 'serious' na maisha yangu.
4. Miaka 35 bado namletea michezo ya kombolela mwenye nyumba. Kodi ikiisha nawahi kuamka na kuchelewa kulala, alimradi kumkwepa tu. Miaka 35 bado nashindwa kulipa kodi ya 35,000? Yaani kila mwaka nilioishi duniani thamani yake ni buku, lakini bado ndefu. Huu ni utani, watu wa rika langu wana nyumba za kupangisha, mimi bado nakimbizana na kodi. Najitambua kweli?
Heri nirudi nyumbani kijijini, huko nitajenga kibanda katika shamba kubwa la urithi. Mwembe wa nje utakuwa sebule; hapo ndipo nitakapofanyia vikao na wageni wangu. Madumu nitayaweka nje kwa kuwa kule kijijini hatuibiani.
Haya maisha ya kuishi mjini kwenye chumba kimoja ilhali mali pekee ya thamani ninayomiliki ni king'amuzi, si maisha. Au niseme, yana ukomo. Si maisha ya sisi 35+.
Nimekubali kushindwa vita. Narudi kijijini...
Naenda kuandaa mikorosho na ufuta