Nimejenga nyumba katika eneo ambalo halijapimwa, je naweza kupata hati ya nyumba?

soma sera ya waziri Lukuvi vizuri kisha nijibu kama huo uwanja umeununua mbele ya serikali ya mtaa au umerithi
 
soma sera ya waziri Lukuvi vizuri kisha nijibu kama huo uwanja umeununua mbele ya serikali ya mtaa au umerithi
Naipata wapi hiyo sera ya lukuvi ndugu maana hata me mdogo mdogo soon ntamaliza mjengo ila nina vibali vya serikali ya mtaa tu na kitambulisho cha umiliki WA eneo ambacho kinatunza kumbukumbu za wamiliki makazi na viwanja eneo husika.
 
Hati ya Nyumba haitolewi katika maeneo ambayo hayajapimwa!!!!
Kinachotolewa katika maeneo kama hayo ni leseni za makazi(residential licence)

Pia kama eneo lipo ndani ya Mji shauriana na majirani zako ili mpimiwe kupitia upimaji shirikishi gharama inashuka kidogo....
 
Back
Top Bottom