Nimechoka kumtetea Dube

Timu haina number 10,Dube mwenyewe leo hajapata nafasi ya maana,Doumbia mzito hana kasi hata kufanya maamuzi anachelewa. Ndio maana wakati wa usajili huwaga sipendagi kuwasikiliza wasemaji mara nyingi wanatuingiza chaka.

Yanga msimu huu ilikuwa inahitaji kujaza nafasi ya Ki,Ikangalombo na Musonda na kocha angebaki yuleyule. Ila ndio hivyo kila msimu wanataka kusajili wapya ili watrend kwenye social media na vyombo vya habari, wakati timu ilikuwa haihitaji mabadiliko makubwa.

Alivyo ingia yule dogo na Ecua ndipo mpira ukabadilika.Ila kwa Yanga hii,tusiwe na matarajio makubwa CAF ila kocha anatakiwa apewe ushirikiano dirisha dogo.
 
Kweli kabisa mkuu
Huwezi kumtoa Ki ukamleta Kouma
Doumbia ana vitu ila anacheza mbali na ni mbivu mno
 
Yanga ilipaswa ipate mechi tatu kabla ya kuingia kwenye mchezo wa klabu bingwa ili kuongeza fitness na muunganiko.
 
Yanga ilipaswa ipate mechi tatu kabla ya kuingia kwenye mchezo wa klabu bingwa ili kuongeza fitness na muunganiko.
Wachezaji wanaenda international break
 
Dube ni shida ila changamoto kubwa ni upangaji wa kikosi, Max ukimuweka namba 8 unaikosesha timu kupata mchango wake kikamilifu, kwanini hawamwamini sure boy acheze na Abuya kwenye midfield!

Hawa wachezaji wapya asilimia kubwa tumefeli kwangu naona hamna mchezaji wa ku upgrade kiwango cha timu, wengi wao hawana kiwango cha kuwazidi waliopo, tukiwalazimisha tutafeli msim huu
 
Nimejikuta hata na mie naumiza kichwa huko Champions League itakuwaje sababu kiufupi timu yetu ipo ipo tu kwa sasa yaani matokeo tunayapata kwa shida mno.
 
Wachezaji wanaenda international break
Hilo nafahamu ila Yanga imekuwa sio ile ya Gamondi, sio ile ya Miloud. Ya Miloud ilikuwa ni strong kwenye ulinzi na kushambulia. Ila hii ni kama aliyekatwa kichwa inajiendea hovyo hovyo tu. Anawezekana ikawa ni msimu mbaya sana kwa Yanga na msababishani ni Hersi.
1kumuacha Miloud kizembe na kuiingiza Yanga katika laana kwa kuchangia CCM.
 
Nimejikuta hata na mie naumiza kichwa huko Champions League itakuwaje sababu kiufupi timu yetu ipo ipo tu kwa sasa yaani matokeo tunayapata kwa shida mno.
Mlipoteza muda kulaumu kocha mkidhani yeye ndiye tatizo, kumbe tatizo kubwa zaidi ni timu yenu.
 
Uko sahihi
Nadhani kila kitu ni funzo
Huu msimu tutafeli kwakweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…