Nimechanganyikiwa.

Nimechanganyikiwa.

Eleine

Member
Joined
Jan 30, 2013
Posts
36
Reaction score
6
Habari wana MMU? Nilikuwa na mpenzi wangu ambaye tulikuwa tunapendana sana na tulipanga Mungu akijaalia tufunge ndoa mwaka huu mwishoni. Sasa leo ameniandikia meseji akiniambia Mama yake amemwambia hawezi kunioa mimi kwa sababu sio wa kabila lake, na yeye kasema hawezi kuacha kumtii mama yake.

Ameniomba tuachane na hivi sasa mama yake amemuunganishia kwa msichana mwingine ambaye ni kabila lao. Hapa nawaza na kuwazua hivi naanza mahusiano na nani? Wanaume wote sio kanisani, ofisini walikuwa wanafahamu mahusiano yetu na waliyaheshimu. Leo hii naanzaje kusema niko single? Ndoto ya kuolewa naona imepaa.

Naombeni ushauri wenu wana MMU, haya mambo yamenichanganya sana.
 
huyo kachoka kukugegeda bwana...kwani mwazoni alikuwa hajui kuwa mama hapendi kabila lako....wanaume wabaya acha tuu
kubali kuwa umetumika move on na utapata mume kamili ila usikae ukafanya kosa la kutoa papuchi kabla ya kuuliza mambo ya dini na kabila na mtazamo wa huyo mwanaume
 
Dunia ndio ilivyo, lilishanikuta hili, kweli inauma lakini utafanyaje???waweza jihisi una gundu vile lakini usiwaze hivyo! piga moyo konde songa mbele, Mungu atakuletea wa kwako ambae ni wa ukweli. Hilo gume gume nalo mpaka linakutongoza lilikuwa halijui mama yake hataki makabila mengine??
 
huyo kachoka kukugegeda bwana...kwani mwazoni alikuwa hajui kuwa mama hapendi kabila lako....wanaume wabaya acha tuu
kubali kuwa umetumika move on na utapata mume kamili ila usikae ukafanya kosa la kutoa papuchi kabla ya kuuliza mambo ya dini na kabila na mtazamo wa huyo mwanaume

Kweli kabisa, mpaka anakula na kupakua hakujua kuwa mama hataki kabila la mdada?huyo mkaka ni mngese sana
 
Duuuh dunia ina maajabu yake yani hadi leo wazazi wanawatafutia wana wake wa kuoa! Pole sana binti, dunia ina watu wengi wala usivunjike moyo hayo ni mapito wala hakuwa wako, muda utafika utapa wa kukuoa wala usiangalie watu watasema nini unatakiwa ujali furaha yako!
++++++++++++++++++++++++++
Naomba nikuulize swali!
Ina maana ulikuwa hujawai kutambulishwa kwao huyo mchumba wako? Maana hila la kabila mbona kama umechelewa kulijua?
Pengine huyo jamaa alikuwa anajua fika hila alihamua kukupotezea muda!
Pole sana!
 
huyo kachoka kukugegeda bwana...kwani mwazoni alikuwa hajui kuwa mama hapendi kabila lako....wanaume wabaya acha tuu
kubali kuwa umetumika move on na utapata mume kamili ila usikae ukafanya kosa la kutoa papuchi kabla ya kuuliza mambo ya dini na kabila na mtazamo wa huyo mwanaume

Asante, unayosema yanawezekana. Mwanzo aliniambia mama yake anapenda aoe kabila lake, lakini kwa sababu yeye ndio kapenda na yeye ndio muoaji hata teteleka. Alikuwa ananipa matumaini na nilimwamini sana, nimeshtushwa na huu ujumbe leo.
 
Habari wana MMU? Nilikuwa na
mpenzi wangu ambaye tulikuwa tunapendana sana na tulipanga Mungu
akijaalia tufunge ndoa mwaka huu mwishoni. Sasa leo ameniandikia meseji
akiniambia Mama yake amemwambia hawezi kunioa mimi kwa sababu sio wa
kabila lake, na yeye kasema hawezi kuacha kumtii mama yake.

Ameniomba tuachane na hivi sasa mama yake amemuunganishia kwa msichana
mwingine ambaye ni kabila lao. Hapa nawaza na kuwazua hivi naanza
mahusiano na nani? Wanaume wote sio kanisani, ofisini walikuwa
wanafahamu mahusiano yetu na waliyaheshimu. Leo hii naanzaje kusema niko
single? Ndoto ya kuolewa naona imepaa.

Naombeni ushauri wenu wana MMU, haya mambo yamenichanganya sana.

nami niko single sijali kabila tuwacliane
 
Duuuh dunia ina maajabu yake yani hadi leo wazazi wanawatafutia wana wake wa kuoa! Pole sana binti, dunia ina watu wengi wala usivunjike moyo hayo ni mapito wala hakuwa wako, muda utafika utapa wa kukuoa wala usiangalie watu watasema nini unatakiwa ujali furaha yako!
Pole sana!

Asante sana. Hata mimi sikuwahi kuamini kama tofauti ya kabila ni kitu ambacho kinaweza achanisha wawili waliopendana. Kila nikitafakari natamani ingekuwa ndoto lakini ndio ukweli wenyewe.
 
Be strong go back to college .success is the best revange utamsahau vibaya halafu ukijakuangalia nyuma utajiuliza hivi nililala na hili jitu

Asante Natalia... Hayo mawazo nitayapata baadae, saivi niko kwenye maumivu ambayo ni makali sana. Ni bora ningekuwa binti mdogo, mimi ni mdada mkubwa hata sihitaji shule tena.
 
Hapa inaonesha huyu jamaa ana mchezea akili tuu na ukuta hata mother hajui hizo ishu na hajasema, sema jamaa kamchoka na katumia hiyo njia kumkimbiza!

huyo kachoka kukugegeda bwana...kwani mwazoni alikuwa hajui kuwa mama hapendi kabila lako....wanaume wabaya acha tuu
kubali kuwa umetumika move on na utapata mume kamili ila usikae ukafanya kosa la kutoa papuchi kabla ya kuuliza mambo ya dini na kabila na mtazamo wa huyo mwanaume
 
pole we mamito, wanaume ndivyo walivyo hana lolote huyo alikua anataka kipochi manyoya chako basi any way ushauri wa bure achana na vijajana date na wazee shost hutalia labda ukute ambae hajielewi lakini vijana wengi wao ni pasua kichwa tu
 
Pole sana na wewe! Unajua huyu jamaa katumia hiyo njia kumkimbiza tu kwani mahusiano yao haya kuanza leo, kwanini hakumwambia toka mwanzo?

Dunia ndio ilivyo, lilishanikuta hili, kweli inauma lakini utafanyaje???waweza jihisi una gundu vile lakini usiwaze hivyo! piga moyo konde songa mbele, Mungu atakuletea wa kwako ambae ni wa ukweli. Hilo gume gume nalo mpaka linakutongoza lilikuwa halijui mama yake hataki makabila mengine??
 
You will be fine. Nothing heals a broken heart like time, love and tenderness.
Look on the brighter side sweetie. He did not stand you up at the altar, hajakuacha na uja uzito, etc. Pole.
 
Pole sana piga moyo konde!

Ina maana haukuwai kwenda kwao kutambulishwa?
Asante sana. Hata mimi sikuwahi kuamini kama tofauti ya kabila ni kitu ambacho kinaweza achanisha wawili waliopendana. Kila nikitafakari natamani ingekuwa ndoto lakini ndio ukweli wenyewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom