1. Nashangaa na kutaka kujua ni nani aliyewafanya baadhi ya wana ccm kuwa na maneno ya kihuni? Kwa mfano; nimejaribu kutafakari kuhusu maneno ya "Musukuma" (Mwenyekiti wa ccm mkao wa Geita) nashindwa kuelewa kama kweli huyo ni kiongozi mkubwa wa chama na mgombea ubunge! Nimejaribu kuuliza watu kama Wasukuma na Wamasai ni watani, nikambiwa sivyo (hata utani wa makabila unazungumzia vitu/tabia za asili za jamii husika sio matusi kwa mtu mmoja mmoja). Japokuwa nampongeza Mh. Lowasa na UKAWA kwa ujumla kutojibu yale maneno ya kifedhuli ya kijana "Musukuma", lakini ni muhimu tukemee vitendo hivyo. Nionavyo mimi mpaka sasa bado hatujampata raisi wa nchi kwa maana hiyo anaweza akashinda yeyote kati ya Mh. Lowasa au Mh. Magufuli, hivyo hata kama tunataka vyama vyetu vishinde ili kupata maslahi fulani binafsi ni vizuri tutumie maneno yasiyo ya kifedhuli tunapokua majukwaani. Matusi hayo yanadakwa na vyombo vya habari vya nje hivyo kudhalilisha utu wetu. Hivi ccm ni nani kawafundisha matusi, maana asilimia kubwa ya wapiga debe wa ccm wapandapo jukwaani badala ya kuzunguzia sera huwa ni kumtukana Mh. Lowasa tu. Pamoja na kasoro za hapa na pale nampongeza sana Mh. Magufuli amejitahidi sana kukwepa kuongea matusi akiwa jukwaani, wakati mwingine natamani hata wangemwachia peke yake ndio aongee jukwaani. Lakini mshangao unapungua kwa sababu hata mtu aliyewahi kuwa kiongozi mkubwa wa chama (katibu mkuu) alipokua anamnadi Mh. Magufuli mjini Morogoro aliporomosha matusi na shutuma tu kwa Mh. Lowasa bila kusema nini kama chama walikifanya ili kuwapa Imani wananchi kuhusu mwenendo wa chama hicho na serikari yake.
2. Nashangaa tena kuhusu mikakati ya Mh. Magufuli kwamba akishinda uraisi atanzisha mahakama ya Mafisadi. Nashangaa kwa sababu ni wazi kwamba hakuna fisadi kijana ambaye anafanya ufisadi wa kutisha (labda wale waliobebwa mgongoni na wazazi wao au ndugu zao). Mafisadi wengi ni wale ambao walitakiwa kuwa wamestaafu lakini bado wanang'ang'ania madaraka kwa sababu hawawezi kufanya biashara nzuri ya kujilimbikizaia mali wakiwa nje ya mfumo wa serikali. Hivi Mh. Magufuli anatuambia kwamba hao wanaompeleka Ikulu ndio atawaundia mahakama ya mafisadi? Nijuavyo ufisadi una sura kuu mbili; moja ni kufanya ufisadi wenyewe na pili ni kunyamazia bila kuwachukulia hatua wale wanaofanya ufisadi (ndio maana watu wanafungwa kwa kutowajibika vizuri). Labda mahakama hiyo itakua kwa ajili ya Mh. Lowasa kama ccm wanavyotuaminisha kwamba ndiye fisadi pekee nchini na ndio maana wanasema kuondoka kwa Lowasa ccm chama kimekua safiii!
3. Nashangaa pia kuwa sijui imetokeaje kwamba wagombea hawa wawili maarufu yaani Mh. Magufuli na Mh. Lowasa nawalinganisha kwa vitu viwili. Moja, wote wawili wanapenda sana kufanya maamuzi kwa kupigiwa makofi (Kiswahili cha mtaani tunasema wanapenda masifa). Hivyo ni vizuri wakashauriwa kupunguza hiyo tabia. Kwa hapa tulipofikia hatuhitaji kiongozi wa kupenda kupigiwa makofi kwa ajili ya umaaru wa kijinga. Tunataka mtu ambaye anamtazamo wa mbele na mpana kwa maslahi ya nchi kiasi kwamba hata akituambia tunafunga mikanda amaanishe hivyo na kila mtu ajifunge mkanda wake akiwemo mwenyewe. Wanasiasa kupenda kupigiwa makofi ndio kumetufikisha hapa na kuwa Taifa la wababaishaji. Nakumbaka Mh. Clean wakati anaingia madarakani ndani ya miaka mitano ya awamu yake ya kwanza alifanya kazi bila kupenda kupigiwa makofi na kazi yake ilonekana. Lakini baadaye naye akabadilika na kuanza kupenda kupigiwa makofi na kupenda kusifiwa ndio matokeo yake tuliyaona mwishoni mwa kipindi chake cha uraisi.
Hawa watu wawili pia wanafanana kwa kufanya maamuzi magumu. Natoa mfano mmoja mmoja kwa kila mtu. Nakumbuka Mh. Magufuli akijua fika kwamba biashara ya Molori yanayoharibu barabara ni ya watu wazito au wanamahusiano na viongozi wazito; akatoa amri ya kupunguza uzito wa mizigo inayoyobebwe na malori hayo kwa ajili ya kunusuri uharibifu wa barabara zetu. Wote tunajua kilichotokea kuhusu wakubwa wake kumwamrisha asitishe hilo zoezi. Japokuwa uamuzi wake haukuzingitia mazingira ya kutokuwa na njia mmbadala na fanisi (kama reli) ya kusafirisha mizigo kwenda mikoani na nchi jirani, lakini nilimpongeza kwa kufanya maamuzi magumu. Wataalamu wanasema ni bora kufanya maamuzi kwa nia njema yenye matokea mabaya kuliko kutofanya maamuzi kabisa (maana yake ni kwamba utakua na mahali pa kuanzia ili kurekebisha mambo). Nije kwa Mh. Lowasa; pamoja na maamuzi mengine magumu aliyofanya, kubwa kuliko yote ni kuhama ccm na kijiunga na Chadema/UKAWA. Haya ni maamuzi magumu sana ukizingitia jinsi dude linaloitwa ccm kujijengea mfumo wa kuogopesha walio ndani kutoka. Kabla ya ccm kumkata kwenye mchakato wao, watu wengi nikiwemo mimi niliona salama ya Mh. Lowasa hata kama atakatwa ni kubaki ndani ya ccm (kutokana na kashfa zilizokua zinamwandama). Nisema ukweli kwamba nilikua miongoni wa watu ambao walikua hawampendi Mh. Lowasa, lakini baada ya kufanya maamuzi hayo magumu sana ghafla nikatokea kumkubali kwa kuamini kwamba ni mtu ambaye anafaa kuwa raisi kwa kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi magumu ambapo alikubali kukorofishana na marafiki zake wengi wa muda mrefu kwa uamuzi wake huo. Watu watasema alihama kwa sababu anapenda madara; inawezekana ni kweli lakini tujiulize kama kuna mwanasiasa ambaye hapendi madaraka. Kwa nchi za kwetu mtu yeyote anayeingia kwenye siasa anatafuta madaraka, hivyo ukiwa mwanasiasa lazima ulenge kuwa kiongozi wa ngazi yoyote. Wengi wanapenda madaraka lakini sio jasiri. Ukitaka kujua kuwa kwa uamuzi huo Mh. Lowasa ni jasiri jaribu kumuuliza Mh. Sitta nini alifanya (alingia mitini) wakati ametendwa ndani ya ccm hivyo Chadema walimuomba afanye maamuzi magumu. Wengine watasema mbona hata Mh. Mrema alifanya hivyo; ni kweli alifanya hivyo lakini mazingira ni tofauti sana. Kwanza hakuwa na kashfa zinazomzunguka (zinaweza kuwa na kweli au uzushi) hivyo hakutegemaea kupigwa mawe sana na chama chake cha zamani, pia kulikua na tetesi (za kweli au uongo) kwamba ilikua ni mbinu ya ccm kudhoofisha vyama vya upinzani (hasa Chedema) ili kuvuruga mfumo wa upinzani ulioanza kujengeka wakati ule.
4. Nashangaa pia kuwa Wazee wa ccm wameng'ang'ania madaraka (hawataki kung'atuka) nadhani bado hawajawamini vijana kama wanaweza kuongoza. Na hawa wazee watakaposhindwa kufanya kazi kwa sababu ya uzee ni wazi kwamba chama kitakufa kifo cha mende. Hivi kuna kijana gani ameshika madaraka makubwa? Ni wachache sana ambao miongoni mwao ni wachache sana wanaojitambua, wengi ndio hao waendesha propaganda, watukanaji na waongolea kashfa za Lowasa tu. Wengine watasema kuna mashirika mengi ya umma au mamlaka za umma zinaongozwa na vijana. Je unafahamu wenyeviti wa Bodi na wajumbe wao ambao ndio watunga sera wa mashirika hayo au mamlaka hizo ni wa namna gani? Tunataka vijana wapewe nafasi ya kuongoza baadhi ya mashirika ya umma au mamlaka za umma kuanzia ukurugenzi mpaka wenyeviti wa Bodi na pawepo na mzee mmoja au wawili wa kutoa ushauri tu
5. Nashangaa kuona tuna matatizo makubwa ya elimu ya uraia hata kwa wenye elimu ya darasani. Ili kudhihirisha hilo natoa mifano miwili mifupi. Moja ni kwamba watu wengi wanashindwa kutofautisha serikali na chama, hii inasabisha watumishi wengi wa umma kudhani kwamba ccm isiposhinda na wao watakua hawana kazi. Hata uwambie vipi kwamba mtumishi wa umma anatakiwa kuwa tayari kutumikia serikali yoyote itakayokuwa madarakani (mbali na nafasi za kisiasa) hivyo anatakiwa apige kura kuchagua serikali ambayo anaona itasaidia utendaji wake wa kazi kuwa na ufanisi, kakini walio wengi bado wanakua na wasiwasi na hawaelewi. Pili, utakuta mtu msomi anakua na mawazo ya ajabu ajabu ati vyama vyote vinafanana hivyo hata chama kingine kikichukua madaraka mambo yatakua yaleyale. Maneno hayo ni sawa na kusema mchezaji fulani akikosa penati basi mashabiki wanasema hata angepewa mcezaji mwingine penati hiyo pia angekosa. Watanzania tumekua watu wa kuishi kwa kudhania tu, hata kama tuna elimu zetu bado hazitusaidii. Mfano, kocha mzuri ni yule anayempa nafasi ya kucheza yule anayechonga sana ili akishindwa kucheza vizuri asiweze kuchonga tena. Mpe mtu nafasi, akishindwa ndio upate nafasi ya kumshusha daraja.
6. Nashangaa kuona watu hawatambui kwamba Mh. Lowasa wa ccm sio Lowasa wa Chadema/UKAWA. Ni wazi kwamba uraisi ni tasisi wala sio mtu mmoja. Uraisi ni timu (team work) ambapo maamuzi makubwa hayafanywi na mtu mmoja. Ikitokea Mh. Lowasa ameshinda uraisi halafu uendeshaji wake wa serikali ukawa ni vile vile alivyokua ccm, kwa upande wangu sitamlaumu Lowasa ila nitawalaumu UKAWA kuwa ndio dhaifu. Nina Imani Mh. Lowasa alivyohamia Chadema/Ukawa lazima afuate misingi na matakwa ya vyama hivyo. Tutakapoona mambo yaleyale yaliyokua yanafanyika kwenye chama cha zamani yakaendeleakufanyika ndani ya UKAWA basi hatutasita kuirejesha tena madarakani ccm, na ccm ikirudi madaraka haitakua ile ya zamani maana lazima watakua wamejipanga vizuri na kujirekebisha. Kwa wale wapenzi wa mpira wa miguu niwape mifano miwili inayoakisi namna ambavyo mazingira yanayomzunguka mtu yanamfanya awe mzuri au sio mzuri; moja ni mchezaji Andriy Shevchenko alipokua AC Milan alikua mchezaji wa kutumainiwa lakini alipokwenda Chelsea (sijui Morinho alimfanya nini) akawa butu. Kwa upande mwingine, mfano wa pili ni Arjen Robben, alipokuwa Chelsea alikua mchezaji wa kawaida sana lakini sasa yupo B. Munich ni mchezaji wa kutegemewa, hivyo mazingiza na watu wanaokuzunguka wanakufanya uwe mzuri au wa hovyo.
7. Nashangaa kuona kwamba tusipokua makini uchaguzi huu utatuacha na vidonda vya ukabila. Wanaojua mambo nadhani wamenielewa
Mwenyezi Mungu tunaomba ibariki Tanzania, utuongoze tufanya uchaguzi kwa Amani na utulivu na haki ikatendeke.
2. Nashangaa tena kuhusu mikakati ya Mh. Magufuli kwamba akishinda uraisi atanzisha mahakama ya Mafisadi. Nashangaa kwa sababu ni wazi kwamba hakuna fisadi kijana ambaye anafanya ufisadi wa kutisha (labda wale waliobebwa mgongoni na wazazi wao au ndugu zao). Mafisadi wengi ni wale ambao walitakiwa kuwa wamestaafu lakini bado wanang'ang'ania madaraka kwa sababu hawawezi kufanya biashara nzuri ya kujilimbikizaia mali wakiwa nje ya mfumo wa serikali. Hivi Mh. Magufuli anatuambia kwamba hao wanaompeleka Ikulu ndio atawaundia mahakama ya mafisadi? Nijuavyo ufisadi una sura kuu mbili; moja ni kufanya ufisadi wenyewe na pili ni kunyamazia bila kuwachukulia hatua wale wanaofanya ufisadi (ndio maana watu wanafungwa kwa kutowajibika vizuri). Labda mahakama hiyo itakua kwa ajili ya Mh. Lowasa kama ccm wanavyotuaminisha kwamba ndiye fisadi pekee nchini na ndio maana wanasema kuondoka kwa Lowasa ccm chama kimekua safiii!
3. Nashangaa pia kuwa sijui imetokeaje kwamba wagombea hawa wawili maarufu yaani Mh. Magufuli na Mh. Lowasa nawalinganisha kwa vitu viwili. Moja, wote wawili wanapenda sana kufanya maamuzi kwa kupigiwa makofi (Kiswahili cha mtaani tunasema wanapenda masifa). Hivyo ni vizuri wakashauriwa kupunguza hiyo tabia. Kwa hapa tulipofikia hatuhitaji kiongozi wa kupenda kupigiwa makofi kwa ajili ya umaaru wa kijinga. Tunataka mtu ambaye anamtazamo wa mbele na mpana kwa maslahi ya nchi kiasi kwamba hata akituambia tunafunga mikanda amaanishe hivyo na kila mtu ajifunge mkanda wake akiwemo mwenyewe. Wanasiasa kupenda kupigiwa makofi ndio kumetufikisha hapa na kuwa Taifa la wababaishaji. Nakumbaka Mh. Clean wakati anaingia madarakani ndani ya miaka mitano ya awamu yake ya kwanza alifanya kazi bila kupenda kupigiwa makofi na kazi yake ilonekana. Lakini baadaye naye akabadilika na kuanza kupenda kupigiwa makofi na kupenda kusifiwa ndio matokeo yake tuliyaona mwishoni mwa kipindi chake cha uraisi.
Hawa watu wawili pia wanafanana kwa kufanya maamuzi magumu. Natoa mfano mmoja mmoja kwa kila mtu. Nakumbuka Mh. Magufuli akijua fika kwamba biashara ya Molori yanayoharibu barabara ni ya watu wazito au wanamahusiano na viongozi wazito; akatoa amri ya kupunguza uzito wa mizigo inayoyobebwe na malori hayo kwa ajili ya kunusuri uharibifu wa barabara zetu. Wote tunajua kilichotokea kuhusu wakubwa wake kumwamrisha asitishe hilo zoezi. Japokuwa uamuzi wake haukuzingitia mazingira ya kutokuwa na njia mmbadala na fanisi (kama reli) ya kusafirisha mizigo kwenda mikoani na nchi jirani, lakini nilimpongeza kwa kufanya maamuzi magumu. Wataalamu wanasema ni bora kufanya maamuzi kwa nia njema yenye matokea mabaya kuliko kutofanya maamuzi kabisa (maana yake ni kwamba utakua na mahali pa kuanzia ili kurekebisha mambo). Nije kwa Mh. Lowasa; pamoja na maamuzi mengine magumu aliyofanya, kubwa kuliko yote ni kuhama ccm na kijiunga na Chadema/UKAWA. Haya ni maamuzi magumu sana ukizingitia jinsi dude linaloitwa ccm kujijengea mfumo wa kuogopesha walio ndani kutoka. Kabla ya ccm kumkata kwenye mchakato wao, watu wengi nikiwemo mimi niliona salama ya Mh. Lowasa hata kama atakatwa ni kubaki ndani ya ccm (kutokana na kashfa zilizokua zinamwandama). Nisema ukweli kwamba nilikua miongoni wa watu ambao walikua hawampendi Mh. Lowasa, lakini baada ya kufanya maamuzi hayo magumu sana ghafla nikatokea kumkubali kwa kuamini kwamba ni mtu ambaye anafaa kuwa raisi kwa kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi magumu ambapo alikubali kukorofishana na marafiki zake wengi wa muda mrefu kwa uamuzi wake huo. Watu watasema alihama kwa sababu anapenda madara; inawezekana ni kweli lakini tujiulize kama kuna mwanasiasa ambaye hapendi madaraka. Kwa nchi za kwetu mtu yeyote anayeingia kwenye siasa anatafuta madaraka, hivyo ukiwa mwanasiasa lazima ulenge kuwa kiongozi wa ngazi yoyote. Wengi wanapenda madaraka lakini sio jasiri. Ukitaka kujua kuwa kwa uamuzi huo Mh. Lowasa ni jasiri jaribu kumuuliza Mh. Sitta nini alifanya (alingia mitini) wakati ametendwa ndani ya ccm hivyo Chadema walimuomba afanye maamuzi magumu. Wengine watasema mbona hata Mh. Mrema alifanya hivyo; ni kweli alifanya hivyo lakini mazingira ni tofauti sana. Kwanza hakuwa na kashfa zinazomzunguka (zinaweza kuwa na kweli au uzushi) hivyo hakutegemaea kupigwa mawe sana na chama chake cha zamani, pia kulikua na tetesi (za kweli au uongo) kwamba ilikua ni mbinu ya ccm kudhoofisha vyama vya upinzani (hasa Chedema) ili kuvuruga mfumo wa upinzani ulioanza kujengeka wakati ule.
4. Nashangaa pia kuwa Wazee wa ccm wameng'ang'ania madaraka (hawataki kung'atuka) nadhani bado hawajawamini vijana kama wanaweza kuongoza. Na hawa wazee watakaposhindwa kufanya kazi kwa sababu ya uzee ni wazi kwamba chama kitakufa kifo cha mende. Hivi kuna kijana gani ameshika madaraka makubwa? Ni wachache sana ambao miongoni mwao ni wachache sana wanaojitambua, wengi ndio hao waendesha propaganda, watukanaji na waongolea kashfa za Lowasa tu. Wengine watasema kuna mashirika mengi ya umma au mamlaka za umma zinaongozwa na vijana. Je unafahamu wenyeviti wa Bodi na wajumbe wao ambao ndio watunga sera wa mashirika hayo au mamlaka hizo ni wa namna gani? Tunataka vijana wapewe nafasi ya kuongoza baadhi ya mashirika ya umma au mamlaka za umma kuanzia ukurugenzi mpaka wenyeviti wa Bodi na pawepo na mzee mmoja au wawili wa kutoa ushauri tu
5. Nashangaa kuona tuna matatizo makubwa ya elimu ya uraia hata kwa wenye elimu ya darasani. Ili kudhihirisha hilo natoa mifano miwili mifupi. Moja ni kwamba watu wengi wanashindwa kutofautisha serikali na chama, hii inasabisha watumishi wengi wa umma kudhani kwamba ccm isiposhinda na wao watakua hawana kazi. Hata uwambie vipi kwamba mtumishi wa umma anatakiwa kuwa tayari kutumikia serikali yoyote itakayokuwa madarakani (mbali na nafasi za kisiasa) hivyo anatakiwa apige kura kuchagua serikali ambayo anaona itasaidia utendaji wake wa kazi kuwa na ufanisi, kakini walio wengi bado wanakua na wasiwasi na hawaelewi. Pili, utakuta mtu msomi anakua na mawazo ya ajabu ajabu ati vyama vyote vinafanana hivyo hata chama kingine kikichukua madaraka mambo yatakua yaleyale. Maneno hayo ni sawa na kusema mchezaji fulani akikosa penati basi mashabiki wanasema hata angepewa mcezaji mwingine penati hiyo pia angekosa. Watanzania tumekua watu wa kuishi kwa kudhania tu, hata kama tuna elimu zetu bado hazitusaidii. Mfano, kocha mzuri ni yule anayempa nafasi ya kucheza yule anayechonga sana ili akishindwa kucheza vizuri asiweze kuchonga tena. Mpe mtu nafasi, akishindwa ndio upate nafasi ya kumshusha daraja.
6. Nashangaa kuona watu hawatambui kwamba Mh. Lowasa wa ccm sio Lowasa wa Chadema/UKAWA. Ni wazi kwamba uraisi ni tasisi wala sio mtu mmoja. Uraisi ni timu (team work) ambapo maamuzi makubwa hayafanywi na mtu mmoja. Ikitokea Mh. Lowasa ameshinda uraisi halafu uendeshaji wake wa serikali ukawa ni vile vile alivyokua ccm, kwa upande wangu sitamlaumu Lowasa ila nitawalaumu UKAWA kuwa ndio dhaifu. Nina Imani Mh. Lowasa alivyohamia Chadema/Ukawa lazima afuate misingi na matakwa ya vyama hivyo. Tutakapoona mambo yaleyale yaliyokua yanafanyika kwenye chama cha zamani yakaendeleakufanyika ndani ya UKAWA basi hatutasita kuirejesha tena madarakani ccm, na ccm ikirudi madaraka haitakua ile ya zamani maana lazima watakua wamejipanga vizuri na kujirekebisha. Kwa wale wapenzi wa mpira wa miguu niwape mifano miwili inayoakisi namna ambavyo mazingira yanayomzunguka mtu yanamfanya awe mzuri au sio mzuri; moja ni mchezaji Andriy Shevchenko alipokua AC Milan alikua mchezaji wa kutumainiwa lakini alipokwenda Chelsea (sijui Morinho alimfanya nini) akawa butu. Kwa upande mwingine, mfano wa pili ni Arjen Robben, alipokuwa Chelsea alikua mchezaji wa kawaida sana lakini sasa yupo B. Munich ni mchezaji wa kutegemewa, hivyo mazingiza na watu wanaokuzunguka wanakufanya uwe mzuri au wa hovyo.
7. Nashangaa kuona kwamba tusipokua makini uchaguzi huu utatuacha na vidonda vya ukabila. Wanaojua mambo nadhani wamenielewa
Mwenyezi Mungu tunaomba ibariki Tanzania, utuongoze tufanya uchaguzi kwa Amani na utulivu na haki ikatendeke.