Kwanza habari zenu wadau,,kiukweli mi nahisi saikolojia yangu imevurugika,..Nilipokuwa mdogo nilikuwa mtundu sana,sasa mama alikuwa akinipa dozi ya kichapo kama mbwa mwizi,,ilifikia hatua akawa ananiwekea kisu shingoni kama anataka kunichinja,,nilikuwa nakung'utwa soli za viatu mpaka basi,,amekuwa akinitamkia maneno makali sana hata nikikosea kitu kidogo tangu nikiwa mdogo hadi nikiwa mkubwa,, sasa nimekuwa bila amani na mamaangu,,na kadri siku zinavyozidi kwenda ndo nazidi kukosa aman na ule upendo wa kutoka moyoni haupo tena kisana kwa mama angu kiasi hata kummisi inakuwa ngumu sana,,,najua hakuna kama mama,najitahidi niishinde hiyo hali lakini nashindwa,,naombeni mnishauri njia ya kuurejesha moyo wangu kwenye hali ya kawaida..[HASHTAG]#Nishaurini[/HASHTAG]..