Nimeambiwa ni Jinamizi!!

Columbus

JF-Expert Member
Nov 5, 2010
2,002
648
Kuna dhana kwamba ukiwa umelala usiku ukakajikuta umekabwa na kushindwa kabisa kujisogeza ni kutokana na jinamizi, hili jinamizi ni nini au kuna sababu za kiafya zinazosababisha hali hiyo? je kuna namna yoyote ya kujiepusha au kuna dawa ya kutibu hali hiyo isikutokee? msaada wetu tafadhali.
 
Heart Failure mkuu hiyo. Hakuna jina mizi wala nini. Ukiona hivyo nenda hospital na utapata matibabu mazuri na kujikuta upo ok mkuu.
 
Jinamizi, ni neno linalotumika kwa waginjwa au watu fulani kutaka kueleza jinsi anavyo "kabwa" wakati akilala usiku!!

Neno la kiingereza huitwa Breathlessness na lile la kitaalamu huitwa "Paroxysmal Nocturnal Dyspnea" (PND)

Hii hutokea pale kunapokuwa hakuna uwiano sawa kati ya damu inayozunguka mwili hasa itokayo na kwenda katika mapafu( Pulmonary Circulation) na Upumuaji wa hewa ya Oxygen..

Mkandamizo/Shinikizo(Pressure/Tension) unapokuwa mkubwa katika uwiano huu hasa kwa watu wenye magonjwa mengine tayari mfano moyo, mapafu, ini, figo pia uzee, n.k husababisha damu kurudi katika mapafu badala ya kuendelea na mzunguko wake wa kawaida...na kwa vile mapafu hutumika kwa kupumulia(Breathing), maji au damu yanapokuwa yakijaa husababisha mtu kushindwa kupumua vizuri, na wagonjwa/watu wengi husema "NIMEKABWA NA JINI ila baada ya kufungua madirisha liliondoka"...
Watu wengi husema hivyo kwa sababu mtu ukisimama mkandamizo ni mkubwa na hivyo kulazimisha kutoka katika mapafu kwenda katika moyo, na ile damu kidogo inayobaki due to gravity haileti madhara..lakini pale mtu anapolala tena, mzunguko ule ule hutokea na hivyo kufanya mtu kushindwa kulala, ..kutumia mito(pillows) husaidia katika hali hii, lakini ikumbukwe kwamba the more the pillows the worse the condition.

MUHIMU: Hali hii PND, "Kukabwa na jinamizi" hutokea na dalili nyingine kama kuchoka haraka,(katika kupanda ngazi, kutembea mwendo mfupi), mapigo ya moyo kwenda kasi, kusikia kizunguzungu n.k ila watu wengi hupuuzia kwani huona ni jambo la kawaida hadi pale hali inapokuwa mbaya kwa kushindwa kulala na hivyo kwenda hospitali..

Ushauri: Ni vema kuwahi HOSPITALI hali hii inapojitokeza.
 
Jinamizi, ni neno linalotumika kwa waginjwa au watu fulani kutaka kueleza jinsi anavyo "kabwa" wakati akilala usiku!!

Neno la kiingereza huitwa Breathlessness na lile la kitaalamu huitwa "Paroxysmal Nocturnal Dyspnea" (PND)

Hii hutokea pale kunapokuwa hakuna uwiano sawa kati ya damu inayozunguka mwili hasa itokayo na kwenda katika mapafu( Pulmonary Circulation) na Upumuaji wa hewa ya Oxygen..

Mkandamizo/Shinikizo(Pressure/Tension) unapokuwa mkubwa katika uwiano huu hasa kwa watu wenye magonjwa mengine tayari mfano moyo, mapafu, ini, figo pia uzee, n.k husababisha damu kurudi katika mapafu badala ya kuendelea na mzunguko wake wa kawaida...na kwa vile mapafu hutumika kwa kupumulia(Breathing), maji au damu yanapokuwa yakijaa husababisha mtu kushindwa kupumua vizuri, na wagonjwa/watu wengi husema "NIMEKABWA NA JINI ila baada ya kufungua madirisha liliondoka"...
Watu wengi husema hivyo kwa sababu mtu ukisimama mkandamizo ni mkubwa na hivyo kulazimisha kutoka katika mapafu kwenda katika moyo, na ile damu kidogo inayobaki due to gravity haileti madhara..lakini pale mtu anapolala tena, mzunguko ule ule hutokea na hivyo kufanya mtu kushindwa kulala, ..kutumia mito(pillows) husaidia katika hali hii, lakini ikumbukwe kwamba the more the pillows the worse the condition.

MUHIMU: Hali hii PND, "Kukabwa na jinamizi" hutokea na dalili nyingine kama kuchoka haraka,(katika kupanda ngazi, kutembea mwendo mfupi), mapigo ya moyo kwenda kasi, kusikia kizunguzungu n.k ila watu wengi hupuuzia kwani huona ni jambo la kawaida hadi pale hali inapokuwa mbaya kwa kushindwa kulala na hivyo kwenda hospitali..

Ushauri: Ni vema kuwahi HOSPITALI hali hii inapojitokeza.

JF naendelea kuikubali siku hadi siku, imekuwa chanzo cha maarifa.Asante sana Mkuu!
 
dawa yake lala na mfupa wa nguruwe hapo chini ya kitanda : anyway jinamizi si ilo hapo kwenye avatar yako?
 
Kule kwetu Katavi enzi zile nakua ni kwamba ukiota unakabwa kusema ukweli wanadai kuwa unakuwa umewangiwa.So dawa pekee niliyoambiwa na babu yangu ni kwamba ukijinyosha ukagusa ukuta au ukagusa mtu ulielala nae hapo hapo hiyo hali inatoweka.And this is proved kwa sababu mimi ikinitokea nikiweza kunyosha mkono na kushika ukuta au kumshika nilielala nae basi kwisha habari ya jinamizi
 
Back
Top Bottom