Niliyoyafanya katika msiba wa Bibi

Niliyoyafanya katika msiba wa Bibi

Daktari wa Meno

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2019
Posts
509
Reaction score
1,617
Bibi yangu aliyekuwa rafiki yangu mkubwa na mshauri ulipotangulia mbele za haki na akaniacha na maumivu makubwa sana. Ukiwa uliisha ila chuki yangu na mjomba imekuwa kubwa mara baada ya msiba wake.

Bibi alipofariki mjomba alikuwa Dar, yeye ndiye kijana mkubwa wa kiume kwa bibi ila mama ndiye mtoto wa kwanza kwa Bibi hivyo mimi pia ni mjukuu wa kwanza kwa bibi, alinipenda sana japo kijana wake hatuelewani sana (mjomba) baada ya bibi kufariki mjomba akapigiwa simu akataka tumpeleke bibi mochwari ili aje kumzika. Kama kawaida nilikuwa mratibu wa mipango yote ya bibi kwenda mochwari mimi ndiye nilitafuta gari mwenyewe ila pesa alikuwa analipia mjomba.

Basi mjomba akafika nyumbani akataka mwili wa Bibi ufuatwe kwa ajili ya mazishi na kwa vile mimi ndiye nilijua nilipoupeleka nikakaa kimya kuona nani ataenda kuufuata. Mjomba akasema anaenda yeye na marafiki zake kutoka Dar nikamuuliza anajua mwili ulipo akasema hajui, nikamwambia basi kaa nyumbani niende mimi. Eti ile kauli ikampa hasira, nikasema kwa vile yeye ni mtu mzima nitampa heshima zake pia sitamuudhi kwani yupo katika majonzi makubwa.

Mjomba alinitaka nije na mtu wa kurekodi video na picha ili aweke kumbukumbu ya tukio hilo kubwa katika maisha yake. Basi nikaenda nikachukua bibi mochwari nikatafuta mtu wa video akanirekodi pale mochwari wakati nafanya mipango ya kurudi nyumbani na mwili akanirekodi sana nikatazama video nikaona amerekodi vizuri basi tukawasha gari yeye akiwa kwenye gari nyingine mbele anaendelea kunirekodi.

Tukafika kijijini nikasimama karibu na nyumbani nikamtaka anirekodi akanirekodi ndipo tukaenda msibani sasa, maana nyumbani na msibani siyo mbali sana, tumefika karibu na msiba nikamwambia yule mtu wa video atarekodi watu ambao mimi nitamwonesha tu kama sijamwonesha asirekodi basi nikamwonesha Mama, mdogo wangu, rafiki yangu yule niliyempiga, kuna dada mmoja nilikuwa namtongoza naye nikamwambia amrekodi na shangazi zangu wawili pia.

Basi tukafanya shughuli zote na muda wa kuzika ukafika, tulipewa maua ya kuweka kaburini nikarekodiwa wakati napeleka maua mimi, mama yangu na wale wengine niliomwonesha mtu wa video. Wakati huo mjomba na wageni wake wa Dar wanajua kuwa na wao wanarekodiwa kumbe hawamo mimi nimenyamaza tu. Basi baada ya siku 4 mjomba alitaka niende kuleta CD ya msiba wa Bibi mjini na nikaenda. Usiku tumemaliza kula akatoa laptop yake akaweka CD na tukakaa yeye na wageni wake tukaanza kutazama video ya msiba wa Bibi.

Tunaangalia ananisema mara kwanini ulikuwa unapiga picha na mama kwa kujidai mara nikaenda na mwili wake hadi nyumbani kurekodi video alikasirika sana eti nimeenda na mwili wa mama yake nyumbani kurekodi kwetu. Alikasirika sana ila mama akawa ananitete kuwa muache mtoto.

Basi video ilipoisha akauliza mbona mimi na marafiki zangu hatupo kwenye video nikamuuliza kwani nimerekodi mimi? Akapata hasira alinipiga mbele ya marafiki zake na mama akisema nimetafuta mpiga picha mbaya hajui kitu video nzima nipo tu mimi. Ugomvi ule ulikuwa mkubwa hadi marafiki zake wakaingilia kati ukiona hadi mjomba analia ujue kweli ana hasira ila nilifanya hivyo kulipiza mengi aliyonifanyia Dar wakati nipo kwake.

Ile CD akaisusa namimi nikasema hakuna shida nikaichukua na kuitunza mara nyingine huwa tunaenda nayo kwa jirani mwenye Tv tunaangalia na mama na wale marafiki zangu tuliorekodiwa tunafurahi na kurudi nyumbani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo umekuwa mtunzi wa Riwaya humu jamvin, walikuwepo wenzako akina K4Real na KidukuLilo wanangonjera kama zako siku hizi nyuzi zao hats hazisomwi na mtu. Unatuchosha
'Tengeneza furaha kwa wenzako bila kujali furaha yako'

Nikikupa kazi ya kutengeneza furaha yangu hutaweza ila mimi naweza kutengeneza furaha za wenzangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ndo unachoka na kufuatilia nyuzi zao na bado unacoment ,umejuaje hazisomwi?
Tatizo umekuwa mtunzi wa Riwaya humu jamvin, walikuwepo wenzako akina K4Real na KidukuLilo wanangonjera kama zako siku hizi nyuzi zao hats hazisomwi na mtu. Unatuchosha

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Huyu mwizi wa mitihani. Siku zake zinahesabika tumeahajuwa anapokaa bado kumkamata tu
 
Back
Top Bottom