Kisa: Nilivyowahi maishani

Kisa: Nilivyowahi maishani

NAENDELEA PARTY 14

Narudi kwa ndugu yangu wa kagera nikiwa pale kwenye pool table yake, nilikuwa na nidhamu sana sana kila kidogo nilichopata nilikuwa nahakikisha nafika nacho home natunza zingne naweka kwenye simu.
Yule ndugu yangu wa pool table yeye alikuwa kaajiliwa ni askari shida yake pombe, mademu ilikuwa ni changamoto sana kwake anapenda mno, mpaka nafika umri huu sinywi pombe hata unipe za bure au unifungie nazo ndani mwaka mzima utazkuta nina nidhamu sn kwenye hilo, siendi bar wala grocery na ukiniona huko bs ujue kuna mtu kaniomba nimpe kampani tu, kuhusu mademu ni kawaida sn ila sina tabia ya kuhonga mwanamke akitaka kunifukuza alete pigo za kupewa hela hela naweza kumpa tu ila si yeye aniletee pigo za kutaka pesa yangu najiondoa.
Haya tuendelee nilisimamia ile pool table ndani ya miezi 4 nikanunua kitanda na godoro 5 kwa 6, nikanunua flat 32 inch smart kbs, then nilikaa tena miezi 2 nikachonga sofa kali ya L shape na kuweka subwoofer la seapiano sp912 nadhan mnalijua hili sub.
Sa pale kijiweni nikajiongeza nikaweka tupombe sungura napima na kuuza full at last nikanunua friji mtumba nikaweka vinywaji full, nikapambana nikaweka mabonanza ya kichina yale na si hilo tu nikaanza na udalali wa simu na tv, subwoofer nilikuwa nafanya research na kujua bei zake kisha natangaza anayetaka alete pesa nimletee mpk mlangoni.
Kimsingi nilipiga hatua sn eeeh watu wakaanza wivu pale kijiweni wakawa wanampanga ndugu yangu kwamba inaonekana kuna hela sn pale hiyo elfu 50 ninayompa ni ndogo mi napata hela sn ndo maana nina vitu sn.
Siku moja ndugu yangu akanambia wkend anataka asimamie mwenyewe pool table lake hapo nikawa nimeshamsoma kwamba anataka afanye uchungu kwa siku anaweza pata shs ngapi, nikamwambia poa kweli akasimamia wkend ikaisha mara akasema anataka awepo wk nzima nikamwambia poa ni yeye tu.
Nilichoamua hiyo wiki yote aliyokuwepo nilifunga biashara zangu bnafs nikawa siendi kabisa pale kijiweni nilitulia tu home kutafakari nawezaje kuachana na pool ya watu na kile kijiwe.
At last wk iliisha akaniambia nimpe elfu 60 wa wiki hapo niligoma niliamua kumwambia mi tampa elfu 40 kuanzia J mpka jmos tampa elfu 40 then jpil yeye aje akusanye pesa yote akasema sawa.

Niliendelea kupga kazi kwa tahadhari sn ulipita kama mwezi huyo ndugu yangu akaja na hoja nyingne kwamba kapata mtu wa kusimamia na wamekubaliana ampe elfu 70 kwa wiki na wameshajaza mkataba mmmh hapo nilimgomea nikamwambia ww ulinipa hii table ndani ya miezi 6 ulikuwa umesharudsha pesa uliyonunulia na ww ndiye uliniomba nije kusimamia leo unataka kuniachisha kienyeji una shida gani ww aisee yule ndugu yangu hakunielewa kabisa.
Basi nikamwambia nipe wk 1 kisha mlete huyo mtu wako umkabiz kiroho safi. Hiyo wiki moja niliitumia kujiandaa kuhamia sehemu nyingne nikapambane kivyangu, kweli wiki iliisha nikamuita nikamwambia mlete huyo mtu pool yako hii hapa hatudaiani kbs nikamshukuru nikamkabizi.

Mimi niliamua kuondoa biashara zangu zote kwenye eneo lile kisha nikasepa zangu skuwahi kanyaga tena pale kwenye kile kijiwe aisee.
Ajabu siku moja huyo ndugu yangu akanipgia simu kwamba kuna jambo anataka nambia anataka tuonane mmmh ilinistua sn kunani tena.
Zilipita siku kadhaa hatuonani niliamua kumpgia simu anieleze kuna nn.
Eeeh nashangaa na kwa maskitiko makubwa sna akadai kwamba mimi kuna watu nimewaambia kwamba yeye atakuja kufa na ukimwi kama mama yake ( RIP AUNT YANGU ) nilistuka sn nikambana aseme nani kasema hayo akagoma anasema tu watu wa kijiweni pale, nikamsihi sn basi naomba umuite mtu huyo aje tuzungumze friendly aseme wp nilitamka maneno mazto kama hayo pia akagoma bt ukweli kbs sjawahi zungumza kitu kama hicho kwa mtu yeyote sjawahi na siwezi ila nilikuja kujua kumbe aliambiwa na mkewe kwamba eti ameskia kwa watu mi nasema hivyo na huyo mkewe akapga mpka simu kwa baadhi ya ndugu zetu akisema mimi nimemwambia hivyo ndugu yangu daaaah 😴😴😴😴😴.

TAENDELEA
Mjue nini kilijiri
 
Vitu ambavyo nimevipenda kwako ni kwamba huwezi kumnyenyekea mtu wala kuomba omba upate ukose unakuwa na amani tu salut kwa hilo japo maisha mapambano
na watu wengi wanadharaulika na hata kukosa fursa kutokana na kuwa omba omba mpk kero kiasi siku anakiwa na shida kweli lkn anashondwa kusaidika

ndio mana hata katika mafundisho ya uislam MTUME alitufundisha kuwa usijidhihirishe sana na ufukara au umasikini wako kwamba kila mtu ajue wewe huna wewe hivi wewe vile kuomba omba kila saa kwa kutaka makuu MUNGU mwenyewe anajua ndio mana siku zote 90% tukiwa kwenye msoto wa maisha MWENYEZIMUNGU anatujalia AFYA NJEMA na hata nguvu nyingi
 
NAENDELEA PARTY 15

Kwa masikitiko makubwa sana ndugu zanguni huyo ndugu yangu huyo ndugu yangu wa kagera alifariki kwa ajari mbaya sana ya pikipiki aligonga lori lililokuwa limepaki mnamo tarehe 21 June 2026 namshukuru sana Mungu kwaajili ya maisha yake na bahati kubwa sana ya kuweza kuishi naye hapa duniani APUMZIKE KWA AMANI.
Ila sasa wanawake wengne bhana mkewe bhana sisi ndugu tupo tunahangaika na msiba na namna ya kumstiri ndugu yetu yeye yuko anafanya mipango ya kuhamisha vitu huko kwake tulikuja kujua hilo sku ya 2 tulipokuwa tunahitaji baadhi ya vitu vya marehemu hasa nguo zake ili twende nazo kijijini eeeh ndo kukuta nyumba nyeupe peeee alooo sa sjui alijua ndugu tutachukua vitu, kwa kifupi alirudi kwao rasmi. Watoto tulibaki nao, hili tuliache turudi kwenye harakati zangu.

Niliendelea na biashara zangu kama vile nilikuwa naanza moja sasa eneo tofauti ila nilipambana sana ingawa mambo hayakuniendea vema sana kama zamani nilibuni biashara nyingine ya kuwa na madogo wawili wa kutembeza mayai kila sku ziuzwe trei 5 za mayai ya kuchemsha kweli nilifanikiwa kufanya biashara hiyo na nilikuwa napga faida kila sku 25,000 nikanunnua kiwanja, nikajinyima nikanunua pia pool table yangu sasa ingawa ilikuwa used ila ilikuwa poa sana.
Eeeh wale madogo wa mayai wakaanza shawishiwa na watu kwamba waache ili wao wawaajiri at last mmoja alikimbia na mtaji wote na faida ya siku mwngn alidanganya ameitwa kwao akasepa ila mpaka wanaaondoka ndani ya miez 3 nilikuwa nimenunua kiwanja na pool table.
Maisha yalisonga sana.
Niliamua kutafuta mke sasa mi bnafsi zamani kidogo niliwahi kuwa na mdada mmoja wa kinyiramba toka singida tulipendana sana mpk nikajikuta napenda sn kwenda singida kwaajili yake tu, na ukizngatia skuwa na mawasiliano makubwa sn na ndugu zangu na hata wazazi kwaiyo nilimuona huyo mdada kama ndugu yangu sana ingawa skumuoa kwasababu ya magumu niliyokuwa napitia alishaolewa ila nilijiapza kuoa singida na kweli nina mke wa kinyaturu na mtoto mmoja jumla watoto wawili na yule wa dsm.
Nina biashara kadhaa na mke wangu pia si haba anapambana pia.

Sasa nikiendelea tarudi kwa wazazi wangu huko ndo mtajua watu ni wabaya watu ni wabaya sana sana....

ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom