Kisa: Nilivyowahi maishani

Kisa: Nilivyowahi maishani

NAENDELEA PARTY 8
Kwanza nirudi kwa yule dada J nini kilifanyika baada ya kuwa mm nimefukuzwa kazi kwasababu ya roho yake ya kwanini, kwani niliskia kwenye kikao akisema eti imekuaje mi naanza tu kazi nalipwa laki 4 wakatu yeye alianza kwa kujitolea tu kwanini na mimi nisijitolee kwanza.
Kumbuka hapo hata hajui mimi na mzungu tumetoana wapi anasahau pia mimi nilikuwa namzd elimu mbali sana maana yeye alikuwa na certificate tu ndo alikuwa anasaka diploma.
Aisee yule dada J alileta rafiki yake pale ofisini ndiye akawa mtu wa marketing na yeye J akarudi kukaa ofisini.
Ni kweli ambavyo nilinena haikupita hata miezi 2 naye akatimuliwa kwa kutia hasara kampuni yeye pamoja na shoga yake wakapgwa chini.

Haya turudi sasa baada ya kufukuzwa kazi sasa maisha yalikuaje kwa kifupi nilirudi kwenye msoto usio wa kawaida kabisa sikuwa na wa kunitia moyo maisha yangu yote, mama yangu alituacha tukiwa wadogo sana tumelelewa kimafungu mafungu tu yeye mama alirudi kwao huko akaolewa akasahau kabisa kuhusu watoto wake. ( Hii story taileta kivyake kuhusu mama na uhusiano wangu na mzee aisee watu wana roho mbaya sana ).
Ok nikiwa sina kazi rasmi sasa hapo mwanamke hajui kitu na niliapa sitamwambia maana nilijua akijua ataniongezea stress tu.
Kale ka hela nilikobakiza kama laki 2, nako siku 1 mchungaji akaniita kwake akaniomba niwaazime kanisani shs 150,000 baada ya wiki 1 itarudi nikasema hiyo sawa nikampa nikitegemea ni waaminifu itarudi mfukoni nikabaki na elfu 40 tu, wakuu skulipwa pesa yangu yaani skurudishiwa mpaka kesho alooo.

At last nilichafuliwa sana na mchungaji kwa washirika maana niliamua kuachana na mambo ya kanisani kabisa maana niliona kumbe hata hawa wachungaji nao ni walewale nikaamua jifunza kufanya meditation tu siyo mambo ya dini tena.

Msoto ulikuwa heavy skubadili ratiba ya kutoka home nilikuwa natoka kama kawaida alfajiri sn kama naenda kazini kumbe naenda town kutafuta kazi mwanamke ye anajua mi naenda kazni.
Mfumo huo nilienda nao karibu miezi 3 iliisha anaona tu mi natoka kwenda kazini kumbe wapi, akiniuliza salary namwambia kampuni imepigwa faini ya kodi hali si nzuri boss kasema tuvumilie atatulipa malimbukizo yetu.
Ikafikia hatua sasa ya kutembea sina kitu mfukoni naikumbuka na hela yangu niliyoazmwa daaah.
Nikawa natoka alfajiri natembea kwa mguu toka goba napita makongo juu to mlimani city mpaka mbezi stand nakanyaga tena mpk kkoo au naamua kuzuga zuga hapo mbezi stand kama nasubiri usafiri wa kwenda mahali kumbe mi na gain time tu muda usogee sogee naposema mbezi namaanisha stand ya mbezi kabla haijaamishiwa makumbusho enzi hzo.

Nilipgika viatu vikaisha, nguo zkachakaa sina wa kunisaidia wala kunionea huruma njaa yangu, jua langu, kiu yangu, joto langu.
Wakati mwngn naishia pale udsm nazama kwenye miti miti kule natafuta sehemu nakaa peke yangu nalia sana kimoyo moyo nafanya meditation mpk nasinzia huko aloooo alooooo...
Sasa nikaanza kuwa siku zingne nabaki home tu.
Je nn kilijili sasa nilipokuwa nikibaki home pale sku moja moja...

TAENDELEA....
 
Wakuu hamjambo nyie madogo na wale wakubwa heshima yenu aisee....

Nikiwa nimemaliza degree yangu na matumaini kibao aisee haya maisha haya yamenifanya kuwa na nidhamu sana.
1. Mtiti ulianza home nilikuwa na chumba changu cha nje sjui kilitokea nn mzee one day ananitumia sms kwamba nikiwa natoka basi nikabidhi key kwa mama ( wa kambo ).
Ukweli nilikuwa natoka asubuhi narudi usku si kwamba nilikuwa naenda kuzurula hapana kutafuta hata kazi tu ya kujitolea .

Nilijibu ile sms kwa kumwambia mzee anipe wiki 1 nihame kabisa mi staki maneno maana maisha yashaanza kunichanganya. Hakujibu ila nilifanya hivyo akakatalia kitanda nikawaachia nikasepa zangu kuanza maisha enzi hizo goba bado sn nalala chini kwenye mkeka, asubuhi naamka natembea kwa mguu mpka posta aloooo.
Nilikuwa na demu wangu 1 akabeba mimba uzuri yeye alikuwa ameajiliwa ni mwalimu but naye alikuwa kichomi sana aisee, sasa kazi ikabaki kwangu nilikuwa natoka asubuhi sana home sjui naenda wapi sjui naenda kutafuta nn mfukoni sina hata 200 ya mihogo.

Natembea kwa mguu goba, mbezi luis, to kkoo to posta kisha narudi sina hali na hakuna wa kunionea huruma.

Sjui kula yangu wala kunywa yangu mwanamke hanielewi na wakati mwngne anasepa kaacha mtoto ndani sina hata 100 niliteseka sn, ajabu wenye maduka walikuwa wananiamini sn sjawahi enda dukani kukopa nikakosa lazma wanipe tu wengne nililipa wengne skulipa aloooo.
Kuna wakati nilitembea kwa mguu nikaenda tulia chini ya daraja fulani nkapitiwa usingzi aisee ile nashtuka nakuta nimezungukwa na ma kenge kama 50 hivi sjui ndo yalikuwa yanajipanga kunivamia nilikimbia hata sjui nilikiwa naelekea wapi 😴.

NILIAMUA KUFUNGUA BIASHARA YA KUCHOMA MAHINDI

Ila nyie mahindi yenyewe sjui kuchoma yakawa yanaungua tu mara mi siuzi wenzangu wanamaliza mi siuzi kbs nikaifunga skuwahi pata faida yoyote ile zaidi ya hasara huku namuwazia mwanangu home maana mwanamke haelewi.

Taendelea....
Wanaume tunapitia shuruba nyingi sana, Mungu alituumba tuvunge tusiongee tu, right Kama tungekuwa na midomo mirefu ungejikuta wewe una afadhari
 
Ila, hivi kuanzisha family (ngono zembe) wakati hali ngumu hivyo inatokeaje hii Kiongozi?

Huyo binti hata kutaka kuondoka ni ugumu wa maisha tuu, msoto huu uwe mwenyewe, ukileta wategemezi inakuwa balaa mara mbili elfu.
Wakati wakaka wengine nasikia kwny maisha magumu hata mdudu hasimami na mwanadada haipitiki...
Ila kwa wengine ni sehemu ya kuapta faraja...
 
NAENDELEA PARTY 10

Nilikuwa sku zingine nabaki home
Niliamua kuwa napokuwa home najichimbia ndani kimya kabisa si rahisi mtu kujua kama nipo ndani labda mtoto akirudi shule si mnajua tena watoto baba baba nyingi sana.
Hili la kubaki home sku moja moja kumbe yule mwanamke akikutana mashoga zake wanaonijua akawa anawaambia yule jamaa leo atanikoma haiwezekani abaki home ngoja nirudi ajabu akirudi hata hasemi kitu ukzngatia pia mi si muongeaji na hajui hata naptia nn.
Mkumbuke hapo unakuta sjala chochote tokea asubuhi nilichokuwa nafanya ni kuhakikisha mtoto akirudi akute chochote ndani basi ila mimi tajijua sasa.
Maneno nikawa naletewa mengi sana na watu anayosema mwanamke ninayeishi naye ilifikia hatu akawa ananiambia nanuka sana maana yake hata kulala naye tu kitandani stakiwi maana anadai nanuka nyie acheni tu.
Nikifikilia nayoptia na haya maneno makali ya mwanamke nilikuwa naishiwa power kbs.

Kuna jamaa yangu mmoja nilimaliza naye chuo alikuwa kapata kazi ya kusimamia kiwanda cha kufyatua tofari maeneo ya goba ingawa kulikuwa na kaumbali toka hapo nilipokuwa siku zngne nilikuwa naenda huko nashinda huko kiwandani wakati mwngne napiga tofari nikirudi home nimechakaa mwili hoi maumivu kila kona lengo nipate ka hela ka kununua chochote kwaajili ya mtoto na mimi pia.

Siku zilisonga sioni kesho yangu kabisa, kuna ndugu yangu mmoja alinitafuta kwamba kuna taasisi mpya imeanzishwa kwaiyo nimekuwekea nafasi utakuja mwanza mmmmh nikasema angalau nimeanza ona nuru sasa.
Siku kadhaa zilipita akasema nitafute passport kubwa niwe nayo, nichome manjano, nichome corona kisha documents zote nizi scan nimtumie nilichakarika hasa kupata 150,000 ya passport mpka nikapata nikatuma vitu vyote alivyosema. Ila msoto uko palepale hakuna ahueni.
Nikawa namsumbua yule ndugu hiyo kazi vp majibu yakawa ni subiri takwambia tu daaah mara mwezi, mara miezi mara mwaka ukaisha story ni zilezile tu. Nilimtafuta jamaa yangu mmoja ni pastor alikuwa kanda ya ziwa huko nikamwambia nataka nije huko kwani kuna mchongo nauskilizia mwanza hapo akasema njoo bahati nzuri naye alikuwa ananikubali sana nilisoma naye A level na chuo nilisoma naye kimoja.
Nikasaka nauli mpaka nikaipata safari ya kuondoka dsm ikaanza mwanamke nakumbuka nilimwambia mi naondoka hapa ila starudi tena hapa nikamshukuru kwa yote na nikaondoka to kanda ya ziwa. Huku nyuma sasa yule mwanamke alikuwa akituma sms za kunitukana sn na kunikejeli madai yake ni hela ya mtoto daaaah kila nikijitetea lakini wp at last nilimwambia ampeleke home kwa mzee tarudi kumchukua hapo akagoma labda kama nataka chukua mtoto mpk nimuue kwanza yeye ndo nichukue mtoto.
Niliamua kubadili namba ya simu ili kuepuka maneno makali aliyokuwa akinitumia, nikiwa nipo kanda ya ziwa na jamaa yangu nili relax kdg akili ilifunguka sn na mwili ulirudi angalau nikawa mtu sasa.

TAENDELEA KUHUSU ILE KAZI YA NDUGU YANGU NI MAJANGA MATUPU...
 
NAENDELEA PARTY 10

Nilikuwa sku zingine nabaki home
Niliamua kuwa napokuwa home najichimbia ndani kimya kabisa si rahisi mtu kujua kama nipo ndani labda mtoto akirudi shule si mnajua tena watoto baba baba nyingi sana.
Hili la kubaki home sku moja moja kumbe yule mwanamke akikutana mashoga zake wanaonijua akawa anawaambia yule jamaa leo atanikoma haiwezekani abaki home ngoja nirudi ajabu akirudi hata hasemi kitu ukzngatia pia mi si muongeaji na hajui hata naptia nn.
Mkumbuke hapo unakuta sjala chochote tokea asubuhi nilichokuwa nafanya ni kuhakikisha mtoto akirudi akute chochote ndani basi ila mimi tajijua sasa.
Maneno nikawa naletewa mengi sana na watu anayosema mwanamke ninayeishi naye ilifikia hatu akawa ananiambia nanuka sana maana yake hata kulala naye tu kitandani stakiwi maana anadai nanuka nyie acheni tu.
Nikifikilia nayoptia na haya maneno makali ya mwanamke nilikuwa naishiwa power kbs.

Kuna jamaa yangu mmoja nilimaliza naye chuo alikuwa kapata kazi ya kusimamia kiwanda cha kufyatua tofari maeneo ya goba ingawa kulikuwa na kaumbali toka hapo nilipokuwa siku zngne nilikuwa naenda huko nashinda huko kiwandani wakati mwngne napiga tofari nikirudi home nimechakaa mwili hoi maumivu kila kona lengo nipate ka hela ka kununua chochote kwaajili ya mtoto na mimi pia.

Siku zilisonga sioni kesho yangu kabisa, kuna ndugu yangu mmoja alinitafuta kwamba kuna taasisi mpya imeanzishwa kwaiyo nimekuwekea nafasi utakuja mwanza mmmmh nikasema angalau nimeanza ona nuru sasa.
Siku kadhaa zilipita akasema nitafute passport kubwa niwe nayo, nichome manjano, nichome corona kisha documents zote nizi scan nimtumie nilichakarika hasa kupata 150,000 ya passport mpka nikapata nikatuma vitu vyote alivyosema. Ila msoto uko palepale hakuna ahueni.
Nikawa namsumbua yule ndugu hiyo kazi vp majibu yakawa ni subiri takwambia tu daaah mara mwezi, mara miezi mara mwaka ukaisha story ni zilezile tu. Nilimtafuta jamaa yangu mmoja ni pastor alikuwa kanda ya ziwa huko nikamwambia nataka nije huko kwani kuna mchongo nauskilizia mwanza hapo akasema njoo bahati nzuri naye alikuwa ananikubali sana nilisoma naye A level na chuo nilisoma naye kimoja.
Nikasaka nauli mpaka nikaipata safari ya kuondoka dsm ikaanza mwanamke nakumbuka nilimwambia mi naondoka hapa ila starudi tena hapa nikamshukuru kwa yote na nikaondoka to kanda ya ziwa. Huku nyuma sasa yule mwanamke alikuwa akituma sms za kunitukana sn na kunikejeli madai yake ni hela ya mtoto daaaah kila nikijitetea lakini wp at last nilimwambia ampeleke home kwa mzee tarudi kumchukua hapo akagoma labda kama nataka chukua mtoto mpk nimuue kwanza yeye ndo nichukue mtoto.
Niliamua kubadili namba ya simu ili kuepuka maneno makali aliyokuwa akinitumia, nikiwa nipo kanda ya ziwa na jamaa yangu nili relax kdg akili ilifunguka sn na mwili ulirudi angalau nikawa mtu sasa.

TAENDELEA KUHUSU ILE KAZI YA NDUGU YANGU NI MAJANGA MATUPU...
Mkuu Kweli shida zinakupa upofu mpaka unamwambia mkeo ampleke mtoto kwa mzee wako(na mama yako wa kambo) ambao walikutimua kama mbwa koko? Ulitegemea huyo mtoto ataishije yani?
 
Mkuu Kweli shida zinakupa upofu mpaka unamwambia mkeo ampleke mtoto kwa mzee wako(na mama yako wa kambo) ambao walikutimua kama mbwa koko? Ulitegemea huyo mtoto ataishije yani?
We acha tu kuna matukio tawapa hapa khs huko kwa mzee ni noma sn raia hawa si ndugu si nani 🤔
 
NAENDELEA
PART 5

NAPATA KAZI YA KUOSHA MAGARI MBEZI LUIS KABLA STEND HAIJAJENGWA.
Nimetoka zangu goba kwa mguu sjui naelekea wapi nikaenda mpaka mbezi luis nikashika ile njia ya kwenda kibaha nikiwa natembea hata sjui naenda kwa nani mara nikakuta jamaa mmoja anaosha madaladala njiani...
Nikampa hi kisha nikamwambia nataka kusaidia kazi japo nipate chochote, jamaa akanambia karibu kwa leo maana mwenzie hajaja kazini.
Kweli nikaanza kazi na sjawahi osha magari aisee nilipambana sana kufanya usafi ndani ya gari na nje ya gari pia kusugua gari itakate.
Nilipga kazi hatari sana nina njaa nina kiu hakuna wa kunionea huruma.
Makondakta na madereva wakawa wananipa nguo zao za kazi kuwafulia nikijua wananilipa chochote but hola nilifua niliosha magari mpka kwenye saa 12 jioni hivi jamaa akanipa elfu 5 tu ila nilishukuru sana aisee.
Nikatoka hapo nikaanza kupiga mguu kurudi home nikanunua juisi ya 500 na vitumbua vya 500 nikawa natafuna huku narudi zangu home na elfu 4 mfukoni kishujaaa.
Nilipofika home nakuta mwanamke kanuna nikampa ile elfu 4 nikamwambia bs kama kuna cha kumnunulia mtoto amnunulie ingawa walikuwa wameshakula maana si mnajua mwanamke yeye alikuwa kaajiliwa ni mwalimu wa secondary.
Kesho kumekucha nikasema wacha niende palepale kwenye kuosha magari nikamkuta mwamba nikaanza kupiga kazi hatari sn mpaka jioni kwenye saa 12 hivi jamaa ananifata ananiambia leo hamna hela kwani hela yote kampa bosi hapo sjala, sjanywa wala sina kitu kbs sionewi huruma na mtu.
Nilishiwa pozi ila ndo ivyo nimefanya kazi bure tu ya kuwaingzia watu hela huyooo nikatoka mdogo mdogo kurudi home nina kiu, njaa, nimechoka sn kwa kazi na sina hela hata mia.
Natembea kwa mguu tena toka mbezi to goba alooo nmefika home mwanamke nikamkuta katulia zake na mtoto wameshakula wapo wanabembelezana, daaah no menu hakuna nilichobakishiwa.
Mkumbuke sjala wala kunywa toka asubuhi hapo na nimetenbea kwa mguu nenda rudi, mi binafsi ni mkimya sn so nilipoona hapa hakuna msosi nilinyamaza tu nikatafuta maji nikaoga nikalala kimyaaa yaliyonikuta huko nilikokuwa ni siri yangu na Mungu wangu.

NITAENDELEA....
Huyo mwanamke wako alikua alikua halipwi kwani?
 
Back
Top Bottom