NAENDELEA 4
NILIAMUA KUFANYA KAZI YA KUSAJIRI LINE NIKAISHIA NDANI..
Wakati naendelea kupambana siijui kesho yangu sina wa kunionea huruma. Nilikutana na dogo mmoja anasajili line nikamuuliza hii kazi unafanyeje , akanipa maelekezo na vigezo uzuri nilikuwa navyo nikaenda aliponielekeza.
Walinipokea wakanisajiri kisha wakanipa smartphone mpya ya kufanyia kazi rasmi nikaanza kutembea mitaani maeneo ya Riverside nasajili line huku nawaza ikitokea nimekutana na wanaonijua tawaambia nn kiukweli yalikuwa mateso tu.
Unazunguka chocho kwa chocho na hupati kitu home nako hamna kitu.
Bado natembea kwa mguu toka goba mpaka ubungo kila sku kuwahi ofisini. Nikapata wazo kwamba liwalo na liwe mi nauza hii smart nitimize mahitaji yangu na family pia hasa mtoto kweli niliuza kisha nikapotea hewani.
Jamaa akaanza kunisaka goba huko anazunguka kuniulizia ila hakufanikiwa kunipata, ulipita kama mwezi 1 nikakutana naye mbezi luis akasema yeye anataka simu au twende polisi nikamwambia simu sina na nikampa hali halisi akalazimisha twende polisi basi tukaanza enda.
Nikapata wazo huyu nimkimbie tu si nikamchomoka akaniitia mwizi mara kuna raia walikuwa wanafyatua matofari wakaibuka na nyundo, mawe, mafimbo nk nikasimama nikawaambia mimi siyo mwizi aisee na nikaelezea situations yote jamaa wakatulia tu wakashauri at last mwenye simu akakomaa polisi kweli kwa mara ya kwanza nazama ndani mahabusu nikakutana na vijana wamepinda mle, harufu kali, ndoo la mavi humohumo mtu anajisaidia hapo pembeni huku watu wanakula kando, funza kama wote, usku mnajazwa kama mizigo plus joto la dsm ooooooh.
Nilikaa kama siku 5 hivi sina matumaini kabisa mwanamke akija ananitolea maneno makali mi kimya tu, siku moja akaja mpelelezi akanitoa akanipiga pingu uelekeo kituo cha polisi shekilango, tulifika kule akanihoji kisha kuna ndugu yangu mmoja akanizamini nikatoka.
Ila kesi iliandikwa nadaiwa hela mi nilikataa sababu nilikuwa nadaiwa simu tu si pesa at last tuliyamaliza mimi na mwenye simu nilimpa property yangu 1 hivi kesi ikaisha.
Siku narudi home mwanamke ananifukuza na ilikuwa usku wa saa sita nikazungumza naye kumtuliza kidogo akawa mpole, kuna ndugu yangu huyo aliyekuja kunidhamini wakati nipo ndani kumbe yeye na mwanamke wangu wananisema mpk mambo yakafika home eti mi ni tapeli mwizi nimefungwa aisee ila binadamu bhana 🥺 ila yalipita na nipo imara sn na mwenye nidhamu kubwa mno.
TAENDELEA..