Watu walikua busy na registration nami nikiwa mmoja wa wanafunzi tuliokua tunaingia first year. Ndipo macho yangu yakamuona huyu mdada wa "kimachame" na kumzamisha kunako "moyo". Nikamsogelea kumsabahi na kumuomba "kampani". Akakubali & from there tukawa marafiki. Kwa kuwa nilishamtamani kimapenzi, haikuchukua muda nikarusha "ndoano" akaniambia nisubiri atanipa jibu. Sikuamini pale aliponiambia hawezi kua na mimi coz ni "mshamba" & naweza kumtia aibu kwa marafiki zake. ILINIUMA SANA. Hivyo ndivyo nilivyoambulia kibuti.. Nilijitahidi nikasahau yote, nikaja kuwa na GF mwngne hapo b'dae, japo hatukudumu kwa muda mrefu.. Nilimaliza chuo na nikaajiriwa at the same time nikawa na b'nes zangu. Siku moja usiku nikaona namba ngeni inaingia kwa simu yangu, nikajaribu kupokea but mpigaji akakata simu. Asubuh iliyofata nilipiga ile namba, sauti ya mdada ikaitika na kunitaja jina langu.. Akazunguka kunambia yeye ninan, nikamtukana then nikakata simu. Ndipo b'dae akaniandia ujumbe mfupi na kuniomba radhi kisha akajitambulisha.. Moyo ulinipasuka paaa..aa, kuona jina la mdada aliyeniumiza wakati nipo chuo!!
Tukapanga kuonana na ikawa hvo. Akanieleza yalomkuta nami nikaeleza yangu, akatoa machozi na kuniomba radhi kwa alonifanyia nikiwa chuo. Mdada anafanya kazi na amenambia she is ready for marriage. Kuna mzee mmoja wakati nipo mwaka wa 2 alishawah kunambia usithubutu kuoa mwanamke ambae alishawah kukukataa kwa kukukashifu. Nashindwa kuamua wadau, naomba busara zenu.