Nilikutana na mwanamke akiwa kama mpangaji mwenzangu, niliishi kwa muda wa miezi minne,ndipo nikaamua kumtongoza huyo mwanamke yeye akiwa mfanya usafi kwenye mamlaka ya hali ya hewa nyanda za juu kusini nami nikiwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo kimoja huko huko nyanda za juu kusini. Mwanzo wa mahusiano alijitahidi sana kuonyesha upendo wa hali ya juu sana,ila baadae nikaanza kuona gari linapaki na mzee mtu mzima anazama ndani kwa mpenzi wangu na wanadumu ndani masaa yakutosha wkati huo anadhani mie nipo chuoni kumbe nipo mwangu! mwisho wa siku nikamuuliza akaniambia yeye alikuwa wakwanza hivyo nitulie amtafutie sababu amuache, nami nilipenda nikavumilia upuuzi huu lakini nikashuhudia kijana kaingia tena kuuliza nikaambiwa ni ndg, ila siku moja nikawa karibu na huyo kijana nikasikia akimuliza mpangaji mwenzetu mwingine mchumbangu hajambo? yule mpangaji mwenzetu akamuuliza nani ? akamtaja jina mpenzi wangu,kuanzia pale nikakata tamaa nanikaamua kuhama,lkn yeye ameshajua udhaifu wangu ametafuta hadi amepajua ninapo ishi kwa sasa na anakuja kwangu na nina mpenda sana tatizo ni malaya na kwakweli kumuacha inana kuwa ngumu nitumie njia gani wadau niepukehili balaaa?