Nilikuwa sijaamini mpaka nilipohakikishiwa na mtu wa karibu kwamba mfalme wa kisiwa cha hapo Guam analindwa na wanajeshi wa nchi tofauti

Nimesikitika sana sana sana,
Inamaana ukilindwa na wanajeshi wa nchi tofauti hapo hekaluni ndo wanaopigana vita ya uchumi utawashinda?

Nilimpuuza Dada mmoja anaishi anapokaa Mr ticha wa profesa Jay, aliposema kuna mfalme wa Guam analindwa na wanajeshi wa kanchi ka pembeni yake, nilimbishia ni kadhani ni kwakuwa yuko mlengo wa kushoto,

Lakin jana nimeamini kabisa na nimeshangaa sana

Nimeamini so kila habari ni ya kupuuza hata kama ni ya kipuuzi

Mungu awabariki watu wa Guam
CHAGUA WIMBO
 
Guam?? Kisiwa cha Guam?? Hakuna mfalme huko. Stori gani hiyo?? Guam ana Rais anayeitwa Joe Biden, hadi Novemba alikuwa Donald Trump.

Guam (kwa Kichamoru: Guåhan) ni eneo la ng'ambo la Marekani (U.S. Territory of Guam) upande wa kusini wa funguvisiwa ya Mariana katika Bahari ya Pasifiki. Huhesabiwa kati ya visiwa vya Mikronesia.
Eneo la kisiwa hicho ni kilometa mraba 543. Mji mkuu ni Hagåtña (Agana). Uchumi wa Guam unategemea kituo cha kijeshi cha Marekani pamoja na utalii.

Historia​

Wakazi wa kwanza wanaojulikana ni Wachamoru walihamia miaka 4,000 hivi iliyopita.
Tangu mwaka 1668 visiwa vya Mariana vilikuwa koloni la Hispania.
Baada ya vita ya Marekani dhidi Hispania Guam ikatwaliwa na Marekani. Visiwa vya upande wa Kaskazini vikauzwa kwa Ujerumani na kuwa Mariana ya Kaskazini.
Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia kisiwa kikatwaliwa na Japani, lakini tarehe 21 Julai 1944 Waamerika walirudi na kuwafukuza Wajapani.
Mwaka 1949 kisiwa kilipewa hadhi ya Eneo la ng'ambo la Marekani, wakazi wake wakapewa uraia wa shirikisho hilo.
Chanzo: Guam katika Wikipedia ya Kiswahili
6e4836ce122b44072a8b11a186b07e42.jpg
 
Guam?? Kisiwa cha Guam?? Hakuna mfalme huko. Stori gani hiyo?? Guam ana Rais anayeitwa Joe Biden, hadi Novemba alikuwa Donald Trump.

Guam (kwa Kichamoru: Guåhan) ni eneo la ng'ambo la Marekani (U.S. Territory of Guam) upande wa kusini wa funguvisiwa ya Mariana katika Bahari ya Pasifiki. Huhesabiwa kati ya visiwa vya Mikronesia.
Eneo la kisiwa hicho ni kilometa mraba 543. Mji mkuu ni Hagåtña (Agana). Uchumi wa Guam unategemea kituo cha kijeshi cha Marekani pamoja na utalii.

Historia​

Wakazi wa kwanza wanaojulikana ni Wachamoru walihamia miaka 4,000 hivi iliyopita.
Tangu mwaka 1668 visiwa vya Mariana vilikuwa koloni la Hispania.
Baada ya vita ya Marekani dhidi Hispania Guam ikatwaliwa na Marekani. Visiwa vya upande wa Kaskazini vikauzwa kwa Ujerumani na kuwa Mariana ya Kaskazini.
Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia kisiwa kikatwaliwa na Japani, lakini tarehe 21 Julai 1944 Waamerika walirudi na kuwafukuza Wajapani.
Mwaka 1949 kisiwa kilipewa hadhi ya Eneo la ng'ambo la Marekani, wakazi wake wakapewa uraia wa shirikisho hilo.
Chanzo: Guam katika Wikipedia ya Kiswahili
Ama kweli asiyejua maana, haambiwi maana.
 
Back
Top Bottom