Nilikuwa napuuza 'Chuma Ulete', leo yamenikuta

Nilikuwa napuuza 'Chuma Ulete', leo yamenikuta

Trinity

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2017
Posts
1,867
Reaction score
3,618
Kwanza kabisa niwape pole kwa msiba mzito wa rais wetu Jpm.
Binafsi nimehuzunika sana kumpoteza mtetezi wa wanyonge, mzalendo, mkweli, mchapa Kazi, mbunifu, mcha Mungu,
na jasiri.

Niende direct kwenye Mada,

Aisee nimekua nashangaa watu nikiwaomba chenji wanapata wasiwasi na kuniuliza, pesa yako haina miguu??

Wengine wamekua wakinyima chenji kabisa mpaka unakasirika na kuwaona wana roho mbaya.!

Ipo hivii, kuna eneo la stend nikiwa nimetulia nasubiri wateja waje, akaja dogo amempakia abiria kwenye boda.
Walisimama Karibu yangu na kuomba chenji ya elfu 10 nikasema ninayo ila ni elfu tano tano, dereva boda akasema hiyo hiyo.
Nikazama mfukoni nikatoa kitita cha elfu 60. Elfu 10, kumi zilikua 3 nyingine zilikua elfu tano tano tu.
Nikatoa elfu tano mbili nikampa ile elfu 10 yake nikaikunja na zile nyingine, kwa hiyo elfu kumi kumi nikawa nazo 4.
Hee, baada ya muda kidogo kupita nikaenda mpesa nimtumie mtu elfu 20.

Kuchomoa kitita changu nakuta elfu kumi aliyonipa siioni, niliikariri maana zangu zilikua mpya nahisi second au first hand kabisa kutoka zitengenezwe ila ile ten yake ilionesha imetumika zaidi.
Nilijisachi mpaka kwenye soksi nikavua viatu lkn wapi.

Nilishangaa sana, ile narudi nikamcheki aliposhuka yule jamaa, akawa hayupo na wakati hakuna bus limepita na abiria wengine walikuwa wamekaa kwenye banda la kungojea usafiri.

Nikaja kuconnect na jinsi walivyofika pale nikaamini walikuwa kitu kimoja maana walipofika walikuwa wanaongea kwa sauti ya chini kabla ya kunifuata, sikuwafikiria sana mi nikawa busy tu na smart yangu nafuatilia matukio ya msiba wa taifa.

Wanaonyima chenji nimeamini hawajipendei, imewapasa kufanya hivyo kutokana na mambo ya kihuni kama hivi.

Kama una kisa cha kuibiwa pesa kimazingara kama hivi, tunaomba ushuhuda na jinsi ya kuzuia hawa chuma ulete.!
 
Binamu yetu aliachwa dukani ( m pesa kiosk)
Jioni alivoulizwa pesa ziko wapi kasema kuna mtu kaja kaomba chenji na baadae pesa kama laki tatu zikapotea kichuma ulete

"Mimi sijawahi kuamini kama ni kweli zilipotea au alitumia tu "
Labda alitupiga ki- kalimani au ki- amfifilo
 
Kuna dogo nilipata goli la chips, yai, vyuku, mishkaki na wenzie Obay huko nikaona si mbaya nimuweke ajiongeze maana alikua mzigo tu home. Goli lilikua linatema, Nikamuwekea mtaji mzuri tu vyombo, misosi na wasaidizi ye kazi yake adeal na malipo tu. Baada ya kuuza.

Na ilikua mi tukutane once a week niende kujua ngapi kaweka duh🤔.
Mwezi tu dogo kaleta hesabu mara 2.
Haya ukimuuliza ok mzigo ulikua nao wa kilo 3, kwa wiki tupate 5 we unakuja na 2 inakuaje?
Na sawa labda biashara ilikua mbovu viko wapi vitu vyote?
Vimeisha Bro.
Hela? anajibu hata mi sijui
Namboost tena tunanunua mazagazaga yote tunaweka golini.
Mara karibia 4 same shit,
kumbuka kuna kodi hapo inatakiwa ilipwe miezi mi3. na ni hela ndefu.
Ilifika mwisho nikimbananisha anaanza kulia kuomba misamaha mingi.
Nikaona kama namwonea tu.
Ilifika mahali mwenyewe akasema bro labda mi sihitajiki kufanya biashara.
Nilimwonea huruma lakini kumforce aendelee ingekua torture.
Kuna siku niliamka tu nikaenda beba kila kitu
Piga mnada,
Nikamrudisha home tutafute la kufanya.
Ilibidi ila hata mimi iliniuma.
Dogo mwenyewe sio mtu wa mademu wala kilevi.
Ndo naamini chuma ulete inawezekana kabisa walikuwepo pale.
Hiyo 2000+
 
Mnaoamini chuma ulete kupiga hatua hua ndoto!
Anywys!
Ni kwenye Hizi biashara ndogo ndogo, km Jamaa kwenye mada ni elfu 10 tu anaongea.
Mi pale nilimvua mtu jiko nikalipa kodi yake na kufungua biashara yangu yani kila kitu ilikua cash imetumika.
Kwa kutegemea hela itarudi.
Na ni sehemu nzuri maana mi na group langu wenyewe kama 10 tukitoka huko tulikua tukigonga vyombo na menyu balaa hapohapo.
Ilikua sehemu ya biashara.
Acha madreva taxi,staff,jirani supermarket wapita njia na kulikua na kituo hapo cha daladala.
Ndo mana nikasema alikua anauza kila kitu kinaisha
Hela haionekani. 🤦‍♂️
 
Back
Top Bottom