Nilikuwa nakula sana ndimi za ng'ombe

Nilikuwa nakula sana ndimi za ng'ombe

Daktari wa Meno

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2019
Posts
509
Reaction score
1,617
Kipindi fulani nikiwa kijijini nilikuwa nimebuni kitoweo ambacho kwa kweli kulikuwa kinanipa sana nyama ila kupatikana kwake haikuwa kazi ndogo.

Nilikuwa nakata ndimi za ng'ombe na kunywa supu bila wenye ng'ombe kujua kama wanyama wao hawana ndimi. Siku moja nikiwa nimekaa wazo likaniijia namna gani naweza kupata vitoweo kwa ajili ya ugali. Niliwaza uvuvi ila kijijini hakukuwa na chanzo chochote cha maji ambacho kinaweza kufanya uvuvi.

Siku moja nikapata wazo na kukata ndimi za ng'ombe na nikafanya majaribio nikaona mafanikio ni makubwa sana. Nilichokuwa nafanya ni kwenda zizini kwa mtu usiku na kumfunga ng'ombe kwa kamba imara ili asinijeruhi (kwa wale ng'ombe wakorofi) nikishamfunga nabana taya zake kwa vidole kisha atatoa ulimi nje, akitoa tu naukata kwa kisu nusu ya ulimi nakuwa nimeikata na kisha nampaka chumvi na dawa moja hivi ya kienyeji ili asioze ulimi.

Basi nilikuwa nafanya hadi kupata ndimi 10 kwa usiku mmoja, ilikuwa ni kazi ya hatari ila nilikuwa napata sana pesa na kitoweo kwa ajili hiyo. Mafanikio yakawa makubwa na sasa nikaamua kuuza supu ya ulimi pale kijijini hakuna mtu alijua kuwa asilimia kadhaa ya ng'ombe wamekatwa ndimi kijijini pale. Basi nikawa napika jioni supu, usiku naenda kutafuta ndimi kwenye mazizi ya ng'ombe.

Ile kazi iliendelea baadae nikaona soko limekuwa baya nikaamua kuacha maana ndimi ziliadimika sana, kuna muda nikawa naenda hadi vijiji jirani kupata hizo ndimi kwa ajili ya biashara na kitoweo.

Vijana ajira ni akili yako sio akili za wanasiasa.
 
Kama ni kweli sio chai basi mateso uliyokuwa ukiwapa hao nawe yatakufika. Tubu kwa Muumba wako upate msamaha na rehma
 
Mkuu kwa hapa umefeli unakata ulimi wa viumbe ulikuwa unawapa mateso makubwa sana ungegundulika nnchi zilizo endelea ungekuwa na mashtaka mawili la wizi na ungeshitakiwa na watetezi wa haki za wanyama kukata ulimi unawaacha na mateso hao hao Ng'ombe.

Na assume tungekukata wewe ulimi hayo maumivu vipi na isitoshe ungekuwa unakulaje?

Hii story ya leo umefeli, ila unajitaidi kutunga leta zingine tuta support unajitaidi ila kwa hii ya leo hapana
 
Mimi nimekulia kijijini; Hii story yako ipelekwe jukwa LA mzaha!
KILA MFUGAJI HAKOSI KUWA NA MBWA! MBWA WAKALI,
we pimbi hao MBWA wasikuone hadi unapanua mdomo ng'ombe? Au hao ng'ombe walikupa ulimi kama denda?

ETI HADI NG'OMBE WAKAADIMIKA NDIMI!
Thubutu, labda ng'ombe Wa mabua!

Kwanza kila zizi kuna ng'ombe kichaa!

Shwain pimbi mkubwa weye uache urongo wako!
 
Lazima kuna ng'ombe walikufa kutokana na ukatili wako! wewe ni muuaji, ni mwizi, umeharibu uchumi wa wanakijiji. Hiyo dhambi itubu tu, Hata Mungu hapendi na ndio maana unafeel guilty na umeanza kuropoka matendo yako!
 
Back
Top Bottom