Nilikufanyia ushenzi wote, Saivi najuta!!

Nilikufanyia ushenzi wote, Saivi najuta!!

L, kila nikikukumbuka moyo wangu unakosa amani.
Wewe ulikuwa mwanamke mwenye roho ya kuvumilia mengi, Nilikuchukulia simple sana nkakufanyia kila aina ya maudhi.
Kila nilipoanzisha mada yenye ugomvi, kwa sura ya upole ulikaa kimya ili kujitenga na ugomvi wangu.
Nilikuonea wivu sana hata kwa vitu ambavyo si kweli.
Ulikuwa tayari kukosana na wazazi ndugu na jamaa kwa ajili yangu.
Kipindi sina pesa ulinisaidia sana, japo na mimi nilipozipata nilikusaidia.
Kipindi chote hukuwahi nikatalia chochote
Uliniaga unaenda nyumbani, imepita mda sasa, meseji hujibu wala kupokea.
*Baada ya mda kupita bila mawasiliano na wewe, mda wote nilikosa furaha, nkaanzisha mahusiano na mwingine,
Ebhana eh, huyu amekuja kudhibitisha kuwa wewe ulikuwa mwanamke uliyevumilia mengi kutoka kwangu.
Nilidhani kuingia mahusiano mapya nitakusahau lakn kumbe ndo nimezidi kukukumbuka,
Tafadhali popote ulipo rudi, nimejifunza na kujutia mengi.
You were the super woman!
Harudi NG'O. Imekula kwako. Mwanamke wa dhati akiondoka, huondoka daima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
daah. umenikumbusha mtu 1, kila nilikuwa nikitaka kuchepuka basi nazua ugomvi wowote ili nizime simu na kuzama gesti kulala huko.

nikirudi asbh ghetto namkuta A. wangu asha fika anafanya usafi, anaomba msamaha kwa yaliyo tokea jana yake.

sijawahi pata mwanamke kama yule, sikushangaa hata aliye muoa alimfatilia kwa 5yrs ila muda wote alikuwa hataki akimini mimi ndo mmewe.

Now nakutana na vizazi jeuri hadi nimeamua kupumzika mahusiano rasmi nimebakiza chapa ilale.
Ulidhani karma itakuacha salama?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom