Niliiona hii laana ikiingia nchini

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,869
Reaction score
828,391
Sasa hivi haya mambo yamekuwa ni ya Kawaida kiasi kwamba watu wakiyasikia hawastuki sana

Haya mambo yalianza miaka ya 90.. Uumbaji ulipoanza kunajisiwa kwa kasi ya aina yake

Wababa kutembea na mabinti zao mpaka wengine kuwapa ujauzito na kuzaa nao ama kufanya abortion
Wamama kuingia kwenye mahusiano na watoto wao wa kiume mpaka kufikia kufunga nao ndoa

Mabinti kugombana na mama zao kwa ajili ya mahusiano na baba zao

Matokeo yake wazazi wakaanza kuwalaani watoto wao na laana hizo ndio zimezaa mauaji mengi ya wazazi wanaouliwa na watoto wao wa kuwazaa

Iwe kwasababu za kishirikina, utajiri, umaarufu urithi nk.. Lakini haya mambo yana asili yake
Haya yanayotokea sasa ya wanandoa kuuana kwa sababu ya mali ama wazazi kuwaua watoto wao hasa wadogo kwa ajili ya mali si mambo ambayo hayana asili ama yametokea bila chanzo

Ni laana kubwa kwa wazazi kuingia kwenye mahusiano ya kingono na watoto wao wa kuwazaa
Ni laana kwa watoto wa tumbo moja kuingia kwenye mahusiano ya kingono

Haya mahusiano huwa na nguvu sana lakini pia huwa na matokeo hasi makubwa sana
Hizi laana za kingono kati ya ndugu wa damu zina athari mpaka kwenye ardhi na vizalia vinavyofuata!
 
Insest
How does inbreeding affect the child?
Inbreeding is related to various unfavorable outcomes in the offspring and is associated with the development of recessive genetic diseases. High rates of abortion and congenital malformations have been observed in the children of inbreeding couples.
 
Mifumo ya kujiingizia kipato ilegezwe, soko liwe huru, ushindaji wenye tija, mikopo iwepo pasipo upendeleo, mfumo wa elimu ubadilishwe, sera zuri za kiuchumi kiundwe, uwezeshwani wa viwanda vidogo na bidhaa bunifu bila masharti, uwepo wa wanasaikolojia ngazi ya kata, kupumguza au kutokomeza waganga haramu wakienyeji, kutumia madini na rasilimali za nchi kuimarisha shilingi ili kuipa thamani na kupumguza mfumuko wa bei, rai kuchukulia kama binadamu na sio watu...

Nadhani tukifanya hayo hii nchi itakua na watu werevu, wachapa kazi, wawajibikaji, wenye upendo, wenyekipato kidhi na zaidi, WENYEFURAHA, wenyemawazo chanya, watii, wanaopenda wenza na WENYEKUPENDA MAISHA. Tusiona watu wanauwana, tunazungukia mbaaaaali tunaimba nyimbo za laana mara sijui utajiri wa waganga BIG NO.

Turudi kwenye misingi tuloiacha hapo juu, tuache uchawa na kusikiliza mawazo ya watu ndo yatumike kuendesha maisha. Happ ndo tunafeli zaidi, hapo tu.

Tusaidiane kuwa na maisha mazuri kijamii, kiuchumi na kisaikolojia. Ndo maana yangu kwa ufupi. Laana haina nafasi hapa.

M.B..... Tusisahau kunywa pombe.
 
Tusisahau kunywa pombe
Duh😂
 
hilo haliwezekani mkuu mpaka yesu anarudi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…