Nestory Semeni
Member
- Jul 8, 2024
- 19
- 37
Jana saa kumi jioni nilihisi kuchoka na kama kukata tamaa vile,
Na kuona mbona ni kama najitahidi kupambana na ninarudishwa nyuma,
Yaani ni kama kuna nguvu zinanifanya nisipige hatua na hata mimi sioni ni nguvu zipi,
Tukio lililonifanya nifike hapa ni swala la dharura ambalo lilinifanya nitumie pesa yote niliyoweka ya akiba,
Na nilikuwa na mipango nayo kweli hiyo pesa na basi dharura ni dharura ikabd pesa itumike,
Lakini nikaa na kufikiria kuhusu swla hili na nikakumbuka kitabu kimoja nilisomaga kuhusu matumizi ya mida,
Mwandishi aliandika "usijiulize ni muda gani umepoteza ila jiulize umebakiwa na muda gani na unatakiwa kuutumiaje?"
Ndipo na mimi nikajiuliza "Hivi nimebakiwa na nini?"
Ni kweli nimetumia akiba yote
Lakini sio kwamba nimeachwa tupu kwamba kesho siwezi kuamka na kupambana,
Nguvu na akili zangu hazijaondoka pia bado ninazo,
Sasa kwa nini nianze kulaumu? Na huku kuna vitu vingi zaidi vimebaki?
Hili ni jambo muhimu sana kwa kila mtu
Maana mara nyingi huwa tunapuuza vile vichache vilivyobaki kwa sababu ya vile vingi vilivyoondoka,
Na kwa bahati mbaya tusichojua ni hiki
Hakuna ambaye anaachwa bila kitu,
Ujue hata huo uzoefu yani kumbukumbu kwamba niliweka akiba na dharura ilitokea akiba yote ikaenda,
Ni muhimu sana kunisaidia kwenye kupambana,
Mana kwa ufupi natakiwa kuhakikisha naongeza bidii ya kupambana
Au hata wakati mwingine kuangalia namna bora zaidi ya kushughulikia dharura kuliko kutoa akiba
Hivyo mpendwa,
Kama unajiona upo kwenye hali isiyoeleweka
Au huko mbele ukijiona kwenye hali kama hiyo
Kupata vitu na baadae kupotea
NI vema kujiuliza "Umebakiwa na nini?"
Na hicho kilichobaki kitumie kupata kila kitu kilichopotea,
Na ni ngumu kupoteza mara nyingine kwa sababu tayari ushajua chanzo cha kupotea vitu mara ya kwanza.
Wewe unasemaje kuhusu hili?
Na kuona mbona ni kama najitahidi kupambana na ninarudishwa nyuma,
Yaani ni kama kuna nguvu zinanifanya nisipige hatua na hata mimi sioni ni nguvu zipi,
Tukio lililonifanya nifike hapa ni swala la dharura ambalo lilinifanya nitumie pesa yote niliyoweka ya akiba,
Na nilikuwa na mipango nayo kweli hiyo pesa na basi dharura ni dharura ikabd pesa itumike,
Lakini nikaa na kufikiria kuhusu swla hili na nikakumbuka kitabu kimoja nilisomaga kuhusu matumizi ya mida,
Mwandishi aliandika "usijiulize ni muda gani umepoteza ila jiulize umebakiwa na muda gani na unatakiwa kuutumiaje?"
Ndipo na mimi nikajiuliza "Hivi nimebakiwa na nini?"
Ni kweli nimetumia akiba yote
Lakini sio kwamba nimeachwa tupu kwamba kesho siwezi kuamka na kupambana,
Nguvu na akili zangu hazijaondoka pia bado ninazo,
Sasa kwa nini nianze kulaumu? Na huku kuna vitu vingi zaidi vimebaki?
Hili ni jambo muhimu sana kwa kila mtu
Maana mara nyingi huwa tunapuuza vile vichache vilivyobaki kwa sababu ya vile vingi vilivyoondoka,
Na kwa bahati mbaya tusichojua ni hiki
Hakuna ambaye anaachwa bila kitu,
Ujue hata huo uzoefu yani kumbukumbu kwamba niliweka akiba na dharura ilitokea akiba yote ikaenda,
Ni muhimu sana kunisaidia kwenye kupambana,
Mana kwa ufupi natakiwa kuhakikisha naongeza bidii ya kupambana
Au hata wakati mwingine kuangalia namna bora zaidi ya kushughulikia dharura kuliko kutoa akiba
Hivyo mpendwa,
Kama unajiona upo kwenye hali isiyoeleweka
Au huko mbele ukijiona kwenye hali kama hiyo
Kupata vitu na baadae kupotea
NI vema kujiuliza "Umebakiwa na nini?"
Na hicho kilichobaki kitumie kupata kila kitu kilichopotea,
Na ni ngumu kupoteza mara nyingine kwa sababu tayari ushajua chanzo cha kupotea vitu mara ya kwanza.
Wewe unasemaje kuhusu hili?