Ochutz,
Kwa bahati mbaya huna ujasiri wa kuandika jina lako la kweli, hivyo siwezi kujua Kama kweli ulinipa ushauri au umetunga tu. Ebu jiulize katika akili ya kawaida, Mimi na wewe ( au Chadema) nani angelimshauri mwenzake, wake moja Kati ya lengo la OPeration Pamoja Daima ni kuishinikiza Serikali kuboresha Daftari Hilo. Hayo yamesemwa na Mbowe, Lisu na Slaa! Kati yako wewe na Slaa ni nani Hana uelewa au nani ampe ushauri mwenzake. Ni vema tusifanye ushabiki katika mambo mazito.
Kama kweli ukielewa na una nia njema, badala ya kutuma ujumbe kwa Slaa, ungeandika kwenye Gazeti ili uishinikize Serikali kwa kuwa kazi ya kuboresha daftari ni ya Serikali na NEC yake. Aidha ungelikuwa na ujasiri wa kupostiwa kwa ID yako ningelijua Kama tuliongea la, kwa sasa hoja yako haina maana yeyote,
Nimejaribu kusoma tena na tena hii post ya Dr. Slaa, nikaona niijadili kwa jicho la tatu
Ni ujumbe mfupi sana, uliobeba maana nyingi sana na ubora wa Slaa kuwa kiongozi hakika unapatikana katika post za namna kama hii
Si mara ya kwanza kwa Dr. kulalamikiwa kuhusu aina ya lugha anayoitumia katika kujibu watu/wapinzani wake, na hii inapelekea kuhisi kuwa ID ya slaa inatumiwa na mwenzi wake, sitaenda huko
Assuming that this Post was written by Dr. Slaa, based on the contents naomba kuidadavua ifuatavyo
Kwa bahati mbaya huna ujasiri wa kuandika jina lako la kweli
Sijajua tone hii au lugha ya namna hii katika kuanza kumjibu mtoa hoja inatokea wapi?
''kwa bahati mbaya? Kuandika jina la kweli hakusaidii sana, maana sidhani kama kila unayekutana naye, au uliowahi kukutana nao huwa unawaandika kwenye diary-AU UNAWAKUMBUKA WOTE???. Sidhani kama angekuwa ameandika jina la kweli , mtoa maada asingefikisha ujumbe aliokusudia. I mean nikfikiria hii sentensi na status ya mwandikaji napata shida kidogo kujua kuwa ' aliandika ili mradi kuandika au kuna kitu?? HOJA IKO MEZANI na aliyetoa hata kama ni nyani maadamu ina faida basi alipaswa kujibiwa. Hii sentensi ni kiashiria au dalili ya kwanza ya
defence mechanism/kujilinda
hivyo siwezi kujua Kama kweli ulinipa ushauri au umetunga tu
Waandishi wa aina hii , wanaoandika kwenye public ni wale ambao; kwanza huawa hawataki kuonekana wamekosea, pili, ni wale ambao status zao hawataki zishuke, tatu ni uandishi wa kukwepa majukumu
1. Iwe mtoa maada/hoja alitunga au hakutunga; kwa statu yako hauna uwezo wa kuwakumbuka watu wote unaokutana nao. Hivyo kama kiongozi wa watu hakupaswa kuweka neno ''AU UMETUNGA''. Ili neno ''au umetunga', linaendeleza ''defence mechanism' ambayo umeianza hapo awali. Kwa level yako ukimchukulia mtu positively, na kila asemacho ni positive kwako na chama chako, basi utagundua kuwa wenye mapenzi na chadema ni wengi sana, ila lugha zenu nyie viongozi zimewakimbiza wengi, na sababu nitaitoa. Kwa lugha nyingine ni kuwa USHAURI UTAUPOKEA TU KWA MTU UNAYEMFAHAMU kwa jina, I mean pengine kwa watu wa karibu sana na wewe au na nyie. na hii ni dalili ya
''progressive defencive mechanism''kuwa mmechora mstari kuwa kuna watu wa kuwapa ushauri na ushauri huo lazima uwafurahishe
''Ebu jiulize katika akili ya kawaida, Mimi na wewe ( au Chadema) nani angelimshauri mwenzake''
Hapa unaanza sasa kujifunua vizuri. au ku reveal tatizo- Hapo juu tulikuwa tunaangalia defencive mechanism, ambayo sijaeleza chanzo chake, ila nilikuahidi msomaji utazijua, hapo juu Dr. Slaa ametusaidia kuanza kujua chanzo cha kuanza kujibu vibaya, na kuendeleza kujibu vibaya
Dr. slaa ana kiburi cha ujuvi/ ujuaji/much know-wengi wenye kiburi au mtazamo wa aina hii, huwa hawashauriki, hawaambiliki, ni watu wenye wivu, watu wasiotaka kushindwa au kuonekana wamekosea. watu wa tabia hii huawa hawataki kukosolewa. watu wa tabia hii ni wababe, ni watu ambao huwa anapelekwa kwa hisia zaidi. wapenzi wasomaji, sio kuwa natunga, waweza acha kusoma kwa dakika jiangalie na wewe ulipokuwa katika hali hii ya ujuvi/ujuaji kama wa Dr. slaa ulikubali ushauri kirahisi?? sisi ni wote ni binadamu na si kuwa Dr. pekee ndie mwenye tatizo. hata hivyo hapa tumemuona yeye ana tatizo
Sisi, wahandisi huwa tuna msemo ' idea is an idea' it can come from anybody. Huko marekani, kuna jengo kubwa lilijengwa na zile lift za ndani za kawaida, traffic ya watu ikawa kubwa na hivyo kulazimika wahandisi, wasanifu majengo na client kuanza kuwaza namna gani ya kuweza kuongeza lift shaft nyingine; kwa hiyo wakawaza na kupanga sehemu ya kubomoa. kwa bahati nzuri katika jengo hilo la ghorofa wakati wanapita kuangalia sehemu ya kubomoa na ku plan kazi itakuwaje wakamkuta mfagizi ambaye aliwasikiliza kwa makini mipango na mijadala yao ya kubomoa. Yeye mfagizi hofu yake ilikuwa kazi itakuwa kubwa ya kusafisha hilo jengo. Akapaaza sauti na kuwaambia, HALLOW HILO MNALOPANGA MSILIFANYE, SITAWARUHUSU MFANYE HIVYO, FIKIRIENI NJIA BORA YA KUTATUA TATIZO' magwiji hawa, ma expert hawa wakiwa wanashangaa maneno ya yule jamaa na kuwa anajiamini nini? injinia mmoja wapo akamueleza tatizo na akasema laima wavunje lile eneo, na asiwe na hofu juu ya usafi. akawaambia kwa upole hivi ndugu injinia, kuliko kuvunja humu ndani haiwezekani lift ikawa nje ikawa aina ambaa ambaa ukutani na kushusha watu kwenye corridor?? wale ma expert wakaangaliana wote wakaenda kumshika mkono. Lift ya kwanza ya nje katika histoa ya dunia hii ilijengwa katika jengo hilo na idea ilitoka kwa mfagizi.
Dr. slaa kuna watu wako nje ya ulingo wa siasa they know better than you, wanaweza kutoa ushauri bora kuliko nyie, na wanaweza kuwakumbusha yaliyo bora; ushauri wa watu wa aina hii, ni kama kufikiria nje ya box. samahani kuwa ulitaka kuwa rais wakati basics hizi hauna
''moja Kati ya lengo la OPeration Pamoja Daima ni kuishinikiza Serikali kuboresha Daftari Hilo''
Ohh my God, where were are you all this while? hili ndio jibu sasa, natamani ungeandika japo sentensi hii moja tu, sentensi iliyobeba information, na imeshiba kiasi ambacho ungemweleza hivi muanzisha tangu mwanzo angefarijika, ebu just imagine, na huwa hamuliwazii hili hakuna kitu kinauma kama kutoa wazo zuri kwa unayempenda na akalikataa au kukukejeli. This has been happening here over and over, impacts zake mnaziona ndogo sana. Ila ukiwa kama mtu ambaye una IDEA YA uchungaji, USINGEPENDA HATA KONDOO MMOJA APOTEE kwa namna yeyote ile. Dhana hii mmeishindwa kwa viongozi wenzenu, sembuse kwa huyu asiye na ID?? ( fikiri kidogo hapa nakuambia jambo kubwa Mr.) Lugha ya upole, upendo na uungwana inashinda HILA ZOTE
Hayo yamesemwa na Mbowe, Lisu na Slaa!
Hii sentensi ndugu msomaji sio ya kawaida pia. Kwake Slaa, anamaanisha kuwa royal na kuwa ana mapenzi sana na Mbowe na Lissu. Ila nina vyojua Operation ile ni ya wana chadema wote na alipaswa kusema kuwa hayo yamesemwa na chadema hii pia itawafanya wanachadema wengine kila sehemu kujiona ni sehemu ya chama. Kutaja majina na umuhimu wa watu fulani imekuwa ni kawaida ya chadema kwa siku za hivi karibuni. Chadema ndani ya chama kuna makundi, kuna walio karibu na viongozi, hao ndio wanaoonekana wenye chama.
Slaa kwa status yake na situation alionayo sasa, lazima aonyeshe kumheshimu Mbowe, na kwa sababu hana jinsi ya kupambana na Lissu,ambaye atamuonyesha pia anamjali. Ila kwa viashiria vya hapo juu slaa is not a trusted leader. Ukiwa inferior kwa kutaja majina hivi ni dalili ya woga , na hili linajulikana, apart of being a padre, Dr. slaa hana professional nyingine yeyote. Hivyo ili kuendelea kuwa katibu lazima aitetee nafasi hii kwa namna yeyote ile.
Kati yako wewe na Slaa ni nani Hana uelewa au nani ampe ushauri mwenzake
Rudia mfano wa hapo juu wa mfagizi, binadamu was created kutegemeana na right after creation ( evolution??) mwanaume akapewa msaidizi, swala la kusaidiana na different ideas ndio iliyoileta dunia hapa tulipo leo. Muda usingetosha kukueleza how ordinary people wameibadilisha dunia kwa idea tu, people who did not even went to school, but their thought and ideas were the most valuable asset that the world is still enjoying today. Lugha yako haijakaa ku inspire, kukuza vipaji, kuongoza, kulinda na kupenda. Lugha yako imejaa umimi, na ni aghalabu kukosolewa. Lugha yako na aina ya watu kama wewe wako radhi hata kuua ili mradi walinde heshima zao. na ntakueleza jambo ambao hata wewe utalikubali. Naomba niandike hapa
kadiri siku zinavyoenda mbele ndivyo hata wewe unathibitisha kuwa hakukufaa kuwa rais wa Tanzania
tusifanye ushabiki katika mambo mazito.
Hii sentensi ni moja ya sentensi inayorudiwa sana na slaa akatika kujitetea. Hamna mantiki ya kuandika hii sentensi maana mtoa hoja hajaonyesha ushabiki wowote ule, na ameonyesha seriousness katika daftari la wapiga kura, kizuri hajatoa kashfa yoyote kwako. Sitajadili hili, hapa Dr. alikuwa ananogesha tu post na kutafuta sympathy
badala ya kutuma ujumbe kwa Slaa, ungeandika kwenye Gazeti ili uishinikize Serikali
Huyu mtu (mtoa maada) anatafuta ujiko wa kuwa aliwahi kuongea na wewe, umeikosa hiyo nafasi ya kuwa awe wako, umemfukuza kwa sentensi zako zisizo na busara. Kibaya zaidi katika sentensi yako hii unakataa majukumu yako. Hapa umechekesha. Kakuambia wewe, akiamini ni kiongozi na utafanya jambo, kuaminiwa huku ndio mtaji wako wewe Dr., inapokuja swala la kukataa majukumu kwa kejeli , ungekuwa rais ingekuwaje?? Umefukuza kondoo hapa. Kila mmoja aende gazetini??? plz cry
kwa kuwa kazi ya kuboresha daftari ni ya Serikali na NEC yake
Umesahau uliishasema kuwa OPD lengo ni kuishinikiza serikali iboreshe daftari?? Na mtoa maada anakueleza umuhimu wa hilo?? Ungemjibu vizuri kuwa asante kwa ushauri na tunapigania hilo, ungepungukiwa nini?? kila mmoja aende gezetini???? Jamani nisaidieni. CDM ni taasisi, watu wanapotoa maoni wanatoa maoni kama vile taasisi iliyoaminiwa ambayo inaweza kukamata dola. Piga mahesabu ungekuwa rais sasa mtu anakuja na ushauri au hoja unamwambia aende gezetini
Hivi Slaa usipojitambua kuwa ulitakiwa kuwa rais na matendo yako yanatakiwa yafanane na hilo, nani atakusaidia?? Waberoya nachoka sana kuandika maneno meengi kisa kuku-tune na kuku-shape uweze ingia ikulu, sio fair kabisa unanipotezea muda. Mpaka leo hauna attributes wala dalili ya kuwa ulitakiwa kuwa ikulu, na kuwa baba wa familia kubwa inayoitwa Tanzania, pole sana
ID yako ningelijua Kama tuliongea la, kwa sasa hoja yako haina maana yeyote
Umemalizia kwa kuhuzunisha sana, umekwepa jukumu, umemfukuza kondoo, umejitanabaisha na kutambulika kuwa siyo kiongozi. Hoja hiyo ina maana sana, woga wako na hofu ndio vinakupelekea kusema hivyo
Slaa, mmefukuzana sana ndani ya CDM na kumbuka action and reaction are equal ulichoonyesha hapa ni athari za kisaikolojia zinazokuandama, meishaitana wasaliti na hautamwamini mtu yeyote dhambi hiyo itaendelea tu. Mtafukuzana sana na kwa sababu brain yako imejaa hayo mambo. Hakuna ushauri mzuri utakaoweza kupokea kwa sababu kila unayeona anakugusa hauoni zuri lake ila baya lake tena la kufikirika
Kwa mnayoyapitia kwa sasa ndani ya chadema na mlivyoleta damage in the past six months, lazima ujilinde, usionyeshwe kosa, upige kwa maneno n.k mnahitaji mshauri wa kuwaondolea tatizo lenu.
Ikiwa wewe mwenyekiti wa taifa wa CDM majibu yako yamejaa utumbo na uozo wa kama hivi, hao wengine wasio fikiriwa hata kuwa viongozi wao huwa ana react vipi?? Kama si matusi ya nguoni