Ng'wanapagi
JF-Expert Member
- Sep 18, 2013
- 9,116
- 8,658
Majuzi kati nilienda kumsalimia rafiki yangu Bukoba baada ya nyumba yake kupitiwa na tetemeko la ardhi pia nikavuka border kufuata vitu fulani vya biashara. Wakati naenda nilitoka Katoro saa 10:30 jioni na kutokana na tochi za trafiki hivyo basi lilikimbia chini ya spidi 80Kmph na kusababisha kupita maeneo ya wilaya ya Muleba ngiza likiwa tayari limeshaingia. Kutokana na hali hiyo sikuona madhari ya nje lkn siku narudi basi lilisimama kupisha lori lililokuwa na kokoto na ndani ya basi kila mtu alikomaa kupiga picha nje kwani kulikuwa na mti umefungwa chupa za maji hadi matawi ambayo si rahisi kuyafunga. Swali kuu na lililokosa jibu ni kwa nini chupa hizo zimefungwa kwa wingi katika mti huo!!?? Wenyeji wa Muleba tunaomba elimu kidogo hapa