Niliaibika sana, sitakaa nisahau

Niliaibika sana, sitakaa nisahau

Mimi nakumbuka siku hiyo ambayo tulikuwa darasa la kwanza karibia watoto 84, na kati ya hao ni wanne tu wanajua kuongea kiswahili, wengine wote wanazungumza kinyumbani tu....! Halafu alikuwepo kaka mmoja mkubwa kahamia shuleni kwetu akitokea darasa la tatu, na ndio mmojawapo wanaoweza kuongea kiswahili...! Sisi ndio tulikuwa waanzilishi wa shule ile....! Ghafla mkaka yule aliingia kwa kuchelewa na kumkuta mwalimu akifundisha...! Wote tulisimama kumsalimia "shikamoo kaka", viniginevyo tungekoma mwalimu akitoka....! Kumbe mezani mwalimu alikuwa na soda yake imefunguliwa na andazi...! Halafu wakati tunaandika yaliyoandikwa ubaoni, mwalimu akatoka nje (nafikiri alienda uani)...! Then, jamaa akainuka na kwenda mezani, akaling'ata lile andazi na kumezea soda ile pia...! Akarudi kukaa kule nyuma ya darasa...!
Kidogo mwalimu akarudi na kukuta andazi lake limemegwa....! Aliongea hadi kimeru (kikwao)...! Wale watoto wanne wanaojua kuongea kiswahili; akiwemo jamaa, walijitetea na kupewa kazi maalum kila mmoja...! Jamaa alipewa kazi ya kuhakikisha kila atakayechapwa atarudi kuunga mstari tena na kusubiri kuchapwa tena, wengine walipewa kazi ya kukata fimbo....! Nakumbuka siku hiyo tulichapwa hadi saa ya kwenda nyumbani....! Hakuna hata mmoja aliyedhubutu kumnyooshea jamaa kidole, kisa ungepita njia gani baadaye....!
hahaaa!! kipindi hicho tulikuwa tunamwogopa mwanafunzi mbabe kuliko hata mwalimu
😀😀
 
Nakumbuka nilipokuwa primary kipindi hiko nilikuwa na girlfriend wangu ambaye tulikuwa tunaishi jirani na tunasoma shule moja, darasa moja na dawati moja. Kila siku tulikuwa tunaenda shuleni pamoja na tunarudi pamoja nyumbani.

Ulikuwa ukinikosa nyumbani basi ujue nko kwao, na kila weekend tulikuwa tunashinda pamoja mpaka tunasahau kama kuna kula. Nakumbuka baba angu alikuwa akinigombeza kuwa nmezidisha michezo sana mpaka perfomance yangu class ikawa inashuka na kusahau hata muda wa kurudi kula kisa michezo.

Sasa siku moja jumapili niliangalia movie sana mpaka mida ya saa 9 za usiku ndo nkaenda kulala, sasa asubuhi yake niliamka mchovu na nikakumbuka ni siku ya shule ikanibdi niende japo nilikuwa nasinzia sana njani huku nikielekea school.

Baada ya kufanya usafi tukaingia class. NILIKUWA NIPO DARASA LA TATU KIPINDI HICHO.
Sasa tulipoingia tena class saa 13:00 baada ya kutoka lunch, tena lunch yenyewe ni makande na jinsi maharage yalivyokuwa na usingizi.

Nikawa NASINZIA mbayaa ukijumlisha tena na jana Kuchelewa kulala ndo ikawa balaa sana. ilikuwa ni somo la English hvyo teacher alivyoingia na kuanza kufundishwa nikawa nimepitiwa na usingizi baada ya ule uchovu mkali.

Punde kidogo nkashtushwa na yule girlfriend wangu kuwa teacher alikuwa amenipoint mm nijibu swali. aaaagrrh! hapo nkashtuka balaaa alafu na hata hili swali lenyewe nlikuwa sijui kaulizaje. basi nikawa nabababika tuu mara teacher akarudia tena kuuliza "what the meaning of TOGETHER?"

Basi nkawa nababaika bila kujua nijibu vipi ila nkasikia yule GF wangu akiniambia kwa mbali "jibu lake ni TUNAWAKILISHA"Heeeeh! basi na mimi ikavuta picha huku nikipambanua lile jibu nililolisikia nikalicombine na lile neno ka kwenye Chanel 5 kuwa wanaandikaga "TOGETHER, TUNAWAKILISHA" basi hapo nikaona Ewaaah! hili ndo jubu, nikajibu kwa sauti kubwa huku nikihiamini kuwa jibu lake ni TUNAWAKILISHA.

Heeh! mara nikasikia kila mtu kaduwaa baada ya hapo wanafunzi pamoja na mwalimu wakacheka mbayaaaa.Basi hyo siku nilichekwa sana karibia siku nzima mpaka nikawa sina raha. keaho yake pia nilipikuja shule wakawa tayari wameshanibatiza jina naitwa TUNAWAKILISHA. ikawa kila mahali nikipita naitwa tunawakilisha, tubawakilisha mpaka jina nikalizoea mpka namaliza darasa la 7 nikawa naitwa hivyo hvyo Tunawakilisha.Tunawakilisha.

YANI ILIKUWA NI AIBU AMBAYO MPAKA SASA HIVI NAONA IMEZIDI KULIKO AIBU ZOTE ZILIZOWAHI KUNIPATA.Je na wewe mdau unakumbuka ulipikuwa scul ni aibu gani ilishawahi kukupa/kukumba?
Mkuu kuna jambo umetuficha hapa.usingizi uliokua nao ukichanganya na yale maharage haikosi kulikua na ushuzi wa matarumbeta.
 
kwani maana ya Girlfriend si rafiki wa kike, ila siyo kwamba alikuwa dem wangu. Hapana mkuu
vipi ujawahi kuwa na boyfriend au mlipotezana mlipo maliza skul
 
Umetisha baab,imefanana na moja ilitokea mahakamani mshtaki katukanwa wakiwa kwenye chumba cha mahakamu hakimu akamuuliza mshtaki unaweza sema mshtakiwa alikutukanaje...Mshtaki akasema hapana hakimu siwezi taja alivyonitukana labda niandike halafu wazee wa mahakama wanisaidie kusoma hakimu akamkubalia, akandika kuwa mshtakiwa alimuambia "Twende tukadu" aliandika bila tafsida hapo nimepyunguza ukali wa maneno...Basi kikaratsi kile akapewa mzee wa mahakama mwanamke asome yule mzee akaona soo...Akampa mzee wa mahakama aliekuwa pembeni yake kumbe yule mzee wa pembeni alikuwa amelala...Yule mama mzee wa mahakama akamgusa kwa taratibu yule mzee alivyoamka akamsogezea hicho kikaratasi..kilichaondikwa ''TWENDE TUKADU" yule mzee bila kujua mahakam yote inamuangalia akamuuliza yule mama mzee wa mahakam aliempa hicho kikaratasi''EEH MAMA TWENDE SASA HIVI? Hakimu akaingilia kati kuwa we saidia mahakama kusoma maneno ya mshtaki si wewe umeulizwa...Mzee akaona soo mbaya.
ha hahahahahaha ha duh
 
acha kutuzingua,aibu gani hiyo kikosea maana ya neo la kiingereza tena ukiwa shule ya msingi? kaje na stori nyingine
 
Umetisha baab,imefanana na moja ilitokea mahakamani mshtaki katukanwa wakiwa kwenye chumba cha mahakamu hakimu akamuuliza mshtaki unaweza sema mshtakiwa alikutukanaje...Mshtaki akasema hapana hakimu siwezi taja alivyonitukana labda niandike halafu wazee wa mahakama wanisaidie kusoma hakimu akamkubalia, akandika kuwa mshtakiwa alimuambia "Twende tukadu" aliandika bila tafsida hapo nimepyunguza ukali wa maneno...Basi kikaratsi kile akapewa mzee wa mahakama mwanamke asome yule mzee akaona soo...Akampa mzee wa mahakama aliekuwa pembeni yake kumbe yule mzee wa pembeni alikuwa amelala...Yule mama mzee wa mahakama akamgusa kwa taratibu yule mzee alivyoamka akamsogezea hicho kikaratasi..kilichaondikwa ''TWENDE TUKADU" yule mzee bila kujua mahakam yote inamuangalia akamuuliza yule mama mzee wa mahakam aliempa hicho kikaratasi''EEH MAMA TWENDE SASA HIVI? Hakimu akaingilia kati kuwa we saidia mahakama kusoma maneno ya mshtaki si wewe umeulizwa...Mzee akaona soo mbaya.
Hahahahahaa uwiiiii
 
Duh, yaani wewe umesoma primary Wakati EATV ishaanzishwa??? Ha ha ha haaa... Kweli humu kuna watoto wengi sikuhizi. Halafu unaonekana unaendekeza mapenzi kuliko shule, no wonder kuna uzi umeandika "Number is don't lie"... ELIMU, ELIMU, ELIMU.
 
wakati nasoma primary EATV haikuanzishwa bado hivyo naona hii ni ya watoto zaidi ila hii imenifundisha kitu kuwa watoto wa siu hizi wanaingia kwenye mahusiano mapema, darasa la tatu ulikuwa na g'friend tayari? this is dangerous.
 
naona unaanza kulitengeneza tatizo, kwani nime mind ndio uniulize inanihusu nini, nimeuliza tu kama mazungumzo ya kawaida
haya sasa ngoja niangalie ngumi wakat ugomvi nmeanzisha mm
 
wakati nasoma primary EATV haikuanzishwa bado hivyo naona hii ni ya watoto zaidi ila hii imenifundisha kitu kuwa watoto wa siu hizi wanaingia kwenye mahusiano mapema, darasa la tatu ulikuwa na g'friend tayari? this is dangerous.
mtoto mwenye miaka 26? au wewe ni ajuza nini..
 
Girlfriend primary ndo mana mnakuwa hamna nguvu mnarukia vitu vya wakubwa mapema sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom