Infopaedia
JF-Expert Member
- Oct 28, 2011
- 1,231
- 1,496
Wakuu kuna movie flani niliiona kama 2008 au 2009 hivi. Hii movie siikumbuki jina, lakini nakumbuka baadhi ya sehemu zake. Part ninayoikumbuka ni kwenye ndege ya abiria. Kulikuwa na ugomvi kati ya pilot na jamaa fulani ambaye pia alikuwa anafahamiana na muhudumu wa ndege. Katika ule ugomvi, jamaa alidhibitiwa. Lakini alifanikiwa kuingia kwenye chumba chenye control circuit ya ndege na akafanikiwa kuchomoa auto pilot circuits. Baadae na yeye akawashinda mapilot. Lakini air hostess mmoja alifanikiwa kumzimisha yule bwana. Kasheshe ilikuwa ni jinsi ya kuishusha ile ndege wakati pilots wote wamezimia na auto pilot iko disabled. Ikabidi sasa ground control tower waanze kumuelekeza yule air hostess jinsi ya kulishusha lide dege. Ilikuwa ni ndege kubwa sana. Yule dada alifanikiwa kuishusha ile ndege lakini baada ya misukosuko mingi sana.
Natafuta jina la hii movie. Kama kuna mkuu yeyote ameiona hii movie na anakumbuka jina lake, naomba anikumbushe. Asanteni.
Natafuta jina la hii movie. Kama kuna mkuu yeyote ameiona hii movie na anakumbuka jina lake, naomba anikumbushe. Asanteni.