Nikubali au nikatae?

Nikubali au nikatae?

jungle boy

Senior Member
Joined
Aug 6, 2015
Posts
107
Reaction score
27
Habarini za jumatatu,

Kuna mdada mmoja ni jirani yangu ana mume na watoto, mara nyingi nimekuwa nikimsaidia kumrekebishia simu yake(Android) kutokana na yeye kushindwa kujua baahi ya vitu fulan kwa iyo likitokea tatizo au kama wwhatsapp imezingua mara nyingi huniomba nimsaidie.

Sasa leo nimeonana naye baada ya kusalimiana nae akanambia japo akapinda kona(kanificha) lakini mwisho mi nikaja kujua kuwa mumewe ana kamchepuko sasa anataka amjue mwanamke uyo.

Kwa hiyo akaniomba nimsaidie kuijua iyo namba pale anapowasiliana naye nikamkatalia na kumwambia hata ukijua haitasaidia kwa sababu anaweza kubadili akatumia simu nyingine lakini ni mng'ang'anizi mwisho nikamwambia hiyo inawezekana lakini ni lazima simu ya mumewe ianze kuwekewa iyo program(application).

Akasema hilo halina tatizo mi nitambadilishia ntampa yangu uweke then baadae nitaichukua yangu na kumpa yake duuh yaan uyu mdada kadhamiria lakini mimi naona its meaningless kufanya ivyo na kuhusu mumewe hajui kabisa masuala ya simu za android mara nyingi mimi ndio huwa nawasaidia lakini pia sitaki kufanya ivi.

Naombeni mnisaidie nimkwepe vipi huyu dada maana kwangu itakuwa kero
 
Mkuu achana nae...umemsaidia mambo muhimu kuhusu simu inatosha...
 
Dogo kuna msala utamwangukia siku si nyingi


Endelea kujihusisha na yasiyo kuhusu hadi siku huyo mumewe
atakapo amini unatembea na mkewe.....ndio utajua faida ya kujihusisha na yasiyo kuhusu

Ngoja tu vuguvugu la mchepuko liishe
 
Endelea tu dogo,siku zako za kuliwa kiboga zinakaribia
 
Nashukuruni nyooooote ntazingatia ushauri wenu wakuu
 
Muwekee tu..andaa na chumba kabisa..akiachika aje kukaa kwako
 
Hiyo ni hatari mkuu...,acha!
Ni kama kumshika sharubu simba jike huku ukijua kafungiwa kwenye box tu
 
Wewe mwanaume unajihusisha na issue zisizokuhusu. Fanya yako kaka utaua watu kwa pressure, simu zetu zinaficha mengi.
 
Ze great sinker anaomba ushauri,,

Hapo kuna ugumu gani kumwambia kile unachokiona ni sahihi??? mpaka kutaka kujaza serve kwa mambo madogo kama hayo??? kweli???? mbona jibu liko wazi??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom