Niko njiapanda ya kuchagua dini sahihi

Niko njiapanda ya kuchagua dini sahihi

nodetz

Senior Member
Joined
May 4, 2024
Posts
173
Reaction score
156
Habari wana jf leo ninaswala gumu linanitatiza naitaji maoni yenu.

Kama binadamu wengine namuamini mungu.

Ila napata wakati mugumu kuchagua dini ya kuabudia. Nikisema hivyo namaanisha mini ni mtu ambaye napenda kujifunza sana.

Na kijifunza kwanga kumefanya nibadili jinsi ninavyo itizama dini yangu iliyonelea (ukristo)

Nimekulia katika familia inayo abudua kupitia roman Catholic ila miaka mitano nyuma baada ya kujifunza na kuelewa vitu fulani mimi kama binadamu ninahaki ya kuchagua wapi nikaabudu ivyo nikaamua kubadili na kuwa katika makanisa ya kilokole.

Now nimwaka wa pili sasa huwa najiuliza kama uamuzi niliofanya ni sahihi make najikuta naitaji kubadili tena na safari hii naonelea zaidi kuwa mwisilam (dini ninayoipenda zaidi).

Kinacho nisukuma kufanya hivi sio nafata mkumbo hapana ila kunavitu vingi uwa vinanipa mwaswali na hayo maswali yakikosa majibu basi huwa naitaji kubadilisha msimamo wangu.

Nitaepuka kuweka maswali hayo hapa ili nisianzishe mjadala wa kinidi.

Kiukweli kabisa niko njia panda na ukizingatia naelewa pia sio rahisi kumwamini mungu kwa kuto shiriki katika dini yoyote maana utakosa malezi ya kidini japo wengine ufikili kuingia kwenye dini ni kama kujiingiza kwenye jela yako mwenyewe.

Ntashukulu kwa maoni yako mwana jf.
 
C
FB_IMG_17502178278845793.jpg
hagua ayatollahrian
 
Kinachokutatiza ni kitu kimoja tu mkuu
Unatumia akili (logic) katika kuchanganua mambo ya dini yako hiyo kitu kinachokufanya uanze kujiuliza jambo fulani linawezekana vipi. Ukitaka kuwa muumini mtiifu wa dini yoyote ni lazima uamini bila kuhoji mistari katika vitabu hivyo vya dini. Maneno kadhaa ya kwenye biblia na Quran hayaendani na uhalisia kwa hiyo we chagua tu dini moja iamini hivyo hivyo.

Kubwa kuliko yote ukitaka kuwa muumini mzuri wa dini fulani basi usitumie philosophy katika kuchanganua mambo ya kidini.
 
Do the right things, tenda wema kwa watu, wanyama na kila chenye uhai na jiepushe na ubaya wowote hasa kwa kiumbe chenye uhai that's enough mkuu, Love itself is a religion, it is our religion. 💚
 
Kinachokutatiza ni kitu kimoja tu mkuu
Unatumika akili (logic) katika kuchanganua mambo ya dini yako hiyo kitu kinachokufanya uanze kujiuliza jambo fulani linawezekana vipi. Ukitaka kuwa muumini mtiifu wa dini yoyote ni lazima uamini bila kuhoji mistari katika vitabu hivyo vya dini. Maneno kadhaa ya kwenye biblia na Quran hayaendani na uhalisia kwa hiyo we chagua tu dini moja iamini hivyo hivyo.

Kubwa kuliko yote ukitaka kuwa muumini mzuri wa dini fulani basi usitumie philosophy katika kuchanganua mambo ya kidini.
Simply unatakiwa uwe zuzu right??
 
Siku zote ukweli haujifichi ndugu yangu hakika ndani ya nafsi yako kuna yakini imekuingia hasa kuhusu ww kuingia kwenye uislamu na jambo hili najua umelifanyia utafiti na kipo ulichokigundua
Mm nakuombea kwa mwenyezi mungu akuongozee kwenye njia iliyoonyoka
 
Kinachokutatiza ni kitu kimoja tu mkuu
Unatumia akili (logic) katika kuchanganua mambo ya dini yako hiyo kitu kinachokufanya uanze kujiuliza jambo fulani linawezekana vipi. Ukitaka kuwa muumini mtiifu wa dini yoyote ni lazima uamini bila kuhoji mistari katika vitabu hivyo vya dini. Maneno kadhaa ya kwenye biblia na Quran hayaendani na uhalisia kwa hiyo we chagua tu dini moja iamini hivyo hivyo.

Kubwa kuliko yote ukitaka kuwa muumini mzuri wa dini fulani basi usitumie philosophy katika kuchanganua mambo ya kidini.
Asante ila sijawai na siwezi kuamin kitu ambacho sikijui
 
Binadamu tumechagua njia rahisi ya kumfuata Mungu ambayo ni dini. Nikivaa kanzu na tasbihi yangu na nikionekana kanisani kila siku basi nakuwa mcha Mungu kuliko Masoud ya Mbagala Kizuiani ambaye hajulikani ni dini ipi ila siku zote ameishi maisha ya kumpenda na kumtendea mazuri kila mtu.

IMANI NI BORA KULIKO DINI.
 
Back
Top Bottom