Ennie
JF-Expert Member
- Jan 15, 2011
- 7,137
- 4,122
Dada yangu alinitumia sms kuwa yu mjamzito nikaenda kumuona,nikajaribu kuhoji baba wa mtoto ni nani na kwa nini hawafungi ndoa? Akadai wanamipango hiyo. Juzi akanitumia sms kuwa jamaa ni mume wa mtu! Namchukia mwanaume yeyote anaye-cheat hata kama ni kaka yangu na dada anajua hilo. Nimemwambia sitaki kumuona huyo jamaa lakini mimi ndio dada pekee hivyo anahitaji msaada wangu akijifungua maana ndio mtoto wake wa kwanza(mimi nina wa 3). Nitawezaje kumu assist dada yangu bila kuwasiliana na baba wa mtoto aliyemsaliti mkewe? Sitaki hata kumuona!