Nikaione hali ya Godbless Lema Arusha

Nikaione hali ya Godbless Lema Arusha

Status
Not open for further replies.
Pesa nyingi zimemwagwa Arusha na CCM za kuhonga ili madiwani na mbunge washinde Arusha. Bendera zao kwenye kila mtaa wa jiji ni wanajaribu kuonyesha kwamba CCM bado iko hai. Kusema la ukweli watu hapa A-City wameichoka CCM, hata waweke bendera zao mpaka mlima Kilimanjaro wanajisumbua tu. Lema hana mpinzani na atashinda kwa kishindo.
 
Nipo Arusha wiki 2 sasa pia nilikua ninahamu sana nione hali ya lema huku jimboni kwake. Nilichokiona na kusikia pia ni kua ameshapita hana hata haja yakupiga kampeni huku ni ✌✌ dam dam"
 
Bado uko mbali karibu sana Arusha tumezoea kubadilisha wabunge kadri tunavyopenda sasa hivi tunapiga chini lema

Kaka Petro huyu hata Korogwe hajawahi kuvuka achana naye.Karibu kwetu Arusha.Lema for real.
 
MCCM hayapo arusha kabisa, siku monabani anahutubia kiwanja cha texi sanawari alikuwa na watu 17 tuu ikabidi daladala moja ikasombe ndugu zake wakafika kama 40 ndio akahutubia mkutano na huo mkutano ulikuwa pia uzinduzi wa diwani wa ccm kata ya sekei. Diwani wa sekei hadhubutu kufanya mkutano wa hadhara kwani hana wa kumhutubia. subiria tarehe 25 hakuna hata kata moja itakayochukuliwa na mccm wala act zote ni Chadema tuuu. Na mbunge wetu ni Lema tena.
 
Namshauri Lena sasa aende Mtera, Iramba na Mtama akamwage sumu kwa wale vidomodomo maana nyumbani hali shwari.
 
Arusha ndio kambi ya mabadiliko ,hongereni sana,huku dar tupo na bingwa kuiba kura hapa ubungo ila tumempa saizi yakeee Kubenea haibiwi hata moja
 
Niko njiani kwenda Arusha kuhudhuria Semina za kiwakili na Mkutano wa nusu mwaka wa Mawakili utakaofanyika tarehe 26 mwezi huu. Nitakuwa Arusha hadi Jumapili ijayo.

Uwepo wangu Arusha utanipa fursa ya kuona hali ya kisiasa ya Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema dhidi ya Monaban wa CCM kuelekea uchaguzi wa Oktoba 25. Hodini wanaJF wa Arusha.

Karibu mkuu ukutane na wadau, bila shaka upo AICC na Tanzania Law Society ...... Karibu sana wana Arusha ni wakarimu, nitakupeleka kwenye nyama ya Mbuzi kwa Morombo hahaha
 
Miaka mitano ya Lema imekuwa miaka ya kulala sero na kesi kibao kisa maandamano yasiyokuwa na tija....

Sasa hivi watu hawataki maandamno , walishapata hasara na zimetosha...

Kina mama wa soko la kilombero hawamtaki...kisa analeta vurugu kwenye biashara za watu.

Japo kuja kwa Lowassa ukawa kunaweza kukawa na unafuu kwake akashinda....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom