Hivi familia ina nafasi kiasi gani kwenye suala zima la ndoa jamani hebu nijuzeni,na je ni haki wao kukupangia uolewe na nani au umuoe nani?
asante sana bacha na je kwa mfano ndugu zako wanamkataa mchumba wako kwa sababu ambazo wao wanaziamini ndivyo wakati wewe unaamini sivyo ilivyo kabisa,utakubaliana nao tu kwa sababu wameamini kitu ambacho si sahihi au ufanyeje?msaada plzswali lako ni zuri, isitoshe naliona linahitaji majibu yenye uchambuzi wa kina kidogo......
Binafsi naona inategemea mambo mengi kidogo.......
1. Malezi yako na familia yako kwa ujumla
2. Misimamo ya wazazi wako kuhusu mustakabhali wa maisha yako
3. Msimamo /mtizamo wako wewe mwenyewe
4. Aina ya maisha ya kifamilia unayotokea, je ni conservative au liberal?
Na mengineyo mengi tu, hata hivyo kwa maisha ya sasa si vema kumchagulia mtoto mpenzi wa kufunga nae ndoa!
maisha yamekuwa ni ya mchangamano sana,hasa katika karne hii ya sasa, wakati mwingine umdhanie ndiye kumbe sie..................
Mzazi anapaswa kumuongoza mtoto kwenye mwelekeo ulio bora katika kumpata mwenza wa maisha yake,
lakini asitoe kauli ya mwisho katika kumchagulia mwenza,
kwani tunaambiwa kuwa,mke/mume bora hutoka kwa mungu.....................(maandiko ya mungu)
Familia inanafasi kubwa sana haswa ktk tamaduni zetu waafrica, kifupi tunasema "in african culture or traditions society/clan/family is our prime centre, i mean mtu hutakwa kufanya mambo kwa kulingana na society moral and values, kwa wazungu individual person ndio basic unity yan mtu hufanya mambo pasipo ingiliwa na mtu and that is what they call it as Liberty!
Ktk swala la ndoa kwa values za ki africa, Familia inanafasi kubwa sana, familia kuhakikisha kizazi chake kinaenda vizuri hutumia muda mwingi kuchunguza wachumba wa wanao b4 ndoa, na huwa wakali sana ktk maamuzi.
Hivi familia ina nafasi kiasi gani kwenye suala zima la ndoa jamani hebu nijuzeni,na je ni haki wao kukupangia uolewe na nani au umuoe nani?
thanx BPM nimekupata
Shadakta!!! umenenaswali lako ni zuri, isitoshe naliona linahitaji majibu yenye uchambuzi wa kina kidogo......
Binafsi naona inategemea mambo mengi kidogo.......
1. Malezi yako na familia yako kwa ujumla
2. Misimamo ya wazazi wako kuhusu mustakabhali wa maisha yako
3. Msimamo /mtizamo wako wewe mwenyewe
4. Aina ya maisha ya kifamilia unayotokea, je ni conservative au liberal?
Na mengineyo mengi tu, hata hivyo kwa maisha ya sasa si vema kumchagulia mtoto mpenzi wa kufunga nae ndoa!
maisha yamekuwa ni ya mchangamano sana,hasa katika karne hii ya sasa, wakati mwingine umdhanie ndiye kumbe sie..................
Mzazi anapaswa kumuongoza mtoto kwenye mwelekeo ulio bora katika kumpata mwenza wa maisha yake,
lakini asitoe kauli ya mwisho katika kumchagulia mwenza,
kwani tunaambiwa kuwa,mke/mume bora hutoka kwa mungu.....................(maandiko ya mungu)
asante sana bacha na je kwa mfano ndugu zako wanamkataa mchumba wako kwa sababu ambazo wao wanaziamini ndivyo wakati wewe unaamini sivyo ilivyo kabisa,utakubaliana nao tu kwa sababu wameamini kitu ambacho si sahihi au ufanyeje?msaada plz
nadhani majibu nimeyatoa kwenye maelezo yangu ya awali....,
inakupasa weye kupima kwanza;
je, wao wanavigezo gani au sababu gani za msingi za kumkataa?
je, wanamjua vizuri au nao wanapewa stori za kuambiwa?
Kumbuka pia si vema kukataa kila neno, ila lazima pia uwe na busara katika kukataa,
na jipe muda wa kuchunguza kinachosemwa hapo..........
isitoshe hiyo ndo maana halisi ya kipindi cha uchumba.....(kipindi cha kupimana uaminifu na thamani ya upendo wenu)
Ila mwisho wa siku weye ndo muamuzi wa mwisho, usuke au unyoe!kwasababu maisha mtakayoishi yatakuwa yenu nyie wawili,
na wala si ndugu zako...........
Maandiko yanasema, "Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye, bali mke mwenye busara mtu hupewa na Bwana" (Mithali 19:14).
Ninaamini, inatupasa kumshirikisha Mungu pale tunapotafuta wenzi wetu. Na vizuri kupata ushauri toka kwa wazazi, lakini the final decision ni ya kwako pale ukiamini uliyempata, ametoka kwa Mungu. Kila la heri na ubarikiwe.
kama siajkosea zbena uliwahi kuleta topic nyingine inayofanana na hii. Pole maana naamini ni kitu kinachokugusa. Nikujibu tu kuwa ukweli ni kuwa watu wanapooana, automatically wanakuwa sehemu za familia za wakwe zao. Maisha yanahitaji upendo hasa kutoka kwa wale wanaokuzunguka. sidhani kama kuna mtu atapenda aishi maisha ambayo majority ya wanaomzunguka na ndugu na jamaa wananchukia. Ni maisha mabaya sana na unaweza kujuta hata kuyaishi. Hata hivyo kuhusu suala la kupendwa na wakwe, halipo direct sana. Kabla mtu hajaoa au kuolewa, wazazi na ndugu wanakuwa wana-preference zao za mtu ambaye ambaye wanaamini akiongezwa katika familia yao itakuwa poa. Hata hivyo, tena kwa experience kubwa kuanzia kwangu mwenyewe, kwa ndgu zangu na kwa marafiki zangu, hali hubadilika sana baada ya huyo mkwe kuja katika familia. Unakuta wakwe walipenda pengine kabila fulani, elimu fulani, rangi fulani, ukoo fulani, dini fulani nk. Atakapoolewa yule 'anayetakiwa', huchukuwa miezi kadhaa ya kupendwa kwa mujibu wa zile sifa alizo nazo, lakini baada ya hapo kinachomfanya mtu apendwe au achukiwe ni tabia yake. Wapo waliokuwa wanapendwa sana wakati wa kuolewa, lakini miezi michache baadae walikuwa wanachukiwa na kila mtu, na wapo waliokuwa wanachukiwa au kudharauliwa wakati wanaolewa, lakini baadae walipendwa na kuheshimiwa na kila mtu. So it depends una-behave vipi katika jamii yako mpya