Pendaelli
JF-Expert Member
- Feb 13, 2014
- 8,920
- 23,246
Tupo kwenye kumbukizi ya mwaka wa pili tokea kufariki kwa Rais Magufuli, tunaendelea kumtakia pumziko jema la milele.
Kabla ya kufariki kwake Magufuli kulitanguliwa na kifo cha aliekuwa rais wa Tanzania mkapa , amabe kwa mtazamo wa haraka haraka walikua wanashabihiana kwenye baadhi ya falsafa zao za uongozi.
Lakini pia Mkapa ndie aliemuibua Magufuli na tunaweza kusema kwa kiasi fulani kulikuwa na strong bond baina yao.
Lakini pia inasemekana kwa nguvu ya ushawishi kwenye chama mkapa alichangia kwa kiasi kikubwa Magufuli kupata nafasi ya kugombea uraisi kwenye chama chao.
Tulipotangaziwa kifo cha mkapa na rais Magufuli tuliona bila ya shaka ni kifo kilicho muuma sana Magufuli kiasi mpaka aliweza kulia hadharani kati kati ya hotuba yake wakati wa maziko ya mkapa.
Ni ishara wazi Magufuli aliumia sana kwa kifo cha mkapa lakini kwa vile ni nature ya kila kiumbe kuwa leo kipo na kesho hakita kuwepo basi alikubali imekuwa ikawa.
Si muda sana Magufuli nae alifariki na hatimae alifanyiwa maziko kama tulivyo ona.
Kwenye msiba na maziko yake Magufuli tulisikia hotuba nyingi za viongozi wakuu na marais wa nchi nyingine na marais wastaafu wa nchi yetu.
Kwenye hotuba za marais wetu wastaafu zilikua za kawaida sana na zenye baadhi maudhui ya vichekesho mipasho .
Ndipo liliponijia wazo kama ingekuwa kinyume na yaliyotokea kwamba Magufuli angemtangulia Mkapa hotuba yake Mkapa kwenye msiba wa Magufuli Inge kuwa ya namna gani?
Wote na wengine waendelee kupumzika kwa amani.
Kabla ya kufariki kwake Magufuli kulitanguliwa na kifo cha aliekuwa rais wa Tanzania mkapa , amabe kwa mtazamo wa haraka haraka walikua wanashabihiana kwenye baadhi ya falsafa zao za uongozi.
Lakini pia Mkapa ndie aliemuibua Magufuli na tunaweza kusema kwa kiasi fulani kulikuwa na strong bond baina yao.
Lakini pia inasemekana kwa nguvu ya ushawishi kwenye chama mkapa alichangia kwa kiasi kikubwa Magufuli kupata nafasi ya kugombea uraisi kwenye chama chao.
Tulipotangaziwa kifo cha mkapa na rais Magufuli tuliona bila ya shaka ni kifo kilicho muuma sana Magufuli kiasi mpaka aliweza kulia hadharani kati kati ya hotuba yake wakati wa maziko ya mkapa.
Ni ishara wazi Magufuli aliumia sana kwa kifo cha mkapa lakini kwa vile ni nature ya kila kiumbe kuwa leo kipo na kesho hakita kuwepo basi alikubali imekuwa ikawa.
Si muda sana Magufuli nae alifariki na hatimae alifanyiwa maziko kama tulivyo ona.
Kwenye msiba na maziko yake Magufuli tulisikia hotuba nyingi za viongozi wakuu na marais wa nchi nyingine na marais wastaafu wa nchi yetu.
Kwenye hotuba za marais wetu wastaafu zilikua za kawaida sana na zenye baadhi maudhui ya vichekesho mipasho .
Ndipo liliponijia wazo kama ingekuwa kinyume na yaliyotokea kwamba Magufuli angemtangulia Mkapa hotuba yake Mkapa kwenye msiba wa Magufuli Inge kuwa ya namna gani?
Wote na wengine waendelee kupumzika kwa amani.