Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Milka Joseph Mkazi wa Chato Mkoani Geita, amejikuta katika wakati mgumu yeye na familia yake na watoto sita baada ya kutapeliwa Fedha kiasi cha Shilingi laki Moja na elfu kumi na Mbili katika kituo Cha mabasi Msamvu na mtu aliyefahamika kwa jina Moja la Mussa akidai kuwa yeye ni Wakala wa Mabasi yaendayo Mlimba Chita Wilaya ya Kilombero.
Mama huyo amesema kuwa alipofika katika kituo hicho alipokelewa na kijana huyo kisha kukatiwa tiketi nne na kutakiwa kutoa Fedha hiyo na mara baada ya kutoa akatokomea kusikojulikana na kuwalazimu kulala nje na watoto wake.
Mama huyo amesema kuwa alipofika katika kituo hicho alipokelewa na kijana huyo kisha kukatiwa tiketi nne na kutakiwa kutoa Fedha hiyo na mara baada ya kutoa akatokomea kusikojulikana na kuwalazimu kulala nje na watoto wake.