Nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa milion 12

Nauza mchele kwa bei ya jumla mkuu(Ifakara -Dar),kila wiki nasafiri mara mbili na kila safari napata faida 250K,kwa huo mtaji wa 5M,piga hesabu 250,000 X 8 = 2,000,000.
Duhh mkuu 5mil faida yake 250,000/=? Hapa risk zikitokea inakuwaje?

Labda sikaelewa vizuri , vyema ukanielewesha
 
Salaam Alleykhum,

Wadau kwa kutumia uzoefu wenu, nishaurini nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa million 12 nilionao ili kila mwisho wa mwezi at least nipate Net profit ya milioni mbili.

Nipo tayari kufanya biashara ktk mkoa wowote Tanzania au hata kama ni importation business kama mtaji unatosha nipo tayari.

Nipeni ushauri ili nami nitoboe.
Ww si mfanyabiashara unataka kufata mkumbo tu
 
Biashara mpya kwa mtaji huo mkubwa is too much risk kama hautasimamia mwenyewe mkuu

Ila kuna option ya kununua mazao ya chakula hasa Mpunga gunia zako za kutosha na kuziweka store na inapofika kipindi cha Masika unafanya kuzikoboa gunia zako na kupata mchele wako swafi tayari kwa kuingiza sokoni kwani kipindi hicho uhitaji wa mchele unakuwa mkubwa sana hapa Dar es Salaam na Zanzibar

Minimum profit calculation

Katika centre nyingi ninazo zifahamu kwa muda huu gunia moja la Mpunga lina range kwenye TSH. 50,000/=
Hivyo basi kwa Pesa uliyonayo yaani TSH. 12,000,000, utaweza kupata gunia zenye debe sita sita 240 za mpunga na kuzihifadhi.

Kipindi ambacho Masika imechanganya hasa mwezi wa kwanza au wa pili, wewe ndo unafanya kukoboa mpunga wako ili upate mchele na gunia 1 la mpunga la debe sita linatoa debe tatu za mchele na debe moja la chenga za mchele

Hivyo basi katika zile gunia 240 unazidisha mara 3 na utapata debe 720 za mchele clear na debe 240 za chenga za mchele

Ukija sokoni debe moja la mchele lina range kwenye 35,000/= kwahyo unazidisha mara debe zako 720 za mchele na utapata kiasi cha TSH. 25,200,000/=, pia debe moja la chenga za mchele ina range kwenye TSH 10,000/= ukizidisha na debe 240 utapata kiasi cha 2,400,000/=

Total itakuwa ni Tsh. 27,600,000/= na ukitoa mtaji wako wa 12,000,000/= utapata net profit ya TSH. 15,600,000/= katika kipindi cha miezi mitano cha kuhifadhi mpunga wako

Ila ukija kutoa gharama za kuhifadhi mpunga na kukoboa haizidi TSH. 5,000,000/=,hivyo bado net profit itabaki kama 10,000,000/= katika miezi mitano yako ya uvumilivu.

Centre zenye mpunga mzuri ni kama zifuatazo Kyela, Kamsamba na kilyatundu, Usangu, Kahama ila kwa Morogoro sizifahamu vizuri

Naomba kuwasilisha na ninakaribisha maswali

 
Salaam Alleykhum,

Wadau kwa kutumia uzoefu wenu, nishaurini nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa million 12 nilionao ili kila mwisho wa mwezi at least nipate Net profit ya milioni mbili.

Nipo tayari kufanya biashara ktk mkoa wowote Tanzania au hata kama ni importation business kama mtaji unatosha nipo tayari.

Nipeni ushauri ili nami nitoboe.
Sawa. Mkuu

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
 
Nauza mchele kwa bei ya jumla mkuu(Ifakara -Dar),kila wiki nasafiri mara mbili na kila safari napata faida 250K,kwa huo mtaji wa 5M,piga hesabu 250,000 X 8 = 2,000,000.

Million 5 namimi ninayo mkuu nipe connections namimi nitoke asee
 
Kweli..
Ila kumbuka biashara nyingi pia ni huduma, mfano: shule, hospitali, usafirishaji, mighahawa, ushonaji, vinyozi/ususi, nk...

Kanisa ni huduma ya kiroho ambayo ikisimama yenyewe haiwezi mpatia anachokitaka
Zaidi yeye ndio anatakiwa kutoa mahitaji
 
Biashara mpya kwa mtaji huo mkubwa is too much risk kama hautasimamia mwenyewe mkuu

Ila kuna option ya kununua mazao ya chakula hasa Mpunga gunia zako za kutosha na kuziweka store na inapofika kipindi cha Masika unafanya kuzikoboa gunia zako na kupata mchele wako swafi tayari kwa kuingiza sokoni kwani kipindi hicho uhitaji wa mchele unakuwa mkubwa sana hapa Dar es Salaam na Zanzibar

Minimum profit calculation

Katika centre nyingi ninazo zifahamu kwa muda huu gunia moja la Mpunga lina range kwenye TSH. 50,000/=
Hivyo basi kwa Pesa uliyonayo yaani TSH. 12,000,000, utaweza kupata gunia zenye debe sita sita 240 za mpunga na kuzihifadhi.

Kipindi ambacho Masika imechanganya hasa mwezi wa kwanza au wa pili, wewe ndo unafanya kukoboa mpunga wako ili upate mchele na gunia 1 la mpunga la debe sita linatoa debe tatu za mchele na debe moja la chenga za mchele

Hivyo basi katika zile gunia 240 unazidisha mara 3 na utapata debe 720 za mchele clear na debe 240 za chenga za mchele

Ukija sokoni debe moja la mchele lina range kwenye 35,000/= kwahyo unazidisha mara debe zako 720 za mchele na utapata kiasi cha TSH. 25,200,000/=, pia debe moja la chenga za mchele ina range kwenye TSH 10,000/= ukizidisha na debe 240 utapata kiasi cha 2,400,000/=

Total itakuwa ni Tsh. 27,600,000/= na ukitoa mtaji wako wa 12,000,000/= utapata net profit ya TSH. 15,600,000/= katika kipindi cha miezi mitano cha kuhifadhi mpunga wako

Ila ukija kutoa gharama za kuhifadhi mpunga na kukoboa haizidi TSH. 5,000,000/=,hivyo bado net profit itabaki kama 10,000,000/= katika miezi mitano yako ya uvumilivu.

Centre zenye mpunga mzuri ni kama zifuatazo Kyela, Kamsamba na kilyatundu, Usangu, Kahama ila kwa Morogoro sizifahamu vizuri

Naomba kuwasilisha na ninakaribisha maswali
Asante sana
 
Duhh mkuu 5mil faida yake 250,000/=? Hapa risk zikitokea inakuwaje?

Labda sikaelewa vizuri , vyema ukanielewesha
Ikitokea imetokea na isipotokea ndio hivyo kila wiki laki tano, biashara ni kujitoa mhanga tu , unaweza ukafanya biashara ya faida kubwa na ukakata hata mtaji wenyewe.
 
Mkuu habari za majukumu. Nimeona thread ukiuliza ufanye biashara ipi kwa milioni 12. Mimi ningependa kukushauri ufungue chuo. Biashara ya chuo inalipa sana, hivi sass wanafunzi wanaohitimu shule za kata ni wengi Sana, na asilimia kubwa hawapati Nafasi ktk vyuo vya serikali na pia wazazi wengi hawapendi watoto wao waishie kidato cha NNE. Hivyo hii ni fursa kubwa Sana. Binafsi ninafanya kazi Kama afisa masoko katika chuo kimojawapo jijini arusha pia Nina uzoefu katika haya masuala. Kwa hiyo pesa uliyonayo inatosha kabisa kuanzisha chuo bila tatizo lolote. Endapo utapenda kufanya biashara hii tunaweza wasiliana 0717051576
 
Ikitokea imetokea na isipotokea ndio hivyo kila wiki laki tano, biashara ni kujitoa mhanga tu , unaweza ukafanya biashara ya faida kubwa na ukakata hata mtaji wenyewe.
Mkuu angalia namna ya kuongeza hiyo 250 kwa trip kama kwa trip hiyo 1 unatumia 5mil.

Maana yake trip moja ukipata hasara ya 1mil... itakuchukuwa trip nne kurudisha faida ..
Na hapo ni kama hizo transaction zote ziende sawa bila shida
 
Back
Top Bottom