Nifanye nini kupata ukimbizi wa kisiasa katika nchi hizi?

Maxmax72

JF-Expert Member
Nov 6, 2018
530
981
Wakuu kwema?

Kwanza naomba niseme kuwa Mimi ni Mzalendo wa nchi yangu lakini pia ni kijana ambaye ni mchakarikaji wa kila kazi halali.

Ingawa ni mhitimu wa shahada ya kwanza ajabu ni kuwa huu ni mwaka wa tatu sina kazi rasmi zaidi ya kupangaiza tu kwenye vibarua kama vya ujenzi, uvuvi, kilimo na kila kazi iliyo halali, lakini bado sioni mwanga wa kuyaweza maisha na kuishi katika ndoto zangu.

Imefika pahala nikakumbuka hata Mungu alivyotuumba wanadamu hatupangia sehemu moja tu ya kuishi kwamba kwavile mimi nimezaliwa Kigoma ni lazima niishi na kufia Kigoma na sasa nimekuwa nikitafuta kila namna ya kutoka nchi hii nikajaribu na kwingine na nchi zilizo katika ndoto zangu ni Ulaya, Canada na Marekani.

Nimekuwa nikisoma na kuufatilia Nimeona siyo rahisi kuhamia nchi hizi kwa urahisi kwani wana masharti magumu sana hasa kwa watu masikini, lakini nimekaa na kuwaza siwezi kupata Viza kama mkimbizi wa kisiasa hasa kwa wakati kama huu ambapo dunia inajua Tanzania kuna kila aina ya ukandamizaji wa wanasiasa wa upinzani?

Je, nifanyeje na nijiandaeje ili niende kwenye Moja ya balozi hizi kama mkimbizi wa kisiasa?

Naombeni msaada wa mawazo maana naamini hakuna kisichowezekana na isitoshe mimi sitokuwa wa kwanza kufanya hivi.

Karibumi kwenye mjadala na mwenye kejeli ongeeni sana lakini kiukweli wasomi nchi hii hatuna maana tena kwani maisha mazuri tunayasikia tu kwa mwenye mamlaka.
 
Usikimbie mkuu, watu wanaoishi maisha ya aina yako tuko wengi.

Muda unaotumia kutafuta uhamie wapi bila kuwa na uhakika wa kupata au kukosa heri uendelee kupambana ndani ya nchi yetu

Hawa mabwana kuna wakati ukifikiria sana unaona hata huu mfumo wa elimu ya kukariri bila vitendo waliotuletea na kutushurtisha kuufata ulikua mpango wa kutuchelewesha kujitafuta sisi na rasilimali zetu.

Na matokeo yake tunayaona maisha magumu baada ya kumalizia miaka karibu 20 shuleni bila kuwa na chochote mfukoni, na kibaya zaidi bado tunawaona wao ndio kimbilio letu na suluhu katika ugumu wa maisha bila kuona vile wenyewe wanavyokimbilia rasilimali zetu zenye thamani zaidi ya hayo makaratasi yao kwa sababu tunashindwa kuzitumia

Wacha twende na John Pombe Magufuli yeye anatuwazia mema sana kuliko tunavyodhani

Cc magu2016 kuna ndugu anataka kuhama nchi huku...
 
Upo kigoma?
Kama ndio
Njia kwanza.
1.Nenda pale maweni Zamani paliitwa TcRC/wanapojaza form za kuapishwa uraia ILI upate kadi ya Nida,kwa juu mle ndani kuna ofisi ya unhcr wanasajili wakimbizi wanaoingia nchini unapewa kitambulisho cha ukimbizi unapelekwa kambini kule kambini mnasajiliwa kwenda ulaya na marekani ila inachukua muda ukihonga hela kidogo unaweka katika list ya watakao ondoka haraka...ila kujieleza hadi ueleweke ni kazi kweli kweli ila kwa wakongo na warundi ni rahisi kuchukuliwa kambini,ila maisha ya kambini ni magumu sana kwa sasa tofauti na zamani na uraia Wa TZ unaukana.

Njia ya 2
Unaenda Kongo kwa njia za wizi unaenda Miji mikubwa kama Lubumbashi au Kinshasa,hiyo miji IPO mbali kufika kutokea kigoma unaweza tumia mwezi...maana ndani ya Kongo barabara za lami hakuna zilizounganisha nchi kama Tanzania,sasa ukifika huko unaungana na wakongo wanaoenda marekani na kanada kwa kupitia brazil-mexico-usA-canada kwa kusafirishwa wasafirisha binadamu
 
Kachukue kadi ya upinzani, then nenda balozini kawaambie unataka kuandanama kwa mujibu wa katiba lakini unahofia kutiwa nguvuni endapo utatekeleza azma hiyo... Hivyo umeamua kukimbia ili ukaandamanie nje ya nchi kwa uhuru zaidi...

Waambie unahofu baada ya viongozi wa upinzani kushikwa, hivyo unadhani wafuasi ndio mnafuata so umeamua kujihami mapema.

Natania Mkuu, subiri wazoefu..
Hii yako ina-sound good ulivyoileta kimasikhara lakini ikiboreshwa kimtindo inaweza kutiki,na jinsi beberu alivyo mtu mzuri na mwenye huruma wanaweza wakamkubalia
 
Wakuu kwema?

Kwanza naomba niseme kuwa Mimi ni Mzalendo wa nchi yangu lakn pia ni kijana ambaye ni mchakarikaji wa kila kazi halali.

Ingawa ni mhitimu wa shahada ya kwanza ajabu ni kuwa huu ni mwaka wa tatu sina kazi rasmi zaidi ya kupangaiza tu kwenye vibarua kama vya ujenzi, uvuvi, kilimo na kila kazi iliyo halali, lakn bado sioni mwanga wa kuyaweza maisha na kuishi katika ndoto zangu.

Imefika pahala nikakumbuka hata Mungu alivyotuumba wanadamu hatupangia sehemu moja tu ya kuishi kwamba kwavile mimi nimezaliwa Kigoma ni lazima niishi na kufia Kigoma na sasa nimekuwa nikitafuta kila namna ya kutoka nchi hii nikajaribu na kwingine na nchi zilizo katika ndoto zangu ni Ulaya, Canada na Marekani.

Nimekuwa nikisoma na kuufatilia Nimeona siyo rahisi kuhamia nchi hizi kwa urahisi kwani wana masharti magumu sana hasa kwa watu masikini, lakn nimekaa na kuwaza siwezi kupata viza kama mkimbizi wa kisiasa hasa kwa wakti kama huu ambapo dunia inajua Tanzania kuna kila aina ya ukadamizaji wa wanasiasa wa upinzani?

Je, nifanyeje na nijiandaeje ili niende kwenye Moja ya balozi hizi kama mkimbizi wa kisiasa?

Naombeni msaada wa mawazo maana naamini hakuna kisicho wezekana na isitoshe mimi sitokuwa wa kwaza kufanya hivi.

Karibumi kwenye mjadala na mwenye kejeli ongeeni sana lakn kiukweli wasomi nchi hii hatuna maana tena kwani maisha mazuri tunayasikia tu kwa mwenye mamlaka.
Canada wana utaratibu wa greencard, sijui umesomea nini, ila kama ni moja ya wanachohitaji, wanaweza kukuchukua. Pitia tovuti zao zinazoongelea mambo ya uhamiaji/ vibali vya kazi uone unaanzia wapi. Kila la kheri!
 
Usikimbie mkuu, watu wanaoishi maisha ya aina yako tuko wengi.

Muda unaotumia kutafuta uhamie wapi bila kuwa na uhakika wa kupata au kukosa heri uendelee kupambana ndani ya nchi yetu

Hawa mabwana kuna wakati ukifikiria sana unaona hata huu mfumo wa elimu ya kukariri bila vitendo waliotuletea na kutushurtisha kuufata ulikua mpango wa kutuchelewesha kujitafuta sisi na rasilimali zetu
Na matokeo yake tunayaona maisha magumu baada ya kumalizia miaka karibu 20 shuleni bila kuwa na chochote mfukoni, na kibaya zaidi bado tunawaona wao ndio kimbilio letu na suluhu katika ugumu wa maisha bila kuona vile wenyewe wanavyokimbilia rasilimali zetu zenye thamani zaidi ya hayo makaratasi yao kwa sababu tunashindwa kuzitumia

Wacha twende na John Pombe Magufuli yeye anatuwazia mema sana kuliko tunavyodhani
Mtaji wa wanasiasa wetu ni Umasikini na Ujinga wa WaTanzania!
 
Tafuta hela mtaji wa kuhamia huko Canada, Huwezi kuhamia canada na Marekani ukaenda kuwa omba omba, Tafuta mtaji ukienda kule ujue unaenda kudil na kazi gani, Mimi binafsi napambana hapa hapa nyumbani ikitiki sikawii kudandia Air-Bus 777-Boeing mpaka Canada, Istoshe wizara inayohusika na idadi ya watu nchini Canada imetangaza nafasi za uhamiaji kwa raia wa kigeni ambao wangependa kufanya kazi nchini humo 2020+
 
Tafuta hela mtaji wa kuhamia huko Canada, Huwezi kuhamia canada na Marekani ukaenda kuwa omba omba, Tafuta mtaji ukienda kule ujue unaenda kudil na kazi gani, Mimi binafsi napambana hapa hapa nyumbani ikitiki sikawii kudandia Air-Bus 777-Boeing mpaka Canada, Istoshe wizara inayohusika na idadi ya watu nchini Canada imetangaza nafasi za uhamiaji kwa raia wa kigeni ambao wangependa kufanya kazi nchini humo 2020+
hizo nafasi uwe na hela nyingi sio mbugila mbugila wao wanataka mafisadi hivi kama wakina manji ndio target yao
 
njia rahisi inatumika na waafrika wengi kama wasudan,wasomali wakongo,unajichanga unapata visa na tiketi yako ya ndege ya nchi iliyokaribu na unapotaka kuingia alafu kuna wajanja pale wa kuwapitisha ni uwe tu na dollar zako
 
Njia rahisi ni tafuta bwana, nenda nae ubalozi wa hizo nchi waambie wewe ni shoga na unataka kufunga ndoa na huyo bwana wako ila serikali inakutafuta ikufunge.
Hapo unapata fasta ila ni lazima uwe shoga kweli. Hivyo uanze kwanza kuwa shoga kabla ya kwenda
 
Njia rahisi ni tafuta bwana, nenda nae ubalozi wa hizo nchi waambie wewe ni shoga na unataka kufunga ndoa na huyo bwana wako ila serikali inakutafuta ikufunge.
Hapo unapata fasta ila ni lazima uwe shoga kweli. Hivyo uanze kwanza kuwa shoga kabla ya kwenda
Per Diem kwa haya maushauri ya men Leo kweli mmevurugwa na man mwenzenu
 
Mkuu mfumo wa elimu yetu ni mbovu haswa.
Sijui kama utaweza pata kazi ya maana huko unapopataka.

Unaweza kuwa homeless japo sikutishi.
 
Unatka kutu kimbia ili na ss tubak na nan hpa bongo
Baki mkuu vyuma vitupige wote
 
Upo kigoma?
Kama ndio
Njia kwanza.
1.Nenda pale maweni Zamani paliitwa TcRC/wanapojaza form za kuapishwa uraia ILI upate kadi ya Nida,kwa juu mle ndani kuna ofisi ya unhcr wanasajili wakimbizi wanaoingia nchini unapewa kitambulisho cha ukimbizi unapelekwa kambini kule kambini mnasajiliwa kwenda ulaya na marekani ila inachukua muda ukihonga hela kidogo unaweka katika list ya watakao ondoka haraka...ila kujieleza hadi ueleweke ni kazi kweli kweli ila kwa wakongo na warundi ni rahisi kuchukuliwa kambini,ila maisha ya kambini ni magumu sana kwa sasa tofauti na zamani na uraia Wa TZ unaukana.

Njia ya 2
Unaenda Kongo kwa njia za wizi unaenda Miji mikubwa kama Lubumbashi au Kinshasa,hiyo miji IPO mbali kufika kutokea kigoma unaweza tumia mwezi...maana ndani ya Kongo barabara za lami hakuna zilizounganisha nchi kama Tanzania,sasa ukifika huko unaungana na wakongo wanaoenda marekani na kanada kwa kupitia brazil-mexico-usA-canada kwa kusafirishwa wasafirisha binadamu
Hiyo njia ya kwanza uliompa sio rahisi Bora atafute njia nyingine , Kila kitu UNHCR imesha weka kwenye data base kwa mkimbizi mpya kupewa hifadhi ya kwenda nchi ya Tatu (resentlement) ni kazi kweli kweli anaweza kupoteza ma millioni za pesa na aka kosa kupata resentlement
 
Back
Top Bottom