Nifanye nini jamani

Dongola

Senior Member
Joined
Oct 19, 2014
Posts
122
Reaction score
15
Ni mwaka na miezi 2 imepita sasa tangia niachane na ex huyu kiukweli tulipendana sana tuliachana coz wazazi wake walimchaguli mke wa kumuoa coz aliwaheshimu sana wazazi wake hakutaka kupingana nao alifanya vile walivyotaka na huo ndo ulikuwa mwisho wetu kiukweli alitoka kwenye familia yenye uwezo na alikuwa mfanyabiashara tofauti na mimi familia yangu ya kawaida tu.

Baada ya yeye kuoa nilikata kabisa mawasiliano naye lakini jana asubuhi nilipokea sms kutoka kwake aliandika hivi (wewe ni mwanake wa pekee kwangu kamwe sitokuja kukusahau pokea pesa hizo nimekuingiazia kwenye account yako kiasi cha sh.milioni 4 naomba nikupatia zawadi hiyo kama kumbukumbu yako kwangu tarehe 13 mimi na mke wangu tunahamia Italy kwa heri na kubaki salama).

Nimebaki njia panda nifanye nini naogopa kuzitumia hizi pesa nimemshilikisha mama yangu kanishauri nizirudishe, nahitaji mawazo yenu nifanye nini nimrudishie pesa zake coz now kiuchumi najiweza na sihitaji kabisa mawasiliano naye na naogopa pesa hizi isije ikawa chanzo cha mimi na yeye kuwasiliana.
 
Si ulikata mawasiliano?kapataje no yako?chukua pesa kula kona lols
 
Use your head. Nikisema nimekata mawasiliano it means upande wangu. Seemingly the dude still kept her number

Mnh ukate mawasiliano afu ukeep number ile ile?strange!
 

Sasa keshakuambia kumbukumbu yake kwako unataka nini?
Kuwa mjasiriamali izungushe hiyo hela....
Kujipa mawazo ya bure...
 
Jitahidi wakati ujao uandike ki-utu uzima maana siku nyingine tunaweza kukupuuza kwa uandishi uliotumia uhitajipo msaada. Kama hukujibu ujumbe aliokutumia kwa simu fanya upige kimya ili mdau aendelee kuwa na viulizo kama umeafiki au la. Na mpunga ufanyie mambo zako kuliko kurudisha kwa mdau ambaye ametoa kiroho safi na pia haya maisha yanaenda mbele, leo yeye kakusaidia yawezekana kesho ikawa zamu yako kutoa msaada si tu wa kifedha bali hata mawazo chanya.
 
Unawaza mbali kumbe mtu kakupa as a good will kama huna mume/mchumba tumia hiyo pesa lakini kama una mume angalia kisiwe kitanzi cha ndoa yako akijua lakini sidhani km huyo bwana ana nia mbaya
 
Unawaza mbali kumbe mtu kakupa as a good will kama huna mume/mchumba tumia hiyo pesa lakini kama una mume angalia kisiwe kitanzi cha ndoa yako akijua lakini sidhani km huyo bwana ana nia mbaya

Sina mume wala mchumba asante kwa ushauli
 

asante kwa ushauli
 
How are the two related?

Kuna watu hawajui maana ya mawasiliano... Jestina refer communication skills ya form 1.
kama unakumbuka sender,receiver,barriers,feedback...
Naweza kukata mawasiliano na no nsibadilishe na wewe usibadilishe...
Simple sijibu wala kupokea ...
Hiyo ndo kukata mawasiliano...
 
Last edited by a moderator:
Chukua hela wewe........khaaaaa........au nichukulie mimi nina kazi nazo........
 
Reactions: BAK
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…