Niende au nimpotezee?

Niende au nimpotezee?

Principle girl

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2014
Posts
1,675
Reaction score
1,754
Wana jf naombeni mnishauri
Hiko hivi mimi kuna kijana nilikua nae kwenye mahusiano ila hatukudumu sana tukaachana na kukata mawasiliano kabisa kwa muda wa mwaka mmoja,sasa cha kushangaza leo niliporudi kwangu kutoka mihangaiko nikaambiwa na dada jirani hapa kwamba kuna kijana kaja kukutafuta kumuuliza nani huyo kijana akanitajia jina afu akanipa na namba za simu akasema amesema nimtafute na ni muhimu kweli,basi nikamtext akanipigia akauliza nipo wapi nikamwambia home akasema anakuja sababu ana shida muhimu sana nikamjibu poa,baada ya nusu saa akawa keshafika baada ya salamu akanza kuomba msamaha kwa yaliyopita na akadai kilichomleta yeye anataka kusafiri na huko anakoenda atakaa kwa muda wa miez mitatu hivo anaomba niende nikakae kwake ili kumuangalizia nyumba yake mpaka ataporudi maana hapo kwake kuna mlinzi tu na house boy,pia akanambia akirudi kuna pesa atanipatia kama zawadi..me sijamjibu nimemwambia kwanza nijifikirie sasa wapendwa nishaurini niende au nimpotezee tu?
 
Kwa hiyo wewe utakuwa mlinzi wa ndani?
Houseboy > mlinzi wa garden/usafi
Mlinzi orinaginali > analinda geti
Wewe utalinda nini?
 
Nenda lakn mlinz akiomba shoo usimkazie coz anaweza kuchukua hatua kali kwny mwili wako
 
Kwa hiyo wewe utakuwa mlinzi wa ndani sio kuludisha mahusiano yenu kama Huna kibarua nenda kafanye kazi upate pesa
 
Kama kuna mlinzi na huyo mfanyakazi, wewe unaenda kufanya nini?
 
Huyo ni mjanja anataka kukugeuza asusa, shauri yako
 
anza kuomba msamaha kwa yaliyopita na akadai kilichomleta yeye anataka kusafiri na huko anakoenda atakaa kwa muda wa miez mitatu hivo anaomba niende nikakae kwake ili kumuangalizia nyumba yake mpaka ataporudi maana hapo kwake kuna mlinzi tu na house boy,pia akanambia akirudi kuna pesa atanipatia kama zawadi..me sijamjibu nimemwambia kwanza nijifikirie sasa wapendwa nishaurini niende au nimpotezee tu?
Unazuga tu! ningeshangaa kwenye pesa ukatae
 
Nenda ukagegedwe na kijiji kizima kwa mpigo dadadeki....!!!!!
 
jitulize we mtoto wa kike. mtu mmepoteleana mwqka mzima na hujui life style yake kwa sasa na unataka kukurupuka tu.
mpe dharura ya uongo lakini usiende huwez jua ana nia gan
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom