Nidhamu ya majeshi yetu na uoga wa watawala

Nidhamu ya majeshi yetu na uoga wa watawala

Jack Daniel

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2021
Posts
4,613
Reaction score
18,840
Kelele zimekuwa nyingi mtandaoni kuhusu majeshi yetu kuonesha yanakiuka katiba na kuivunja Kwa kuzuia mikutano,kuteka na hata kutesa wananchi ambao majeshi yetu yana jukumu la kuwalinda.

Lakini niseme tu kuwa tunayaonea Sana majeshi yetu Kwa kila yanachokifanya kwasababu kila kinachofanyika ni kutii mamlaka Kwa maboss zao.

Utekaji,utesaji na dhulmat zote zinatokana na shinikizo au maamuzi ya maboss,sasa hebu fikirieni ni Nani anaweza kumgomea au kupingana na boss wake?

Tunaangalia tulipoangukia badala ya tulipojikwaa, huko juu watu Wana hofu na wasiwasi na kila linalofanyika si Kwa bahati mbaya.

Mtalaumu wote IGP na wadogo zake ,lakini ukweli ni kwamba kiapo walichoapa ,si kulitumikia taifa bali kuwaheshimu viongozi wao ndicho kinachowasumbua.

Mungu ibariki Tanzania
Mungu wabariki viongozi wetu.
 
Mwisho wa dhuluma haupo mbali, wataaibika tu very soon
 
Back
Top Bottom