Niachane vipi na huu mchepuko?

hahaha....naona ulikuwa unabadilisha mboga mkuu sasa kitu kimetiki kote kote!
Jiandae kulea watoto wote mkuu, assume mkeo ndio amekuzalia mapacha😀😀
Mkuu kwa mchepuko sihusiki kwa asilimia mia ila kwa wife nina imani kubwa kuwa nahusika.
 
Mkuu sisi sote ni wanaume tunapaswa kusaidiana katika kipindi kigumu kama hiki naomba usinivunje moyo nipe msaada wa ushauri nami nitakushukuru.
Ndo nshakuambia hivyo...
 
Mkuu kwa mchepuko sihusiki kwa asilimia mia ila kwa wife nina imani kubwa kuwa nahusika.
Kwanini kwa mchepuko hutaki kuamini kwamba hiyo mimba ni yako ili hali ulikuwa unapiga??Nenda ukacheki DNA kabla huo mchepuko haujakuharibia mkuu
 
Mkuu hata mimi nadhani hilo ndo jambo la maana manake hakuna namna na ukizingatia mwenzangu anajua namtaka kweli wakati nilikuwa nampozea maumivu.

This is even worse, kwa nini wamdanganya mtoto wa watu? Hivi huwezi mwambie mwanamke ukweli akakukubali tu? Usije kuomba ushauri hapa wakati wewe ndo jipu, achana na mtoto wa watu kwa kumwambia ukweli otherwise you will have issues baadae sitakugharimu, the truth will set you free.
 
Kumuacha sio tatizo kwake, ila amwachaje ndio tatizo maana anahofia sijuwi kurogwa.

Mbali na kuhofia kurogwa naomba uzingatie UTU kwanza. Usikurupuke kumuacha ghafra hasa ukizingatia mwenzio yupo katika kipindi kigumu.

Muache kama mpenzi wako ila si kama rafiki yako wa karibu.Namaanisha Endelea kuwa karibu nae kihuduma za msingi hasa katika mahitaji yake uliyokuwa unamsaidia awali. Ila kuwa nae mbali ktk mambo ya kimapenzi.

Pengine wewe ndio ulikuwa faraja yake, Hivyo kumuacha ghafra inaweza kumpelekea akaumia sana, Mwisho Siraha(UCHAWI) uliyoihofia ikawa njia yake pekee kuripiza kisasi.

ALIKUSTIRI WAKATI WA DHIKI ZAKO NAWE MSTIRI KTK DHIKI YAKE.
 
Nimekuelewa na nitazingatia unaloniambia ila kiukweli najilaumu kwa niliyoyatenda.
 
Kama umeshatambua na una hakika mtoto so wako unapata shida gani mweleze ukweli kwamba baba Wa mtoto aendelee kuhudumia mke wangu asijetambua mahusiano yangu Mimi na wewe Usijevunja ndoa yako 'POLE SANA'
 
Wanaume mmezidi kwa tamaa
acha ulogwe Tu sasa
 
USIKIMBIE MAJUKUMU watafutie Card ya BIMA tunza wote mungu atakulipa usimkimbie mchepuko fanya ubinadamu kidogo... wewe mwache azae kwanza ndiyo umueleze baada ya kuzaa kaa miezi kama 3 hivi basi
 
WEWE LEA WOTE HATA HUYO UMPENDAE UNAUHAKIKA GANI KAMA SIO KIRUNJE ? MTOTO HASARA WEWE BAS TU
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…