Naomba niwaulize wale ambao wanasema muda hautoshi wa kufanya reforms, je, wapo tayari kwa reforms na katiba mpya kwa ujumla hata kwa baadae baada ya uchaguzi wa mwaka huu? Hii ni kwa sababu CCM wanasema kwa sasa muda uliobaki hautoshi na hawataki kuongezewa muda wa kukaa madarakani ili wafanye reforms.
Jamani tusicheze na muda kabisa. Unajua siku hazigandi. Kinachotakiwa hapa ni nia ya dhati na siyo danadana!
Ikitokea Lisu kakubali kwenda kwenye uchaguzi bila reforms, je, CCM wataanzisha mchakato wa reforms na katiba mpya mapema iwezekanavyo mara baada ya kumaliza uchaguzi wa mwaka huu? Au itaibuliwa sababu nyingine kwamba Watanzania hitaji lao siyo katiba bali ugali na football?
Nimeuliza hivyo kwa sababu tusiwe tunasema muda hautoshi kumbe hata ile nia tu haipo bali kigezo cha muda kutotosha ni kama silaha ya kuchelewesha mambo!
Hivi leo tukasema tupige kura ya maoni kama Watanzania wanataka katiba mpya au la, unahisi majibu yatakuwaje?
Jamani tusicheze na muda kabisa. Unajua siku hazigandi. Kinachotakiwa hapa ni nia ya dhati na siyo danadana!
Ikitokea Lisu kakubali kwenda kwenye uchaguzi bila reforms, je, CCM wataanzisha mchakato wa reforms na katiba mpya mapema iwezekanavyo mara baada ya kumaliza uchaguzi wa mwaka huu? Au itaibuliwa sababu nyingine kwamba Watanzania hitaji lao siyo katiba bali ugali na football?
Nimeuliza hivyo kwa sababu tusiwe tunasema muda hautoshi kumbe hata ile nia tu haipo bali kigezo cha muda kutotosha ni kama silaha ya kuchelewesha mambo!
Hivi leo tukasema tupige kura ya maoni kama Watanzania wanataka katiba mpya au la, unahisi majibu yatakuwaje?