kambiyamkaa
Senior Member
- Aug 9, 2020
- 122
- 110
Niwaombe Sana Wasome kutoka Vyuo mbalimbali hapa Nchini , Wanaharakati , Na Wadau wote wa Maendeleo Na wanaoitakia Maendeleo zaidi Nchi yetu kwamba , huu Ni wakati muafaka wa kumfahamu kila Mgombea hususani hii ya Rais !
Ninaonavyo Mimi , Ni muhimu Sana , Sana ukaandaliwa Mdahalo Na Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali ( NGO's ) mbalimbali kwa Wagombea wa nafasi hii ya Urais angalau Mara mbili Mara tu baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kukamilisha kazi ya Uteuzi tarehe 25 August mwaka huu !
Watanzania tuna haki ya kuwajua Wagombea kwa undani ili tufanye Maamuzi sahihi ya kumpigia Kura Mgombea sahihi , Na hatimaye tumpate Rais ambaye kweli atakuwa Ni Chaguo la Watanzania !
Hatutaki kuchezewa safari hii ! Kwa mara ya kwanza na ya mwisho kama nakumbuka vizuri , mdahalo wa Wagombea Urais ulifanyika mwaka 1995 wakati wa Uchaguzi wa kwanza wa Vyama vingi . Tokea wakati huo , Chaguzi zilizofuata , Wagombea wamekuwa wakiikwepa Midahalo!Na hata wengine kuibeza miongoni mwa Presidential Candidates !
Mwaka 2010 , Kituo cha television cha TBC kinachomilikiwa na Shirika la Utangazaji la Taifa ( Shirika la Umma ) Shirika letu sote Watanzania, Shirika lilianzisha mdahalo kwa Wagombea Ubunge . Huwezi kuamini , ghafla midahalo hiyo ilifutwa ! You can not believe !
Chama za Mapinduzi kiliwazuia haraka Sana Na kutoa agizo zito kwamba wanachama wake ( wagombea ubunge ) , Ni marufuku kushiriki midahalo hiyo ! Uamuzi ule wa TBC kusitisha midahalo ile kwa kweli binafsi niliumia Sana , Sana !
Ni kuwanyima fursa wapiga Kura kuwajua wagombea Na kuwapima Na pia kuwanyima fursa Wagombea kuulezea Umma Sera zao pamoja na Mikakati huku wakisiliza changamoto kutoka kwa wapinzani Wao . Ili Uchaguzi uweze kuwa huru Na haki , Ni lazima wapigakura wawaelewe vizuri Wagombea Wao , Sera na ilani za vyama vyao ili tunapofanya uamuzi tarehe 28 October wa kumchagua mgombea mmoja , tufanye kwa usahihi badala ya kufanya maamuzi ya kishabiki !
Ni hatari Sana kufanya maamuzi ya kishabiki ! Narudia tena kwa Msisitizo Sana , kuyaomba mashirika yasiyo ya Kiserikali , na hata TBC Shirika la Umma , nanyi pia bado mnaweza kuandaa Midahalo hii !
Nikuombe Mkurugenzi wa TBC , asiogope . Midahalo inajenga na bila shaka tutawapata Wabunge Wazuri na Rais ambaye kweli atakuwa Ni chaguo la Watanzania .
Vyama pia vya Siasa , niviombe Sana vitoe Ushirikiano utakaohitajika na Mashirika hayo ili kufanikisha azma hii muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu .
Naamini na mtakuwa pamoja nami kwamba , kwa yeyote Mgombea atakayekwepa Midahalo hiyo ,
Ninaonavyo Mimi , Ni muhimu Sana , Sana ukaandaliwa Mdahalo Na Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali ( NGO's ) mbalimbali kwa Wagombea wa nafasi hii ya Urais angalau Mara mbili Mara tu baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kukamilisha kazi ya Uteuzi tarehe 25 August mwaka huu !
Watanzania tuna haki ya kuwajua Wagombea kwa undani ili tufanye Maamuzi sahihi ya kumpigia Kura Mgombea sahihi , Na hatimaye tumpate Rais ambaye kweli atakuwa Ni Chaguo la Watanzania !
Hatutaki kuchezewa safari hii ! Kwa mara ya kwanza na ya mwisho kama nakumbuka vizuri , mdahalo wa Wagombea Urais ulifanyika mwaka 1995 wakati wa Uchaguzi wa kwanza wa Vyama vingi . Tokea wakati huo , Chaguzi zilizofuata , Wagombea wamekuwa wakiikwepa Midahalo!Na hata wengine kuibeza miongoni mwa Presidential Candidates !
Mwaka 2010 , Kituo cha television cha TBC kinachomilikiwa na Shirika la Utangazaji la Taifa ( Shirika la Umma ) Shirika letu sote Watanzania, Shirika lilianzisha mdahalo kwa Wagombea Ubunge . Huwezi kuamini , ghafla midahalo hiyo ilifutwa ! You can not believe !
Chama za Mapinduzi kiliwazuia haraka Sana Na kutoa agizo zito kwamba wanachama wake ( wagombea ubunge ) , Ni marufuku kushiriki midahalo hiyo ! Uamuzi ule wa TBC kusitisha midahalo ile kwa kweli binafsi niliumia Sana , Sana !
Ni kuwanyima fursa wapiga Kura kuwajua wagombea Na kuwapima Na pia kuwanyima fursa Wagombea kuulezea Umma Sera zao pamoja na Mikakati huku wakisiliza changamoto kutoka kwa wapinzani Wao . Ili Uchaguzi uweze kuwa huru Na haki , Ni lazima wapigakura wawaelewe vizuri Wagombea Wao , Sera na ilani za vyama vyao ili tunapofanya uamuzi tarehe 28 October wa kumchagua mgombea mmoja , tufanye kwa usahihi badala ya kufanya maamuzi ya kishabiki !
Ni hatari Sana kufanya maamuzi ya kishabiki ! Narudia tena kwa Msisitizo Sana , kuyaomba mashirika yasiyo ya Kiserikali , na hata TBC Shirika la Umma , nanyi pia bado mnaweza kuandaa Midahalo hii !
Nikuombe Mkurugenzi wa TBC , asiogope . Midahalo inajenga na bila shaka tutawapata Wabunge Wazuri na Rais ambaye kweli atakuwa Ni chaguo la Watanzania .
Vyama pia vya Siasa , niviombe Sana vitoe Ushirikiano utakaohitajika na Mashirika hayo ili kufanikisha azma hii muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu .
Naamini na mtakuwa pamoja nami kwamba , kwa yeyote Mgombea atakayekwepa Midahalo hiyo ,