Ni wakati gani mtu anaokoka?

Ni wakati gani mtu anaokoka?

Yes jamii nyingi pamoja na wewe hawamjui Yesu Kristo na upendo wake ndio maana tunashare na kuhubiri injili kwa nguvu zote ili mpate kumfahamu kwamba sio wa kuletwa na wazungu bali ni Mungu aliyekuwako kabla ya kuumbwa ulimwengu na vyote vilifanyika kupitia Yeye.

Ni Mungu aliyejifunua kwa wanadamu kupitia utu wa Yesu Kristo. Sio imaginations au mastori ya kutungwa bali anaelezewa na kuhushudiwa kupitia maandiko matakatifu.

Yoh 1 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
² Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
³ Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
⁴ Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.
⁵ Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.
⁶ Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
⁷ Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye.
⁸ Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru.
⁹ Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu.
¹⁰ Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua.
¹¹ Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.
¹² Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

Unaamini maandiko matakatifu? Unaamini ujumbe wake? Ikiwa waamini yote waliyosema manabii juu yake, huwezi kuwa na ufahamu tena imani ya kikristo ni imani ya kuletwa na wakoloni.



Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
Usku mwema mkuu
 
Kutoka kwenye tafsiri ipi hiyo ya Biblia? Leta hapa tuone? Usichukue maneno ya mtaani ukayaleta kwenye biblia.

Biblia tafsiri ya kiswahili haina neno kuongoka. Hata tafsiri za English wala lugha za asili.

Kama ilivyo maneno katika uwanja wa sheria, kidaktari, jeshi, engineering nk maneno katika nyanja hizo hayana maana za jumla. Ndivyo hivyo hivyo maneno ya kwenye biblia yanapata maana zake ndani ya muktadha wa biblia. Ukiyapa maana toka kwenye kamusi za kawaida au 'gugo'[emoji38] lazima uende chaka.

Hivyo neno "kuokoka" litapata maana yake kulingana na biblia na sio vinginevyo.

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
kwani Biblia Takatifu ni Neno Pekee la Mungu!
 
Haya ni maoni yako wewe kama wewe sio kama Neno la Mungu linavyosema. Ukiacha kuliamini neno la Mungu linavyosema utautafsiri wokovu kwa maoni yako, utajiokoa kwa maoni yako, utapata mwokozi wa maoni yako. Hata mbingu na pepo itakuwa kulingana na maoni yako.

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
Sasa,wewe sijui unasema nini. Mtu anaambiwa na daktari,"Acha ulevi we. Huu ulevi utakuua."
Huyu mtu anamsikia daktari,anamuekewa,lakini anashindwa kuacha. Ndio tunasema hajaokoka.Akiokoka,ataacha,ataachaulevi, ulafi,ataacha fitina,ataacha ngono questionable. Kuokoka kunaanza na mwili. Baadaye akipata mafanikio makubwa kuondoa dhambi zake za roho,ndio anaitwa mtakatifu.
Halafu kumbuka hawa walokoke mara nyingi wana- relapse( wanarudia hali zao za zamani).
 
UMEKOMBOLEWA? INA MAANA GANI KUKOMBOLEWA?[emoji848]

Na Pastor Felician Makarios

Wakati mwingi tunaimba tumekombolewa na Yesu halafu hatukai katika kina cha maana ya maneno hayo. Tunaimba au kutamka tu kama kasuku.

Imekua kawaida katika jamii ya Kikristo, kusema tu maneno ya kidini hata kama hatuamini tunachosema au hatuelewi tunachosema.

Neno "ukombozi" linarejea gharama iliyolipwa, hiyo gharama ni thamani ya mtu.

1Timotheo 2:5 Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; 6 ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.

Neno "ukombozi" limetafsiriwa kutoka katika neno la kigiriki 'lutron' linalomaanisha gharama iliyolipwa.

Kwa hiyo Paulo anasema Yesu alijitoa kua gharama inayolipwa

Mathayo 26:28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

Damu ya Yesu (maisha ya Yesu) ndiyo gharama iliyolipwa kwaajili ya dhambi.

Tazama hapa,

Luka 22:20 Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.]
Hapa tena,

Warumi 3:23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 25 ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilzotangulia kufanywa.

Damu ya Yesu ndiyo gharama iliyolipwa, ni bure, na ni katika Kristo. Hakuna gharama nyingine inayohitajika kwa ajili ya ukombozi.

Angalia hapa, nani aliyenunua;

Matendo 20:28 Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.

Hapa tena;

Wagalatia 3:13 Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;

Kwa kifo chake, alitukomboa kutoka katika dhambi.

Ni kazi ya Kristo, siyo kazi yetu. Ni yeye mwenye kufanya ukombozi.

Angalia hapa;

Tito 2:14 ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.

Tumekombolewa na maasi yote, tumesafishwa kuwa miliki yake na ndipo tuna juhudi katika kutenda mema.

Si kwa matendo ya haki tuliyotenda;

Tito 3:4 Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa,alituokoa; 5 si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu; 6 ambaye alitumwagia kwa wingi, kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu; 7 ili tukihesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele, kama lilivyo tumaini letu.

Gharama ililipwa kwa niaba yetu.

1Wakorintho 6:19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; 20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.

Hapa tena;

1Wakorintho 7:23 Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu.

Hivyo, tulinunuliwa kwa gharama iliyolipwa, kwahiyo ukombozi wetu ni katika Kristo.
Hivyo tunao ukombozi, siyo tutakua na ukombozi; ni sasa, tunamiliki ukombozi.

Waefeso 1:7 Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.
Neema maana yake ni kwamba ilitolewa bure, na msamaha wa dhambi unapatikana kwa sababu ya wingi wa neema yake.

Wakolosai 1:12 mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru. 13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; 14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;

Katika ukombozi, tuna masamaha ya dhambi. Mungu hakuomba badiliko la moyo kutoka kwetu kabla hajatusamehe; ilitolewa kwetu kwa msingi wa kile ambacho Kristo amefanya.

Hapahitaji kujitutumua, ni kazi yake. Ni neema yake kwetu.

Waebrania 9:11 Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu, 12 wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele.

Alipata ukombozi wa milele kwaajili yetu kwa damu yake! Huku ndiko kuachiliwa kabisa kutoka kwenye dhambi.

Mwamini hayupo tena katika dhambi, ameachiliwa kabisa, amekombolewa milele.
Kumbuka kwamba Wokovu una msingi katika kweli tatu; kifo cha Yesu, kuzikwa kwake, ufufuo wa Yesu katika mwili na kwasababu hiyo kupaa kwake.

1Wakorintho 15:17 Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu.

Maana kuwepo kwa dhambi kunategemea kutofufuka kwa Yesu. Ikiwa alifufuka basi imani yetu siyo bure na tayari tuna msamaha wa dhambi, hatumo dhambini tena.

Ufufuo wa Yesu ni ushahidi kwamba gharama imelipwa kwaajili ya dhambi. Ufufuo wa Yesu unathibitisha kazi ya ukombozi. Inaweka muhuri wa mwisho kabisa na inatoa uhakika wa wokovu wa milele kwa mwamini.

Angalia hapa;

Waebrania 5:9 naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;

Wanaomtii katika matumizi ya mwandishi wa Waebrania inarejea “wanaomwamini”. Kuamini ndiko kutii.

Wokovu huo, unaitwa wa milele. na Kristo ndiye anayeutunza. UKOMBOZI WA MILELE
Siyo wewe unayetunza, hapana. Ni mkombozi anayetunza ukombozi wa aliyekombolewa.
Angalia mstari huu.

Waebrania 7:22 basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi...., 25 Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.

Mwandishi anasema anaweza kuwaokoa kabisa, ni muhimu kuzingatia hili

Neno kabisa ni neno milele katika andiko hilo. Hiyo inamaanisha kwamba Yesu anaokoa milele kwa sababu amefufuka na yu hai hivi leo. Yaani Yesu haokoi kwa mwaka mmoja, hapana, anaokoa kwa milele.

1Yohana 2:1 Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, 2 naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.

Yeye ndiye mtetezi wetu mbele za Baba. Hivyo, hatuhukumiwi kwa dhambi tena.

Uwepo wake mbele za Baba siku zote ndiyo utetezi wetu na ndiyo hakikisho la usalama wa kile tumepokea katika Yeye, kwa kua yuko hai milele na sisi tuko hai milele. Dhambi haina nguvu tena, tuna huduma yake ya ukuhani kwa ajili yetu milele.

Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

Mwamini yuko huru kutoka katika hukumu. Hakuna ina maana ya hakuna, usiweke “lakini”, hiyo inatoka kwa adui.

Waebrania 8:8 Maana, awalaumupo, asema Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, Nami nitawatimizia nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda agano jipya; 9 Halitakuwa kama agano lile nililoagana na baba zao, Katika siku ile nilipowashika mikono yao niwatoe katika nchi ya Misri. Kwa sababu hawakudumu katika agano langu, Mimi nami sikuwajali asema Bwana. 10 Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu. 11 Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa maana wote watanijua, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao. 12 Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena.

Hakuna kumbukumbu ya dhambi katika wokovu, Mungu hashikilii dhambi kwa mwamini.

Angalia hapa tena;

Waebrania 10:17 Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa.
Wewe kwa nini unakumbuka dhambi zako? Yeye hakumbuki tena.

Unyenyekevu ni kukubali kile Mungu anasema kwako, hakumbuki! Usitake kuanza kukumbusha!

Katika uzao mpya, tuna zawadi ya kutokuwa na hukumu.

Waebrania 10:12 Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu; 13 tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake. 14 Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.

Chote ambacho Kristo amefanya, amekifanya milele na ameketi mkono wa kuumne wa Mungu.

Yesu hakufanya kazi ya siku mbili au ya kujirudia rudia.

Waebrania 13:5 Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.

Tazama sentensi, "sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa", inaonyesha kujitoa. Ni maneno ya uhakika (absolute words), ni ahadi yake na kujifunga kwake HATAKUACHA KAMWE!

Isitokee wakati wowote ukajiskia au kuona umeachwa, hawezi kukuacha kwa sababu yeyote ile. Kuwepo kwake pamoja na wewe kunategemea alichofanya Kristo na sio unachotenda wewe.

Waebrania 12:22 Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi, 23 mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika,
Umefika hauko safarini kuelekea. Wokovu wako au ukombozi wako ni halisi leo.

Waebrania 9:11 Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu, 12 wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele.

Gharama aliyolipa ni mara moja na milele. Halipi kila siku, hakusamehi kila siku. Umelipiwa milele, umesamehewe milele. Unyenyekevu ni kukubali neno lake. Acha kubishana naye, anasema amepata ukombozi wa milele.
Waebrania 9:15 Na kwa sababu hii ni mjumbe wa agano jipya, ili, mauti ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya urithi wa milele.

Millele ni kinyume cha “ya muda tu”. Inamaanisha milele, kinachodumu. Wale waliomwamini Kristo wamepokea urithi wa milele kwa dhabihu ya Yesu ya mara moja kwa milele.

Utakua na maana sana ukikubaliana na neno lake ukaachana na stori za mtaani.

1Wathesalonike 5:23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo. 24 Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya.

Haya hayakuwa maombi kwakuwa Paulo hakuwa anaomba kwasababu hatuombi kwaajili ya utakaso, ni kazi ya Mungu. Lakini Paulo alikua anasisitiza uaminifu wa Mungu hapa, anatuweka wakamilifu, watakatifu na salama. Anafanya hivyo kwa sababu YEYE NI MWAMINIFU.

Katika Injili nne, Bwana wetu Yesu alifundisha kweli iyo hiyo.

Yohana 5:24 Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.

Mwamini hatahukumiwa. Amevuka mautini au hukumuni na ameingia uzimani.

Huu ndiyo uzima wa milele; kupita kutoka kifo cha kiroho kuingia uzimani, hii ilifanyika katika ufufuo, katika ukombozi. Ni kazi ya uhakika.

Yohana 10:28 Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.

[emoji123]Yesu anatoa senstensi ya uhakika na ya kibabe hapa "hakuna mtu". Hivyo hakuna kitu, ikiwamo shetani kinaweza kutuchukua mbali kutoka katika wokovu wetu. Hii ni Jumla na kamili kiasi kwamba kila mwamini anapaswa authibitishe ufahamu wake. Mwamini amesalimishwa milele katika Kristo.

Hakuna hatari ya kupotea ama kupoteza wokovu wako. Ni yeye aliyeapa kua hutapokonywa.

Acha ushamba jubali hii, huwezi kupokonyoka hata ungetaka. Yuko na wewe milele.[emoji4]

Mathayo 28:20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.

Yuko pamoja nasi hata mwisho wa dahari sio mwisho wa mwaka.

Jina la mwamini limeandikwa mbinguni.
Luka 10:20 Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.

Sisi ni raia wa ufalme wa Mungu.

Waefeso 2:19 Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu.

Sisi ni washirika kabisa wa familia ya Mungu. Sisi ni raia wa mbinguni. Sio kwamba tunajipendekeza, ndivyo ametufanya.
Wafilipi 3:20 Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;

Neno, "wenyeji" limetafsiriwa kutoka katika neno la kigiriki linalomaanisha uraia.

Hivyo wokovu wetu umepewa usalama wa milele, na hapa ndipo anaposimama mwamini, huu ndiyo uhakika wake. Huu ndiyo uhalisia wa ukombozi wetu. Simama hapo hapo, ndipo ulipo.

1Petro 1:18 Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; 19 bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.

Umekombolewa kwa bei ya thamani, usianze kujiona wa bei rahisi. Usianze kutumikishwa na utoaji wa vitu vya hovyo ili kupata kupatanishwa na Mungu au vipawa na baraka za Mungu.

Ufunuo 5:9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,
Hivyo, ukombozi wa mwamini ni katika damu ya Kristo, ni katika utu wa Yesu.

Na katika huo, tunastarehe!

Tuna amani, hakuna mashaka.

Unajisikiaje?

Fanya nijue.

Pastor Makarios

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
#WOKOVU vs #MWENENDO

Wokovu ni kazi ya Mungu mwenyewe; matendo mema yanachipuka kutokana na wokovu, na kazi za mwamini au kazi za mkristo sio wokovu.

Wokovu sio malipo kwa kutenda mema; wokovu ni kwa Imani katika Kristo Yesu pekee. Panapotumika neno “ujira/thawabu” katika maandiko ni kwaajili ya kazi/matendo ama mwenendo katika mwili wa Kristo! ujira huu si wokovu bali ni ujira kwa ajili ya huduma, maisha ya Ukristo na mwenendo hudumani, kwa kuleta nafsi kwa Yesu, kwa kukuza waamini (kufanya wafuasi/wanafunzi).

Kwahiyo, Luka 9:24-27, Yesu alikua anamaanisha ujira na si wokovu.

Hebu tusome hapa;

Luka 14:25-35 Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia, [26] Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. [27] Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. [28] Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? [29] Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, [30] wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza. [31] Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini? [32] Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali. [33] Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. [34] Chumvi ni kitu chema; lakini chumvi ikiwa imeharibika, itiwe nini ikolee? [35] Haiifai nchi wala jaa; watu huitupa nje. Mwenye masikio ya kusikilia, na asikie.

Katika mazingira hayo, mstari wa 26, Yesu anatumia hyperbole kueleza kuwa upendeleo/kipaumbele ni kumweka Kristo katika nafasi ya kwanza.

Huu sio wokovu bali ni wito kwa kuwa wakfu, wakfu kwa ajili ya Mungu na kazi ya huduma.

#Wokovu una matendo yake, lakini MATENDO SI WOKOVU

1. Yesu anawaita wanafunzi wake (Mathayo 4:18-22, Luka 5:1- 11, Yohana 1:35-51)

2. Aliwaita, wakamfuata, sasa akawapa majukumu/kazi (Mathayo 10:1-15, Marko 6:7-11, Luka 9:1-5)

3. Sasa anawaita au anawataka katika kujitoa zaidi (deeper commitment)

#WOKOVU UNAPATIKANA #MARA MOJA TU, KUKUA KIROHO NA KUTAKASWA NI #ENDELEVU (kitu kinachoendelea kila siku).

KUNA WAAMINI WASIOZAA MATUNDA

Wakristo wenye matendo/ mwenendo mbaya

Hebu tazama hapa;

1Wakorintho 3:1 Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. [2] Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi, [3] kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? [4] Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu?

Mstari wa 1

Neno “rohoni” linamaanisha vitu ambavyo vinahusiana na Roho.

Hakuweza kuzungumza nao kama watu wa rohoni bali kama watu wa mwilini. Hii inamaanisha kuwa watu aliokua anawaandikia walikaua ni watu wa “rohoni” yaani walikua ni wa Roho; walikuwa wamepokea Roho ambayo ni ya Mungu.

1Wakorintho 2:10 Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. [11] Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. [12] Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. [13] Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. [14] Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni. [15] Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu. [16] Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.

Walikua wa “rohoni” kwasababu Roho anakaa ndani yao.

1Wakorintho 3:16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

1Wakorintho 6:11 Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

1Wakorintho 6:19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; [20] maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.

Watu hawa wameoshwa, wametakaswa, wamehesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu, wao ni hekalu la Mungu, wana Roho Mtakatifu ndani yao. Hivyo ni wa “rohoni” kwa kuzaliwa, lakini hakuweza kuzungumza nao kwa namna ya “rohoni” bali kama watu wa mwilini kama watoto wachanga katika Kristo.

Neno “mwilini” (carnal- KJV) limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “sarkinos” –ya/wa mwilini. (Of the flesh)

Mwamini sio wa mwilini lakini ni wa Roho. Matumizi ya neno “wa mwilini” kwa mwamini ni kuelezea matendo/mwenendo mbaya. Matumizi ya neno “wa mwilini” ni matumizi ya lugha yanayoonesha hali tofauti na uhalisia (an oxymoron); ni kuonyesha au kuelekezea tabia yao ambayo imekua tofauti na asili yao (ya rohoni).

Yaani wao ni wa rohoni, lakini matendo yao ni ya mwilini, wanaenenda kama watu wa kawaida, kama watu wasio na Roho.

Chunguza mwenendo wao

1Wakorintho 1:10 Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja. [11] Kwa maana, ndugu zangu, nimearifiwa habari zenu na wale walio wa nyumbani mwa Kloe, ya kwamba iko fitina kwenu.

1Wakorintho 3:3 kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?

1Wakorintho 5:1 Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.

1Wakorintho 6:1 Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu? [2] Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo?

1. Kulikua na mashindano/mizozo (contentions) hawakua wanazungumza kitu kimoja (hawakuwa na kauli moja), kulikua na kutokuelewana baina yao

2. Kulikua na migongano/ugomvi, wivu, kutengana baina yao

3. Mwamini alimchukua mke wa babaye

4. Walikwenda katika mahakama za wasioamini ili kuamua mambo yanayowahusu waamini

5. Hawakuenenda katika upendo, hawakuwa wanawajali wengine (walio waamini) katika mambo waliyokuwa wanafanya.

Ni wazi kuwa, hawakuwa wanaennenda kama watu wa rohoni, walikua kama watu wa mwilini. Kwa hiyo matendo/mwenendo wao ulikua mbaya licha ya kuwa wameokolewa (wamepata wokovu).

#Katika waraka huo huo Paulo #aliwasifia baadhi ya waamini wenye mwenendo #mzuri;

1Wakorintho 6:15 Tena ndugu, nawasihi; (mnawajua watu wa nyumbani mwa Stefana kwamba ni malimbuko ya Akaya, nao wamejitia katika kazi ya kuwahudumu watakatifu); [16] watiini watu kama hawa, na kila mtu afanyaye kazi pamoja nao, na kujitaabisha. [17] Nami nafurahi kwa sababu ya kuja kwao Stefana na Fortunato na Akaiko; maana hawa wamenikirimia kwa wingi yale niliyopungukiwa kwenu. [18] Maana wameniburudisha roho yangu, na roho zenu pia; basi wajueni sana watu kama hao.

Anawataja wale waliokuwa katika nyumba ya Stefana na jinsi ambavyo walijitoa kwaajili ya kuwahudumia watakatifu.

Anawataja Fortunato na Akaiko jinsi walivyomkirimia (Paulo) na watakatifu wengine

MWENENDO SIO WOKOVU, LAKINI MATENDO AU MWENENDO UNA UJIRA WAKE na pia ujira wake sio vitu (material).

Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

#Matendo/mwenendo mzuri una shina katika asili yetu; tunaenenda katika mwenendo mwema si ili tuokolewe,tunaenenda na kutembea katika hayo kwasababu tumeumbwa na Mungu kufanya matendo mema.

TUENDELEE KUTENDA MEMA NA KUWA NA MWENENDO MZURI BILA KUSAHAU KUWA MWENENDO SIO WOKOVU!

Pst Felician Makarios

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
#WOKOVU vs #MWENENDO

Wokovu ni kazi ya Mungu mwenyewe; matendo mema yanachipuka kutokana na wokovu, na kazi za mwamini au kazi za mkristo sio wokovu.

Wokovu sio malipo kwa kutenda mema; wokovu ni kwa Imani katika Kristo Yesu pekee. Panapotumika neno “ujira/thawabu” katika maandiko ni kwaajili ya kazi/matendo ama mwenendo katika mwili wa Kristo! ujira huu si wokovu bali ni ujira kwa ajili ya huduma, maisha ya Ukristo na mwenendo hudumani, kwa kuleta nafsi kwa Yesu, kwa kukuza waamini (kufanya wafuasi/wanafunzi).

Kwahiyo, Luka 9:24-27, Yesu alikua anamaanisha ujira na si wokovu.

Hebu tusome hapa;

Luka 14:25-35 Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia, [26] Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. [27] Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. [28] Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? [29] Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, [30] wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza. [31] Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini? [32] Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali. [33] Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. [34] Chumvi ni kitu chema; lakini chumvi ikiwa imeharibika, itiwe nini ikolee? [35] Haiifai nchi wala jaa; watu huitupa nje. Mwenye masikio ya kusikilia, na asikie.

Katika mazingira hayo, mstari wa 26, Yesu anatumia hyperbole kueleza kuwa upendeleo/kipaumbele ni kumweka Kristo katika nafasi ya kwanza.

Huu sio wokovu bali ni wito kwa kuwa wakfu, wakfu kwa ajili ya Mungu na kazi ya huduma.

#Wokovu una matendo yake, lakini MATENDO SI WOKOVU

1. Yesu anawaita wanafunzi wake (Mathayo 4:18-22, Luka 5:1- 11, Yohana 1:35-51)

2. Aliwaita, wakamfuata, sasa akawapa majukumu/kazi (Mathayo 10:1-15, Marko 6:7-11, Luka 9:1-5)

3. Sasa anawaita au anawataka katika kujitoa zaidi (deeper commitment)

#WOKOVU UNAPATIKANA #MARA MOJA TU, KUKUA KIROHO NA KUTAKASWA NI #ENDELEVU (kitu kinachoendelea kila siku).

KUNA WAAMINI WASIOZAA MATUNDA

Wakristo wenye matendo/ mwenendo mbaya

Hebu tazama hapa;

1Wakorintho 3:1 Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. [2] Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi, [3] kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? [4] Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu?

Mstari wa 1

Neno “rohoni” linamaanisha vitu ambavyo vinahusiana na Roho.

Hakuweza kuzungumza nao kama watu wa rohoni bali kama watu wa mwilini. Hii inamaanisha kuwa watu aliokua anawaandikia walikaua ni watu wa “rohoni” yaani walikua ni wa Roho; walikuwa wamepokea Roho ambayo ni ya Mungu.

1Wakorintho 2:10 Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. [11] Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. [12] Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. [13] Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. [14] Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni. [15] Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu. [16] Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.

Walikua wa “rohoni” kwasababu Roho anakaa ndani yao.

1Wakorintho 3:16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

1Wakorintho 6:11 Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

1Wakorintho 6:19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; [20] maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.

Watu hawa wameoshwa, wametakaswa, wamehesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu, wao ni hekalu la Mungu, wana Roho Mtakatifu ndani yao. Hivyo ni wa “rohoni” kwa kuzaliwa, lakini hakuweza kuzungumza nao kwa namna ya “rohoni” bali kama watu wa mwilini kama watoto wachanga katika Kristo.

Neno “mwilini” (carnal- KJV) limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “sarkinos” –ya/wa mwilini. (Of the flesh)

Mwamini sio wa mwilini lakini ni wa Roho. Matumizi ya neno “wa mwilini” kwa mwamini ni kuelezea matendo/mwenendo mbaya. Matumizi ya neno “wa mwilini” ni matumizi ya lugha yanayoonesha hali tofauti na uhalisia (an oxymoron); ni kuonyesha au kuelekezea tabia yao ambayo imekua tofauti na asili yao (ya rohoni).

Yaani wao ni wa rohoni, lakini matendo yao ni ya mwilini, wanaenenda kama watu wa kawaida, kama watu wasio na Roho.

Chunguza mwenendo wao

1Wakorintho 1:10 Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja. [11] Kwa maana, ndugu zangu, nimearifiwa habari zenu na wale walio wa nyumbani mwa Kloe, ya kwamba iko fitina kwenu.

1Wakorintho 3:3 kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?

1Wakorintho 5:1 Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.

1Wakorintho 6:1 Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu? [2] Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo?
JamiiForums mobile app
Amen
 
Maswali ya msingi kujiuliza

1. Ni mambo gani yanatakiwa kuaminiwa ili mtu kuokoka?
2. Umeokoka? Uliamini nini?
3. Unaweza kuelezea kwa maneno rahisi nini maana ya kuokoka?

Imani katika Kristo ni KUPOKEA kutoka kwa Kristo na sio KUMPA Yesu au kutoa kwa Yesu.

“Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;”
— Yohana 1:12 (SUV)

KUAMINI SIO KUTOA BALI KUPOKEA.

Katika wokovu mtu anapokea maisha/uzima kwa imani katika injili ya Yesu Kristo pekee.

“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”
— Yoh 3:16 (SUV)

Yeye(MUNGU Baba) alitoa uzima na sisi tunaupokea. Sisi ni kazi ya mikono yake tu.

Ef 2 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁸ Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;
⁹ wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
¹⁰ Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Wokovu hautokani na sisi, sio kwa kupenda kwetu, sio kwa kustahili kwetu, sio kwa matendo yetu bali kwa neema ya bure ya Mungu.

“Akasema, Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
— Yoh 6:65 (SUV)

Mtu ambaye bado hajaokoka hana kitu cha kutoa. Sote tulikuwa tumekufa katika dhambi zetu na makosa yetu, hatukuwa na maisha ya kutoa.

“Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;”
— Ef 2:1 (SUV)

Hii ndio maana ya wokovu --MUNGU ndiye mtoaji na sisi ni wapokeaji.

“Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?”
— Rum 8:32 (SUV)

Matendo yetu yote yalikuwa kupokea kile ambacho Mungu alitoa. Mwitikio wetu ulikuwa kuamini tu.
Hatukutoa maisha yetu ili tuokolewe. Badala yake tulipokea maisha yake na tukaokolewa.

Hivyo wokovu sio KUBADILISHANA MAISHA ILA MAISHA MAPYA KUTOKA MAUTINI KWENDA UZIMANI.

“Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.”
— Yoh 5:24 (SUV)

“Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.”
— Rum 8:2 (SUV)

Hivyo haiwezekani kwa mwamini kukosa kile Mungu alikwisha kutoa, kilichopo ni yeye(mwamini) kuja kwenye uhalisia wa kila kitu chema kilichoko ndani yake ndani ya Kristo.

IMANI KATIKA KRISTO

2Timotheo 3:15-16 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁵ na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.
¹⁶ Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

Wokovu ni kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.

“Paulo, mtumwa wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa aihubiri Injili ya Mungu;”
— Rum 1:1 (SUV)

“Sasa na atukuzwe yeye awezaye kuwafanya imara, sawasawa na injili yangu na kwa kuhubiriwa kwake Yesu Kristo, sawasawa na ufunuo wa ile siri iliyositirika tangu zamani za milele,”
— Rum 16:25 (SUV)

Kujua maandiko haina maana ya kuyakariri bali kuyaelewa kiasi cha kuweza kuyaelezea/ kuyafasiri kwa usahihi wake.
2Petro 1:16

Kuyaelewa maandiko matakatifu sio kipaji, au uwezo ambao mtu anazaliwa nao bali kwa kuyapata maarifa yaani kufundishwa, kuwa stadi/mahiri.

Ustadi/umahiri wa Timotheo ulionekana katika uwezo wake wa kufundisha maandiko matakatifu kwa usahihi.

Wokovu ambao ni kwa imani katika Kristo ni ujumbe wa maandiko matakatifu ukiwa umejikita katika utu wa Yesu Kristo.

Waamini hawatarajiwi kwa njia yoyote kuishi katika msingi wa dhahania, hisia au misemo ila katika msingi wa imani katika maandiko matakatifu.

Luka 24:25-27, 1Petr1:10-11, Rumi 1:1-4, Gal 3:6-8, Yohana 6:26-35 anza kwanza(1-25)

●Kumwamini Yeye ni kupokea uzima.
●Tofauti kati ya kupokea miujiza na kumpokea Yesu (mkate wa uzima)
●kumwamini Yeye ambaye Mungu alimtuma
●Yeye ni mkate wa uzima na yule amwaminiye Yeye hataona njaa kamwe.
●Alikuja toka mbinguni kufanya mapenzi ya Baba yake ambayo ni kuwapa uzima wale watakaomwamini.
●Aliyemwona Mwana na kumwamini anao uzima wa milele naye atamfufua siku ya mwisho.
●Atakaye mwamini Yeye anao uzima wa milele.

Yohana 6:60-66
●Imani ya uponyaji na miujiza sio sawa na imani kwa Kristo kwa wokovu. Mtu anaweza kutenda miujiza kwa jina la Yesu na asiwe mwamini.
Luka 10:1, 17, 9:49

Imani kwa Kristo kupata wokovu sio sawa na imani ya kupokea uponyaji na miujiza.

“Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.”
— Mat 7:21 (SUV)

Ni jinsi gani mtu anaingia katika ufalme wa mbinguni?
●Aliongea kuhusu kuingia mbinguni katika Yoh 3:3-5
●Kuzaliwa mara ya pili Yoh 3:16-17
●KUMWAMINI YEYE alirejea katika kuamini katika kufufuka kwake. Yoh 3:14,15,16-17
●Kuinuliwa ni ufufuo kutoka katika wafu

Mathayo 7:21
Hakusema "Yeye atakayebakia kufanya mapenzi ya Baba yangu" bali "Yeye afanye mapenzi ya Baba yangu"

Mathayo 7:22-23
Hakuwa anarejea juu ya kupoteza wokovu. (Angalia muktadha) bali kutokutii ambako ndiko kutokuamini
Mathayo 7:26, 7:24-25, 7:26-27

Yeye alikuwa akizungumzia wale ambao husikia maneno yake na wasiwe na imani kwa wokovu wake.

Watu wanaweza kupokea miujiza na hata kutoa mapepo kwa jina lake lakini wasiamini injili katika kufa na kufufuka kwake.

Yohana alimaanisha nini kwa "hawakumpokea?"

Yohana 1:12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

Hivyo, kumpokea kunamwamini Yeye- katika jina lake ni katika injili! Neno "kuamini" linamaanisha kuwa na imani ndani ya...

Angalia maneno "kama wengi waliompokea", sio "wengi waliopokea muujiza". Ndiyo sababu wengi waliopokea miujiza, uponyaji kutoka kwake, hawakupokea / kumwamini, kama ilivyokuwa katika Yohana 6.

Imani ya uponyaji au matendo ya nguvu/miujiza ni tofauti na imani katika Kristo iletayo uzima wa milele.

Kwamba mtu anaweza kuamini kupokea uponyaji lakini asimwamini Kristo atoaye uzima wa milele.

Sasa ni jinsi gani mtu anaokoka?

Mtume Paulo anaelezea katika Rumi 10: 8-17
Neno (ujumbe) wa imani (mstari wa 8) ni Injili (Mstari wa 16, 17), ambayo alikuwa amefafanua katika mstari wa 9 kama ufufuo wa Yesu kutoka kwa wafu.
ambayo ni nguvu ya Mungu kwa wokovu.

Hiyo tuu mtu anapoiamini anakuwa ameokoka/ kupata wokovu.

Kwa maneno mengine kama ujumbe aliohubiriwa mtu haumhusu(SIO) Yesu yaani kufufuka kwake kutoka kwa wafu ili kuhesabiwa haki kwetu, mpokeaji wa ujumbe huo mwingine HAJAOKOKA.

Hii haimjalishi mhubiri na msikiaji, kwa sababu injili pekee ndio ujumbe wenye nguvu ya kuweza kuokoa.

Imani katika Kristo ni imani katika injili ya Kristo; katika ufufuo wake. Hiyo ndiyo imani ya wokovu.
pale unapovka chaka la fisi bila kujeruhiwa,tayari unakuwa umeokoka!!
 
pale unapovka chaka la fisi bila kujeruhiwa,tayari unakuwa umeokoka!!
Rudia tena na tena kusoma. Kuokolewa na hatari mbalimbali nao ni aina ya wokovu mwingine ila sio WOKOVU kama unaoelezewa katika maandiko matakatifu. Uko mahususi kabisa. Rudia tena kusoma kwa umakini

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
Kuokoka ni raha sana nina raha ya ajabu sana baada ya kuokoka nina amani rohoni

LIBARIKIWE JINA LA YESU KRISTO
 
Wokovu ni nini?
Au Kuokoka ni Nini?

Kwa mara ya kwanza katika nyaraka neno “wokovu” linatajwa ni katika kitabu cha Warumi. Warumi 1:16 Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.

Neno Wokovu lililotumika hapa lina maana ya kuokoa; au kuleta katika usalama. Hii inaweza kuwa kimwili au kiroho. Pia humaanisha ukombozi au hutumika kuhusiana na afya; uponyaji.

Neno hili huwa na neno mzizi (kitenzi) lenye maana ya kuokoa, kuokolewa, au kukombolewa. Linaweza pia kuwa na maana ya kutunza, kuponya, au kukifanya kitu kuwa kizima.

Katika Biblia, maneno hayo yalitumika na waandishi kwa kuhusiana na utunzaji kutoka katika hatari au uovu, hivyo ni kusema: “wokovu kutoka” au “kuokolewa kutoka”. Hivyo, kuna uhitaji wa kuzingatia kwa umakini jinsi gani waandishi waliyatumia, katika muktadha, na sio kufikiri tu kwamba walimaanisha kitu kimoja walipotumia maneno hayo. Kwa asili, maneno wokovu na okoa au okoka ni maneno mapana au yenye maana pana, ni maneno ya jumla, na hivyo lazima yatafsiriwe ndani ya muktadha ambamo yalitumika na waandishi.

Katika Nyaraka, kitenzi cha neno “wokovu” hutumika kimsingi kabisa kwa kurejea (kuongelea) kazi ya Kristo, yaani utimilifu wa yote ambayo manabii waliyasema kuhusu mateso yake kwa ajili ya dhambi za wanadamu na matokeo yake. Maandiko yafuatayo yanaelezea baadhi ya maeneo ambamo neno hilo limetumika hivyo.

Warumi 5:9 Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. 10 Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake; zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake

Warumi 8:24 Kwa maana tuliokolewa kwa taraja; lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana, hakuna taraja tena. Kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho?

Warumi 9:27 Isaya naye atoa sauti yake juu ya Israeli, kusema, Hesabu ya wana wa Israeli, ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari, ni mabaki yao tu watakaookolewa

2Timotheo 1:9 ambaye alituokoa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu sisi, bali kwa kadiri ya makusudi yake yeye na neema yake. Neema hiyo tulipewa katika Kristo Yesu tangu milele,

Waebrania 7:25 Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.

Kwa uwazi kabisa hii inaonesha kwamba, neno (–okoa au okolewa) lilitumika mara kadhaa lakini kwa makusudi tofauti.

Hivyo, maana ya neno kwa wakati itaamuliwa na muktadha ambamo limetumiwa na mwandishi. Kwamba, neno hilo lisipewe matumizi ya jumla wakati wa kujifunza maandiko.
Vivyo hivyo kwa neno “wokovu”.

Baada ya kusema hivyo. Swali la msingi la kuuliza ni: Wokovu ni nini?

Maelezo ya Paulo katika barua yake ya pili kwa Timotheo yanatupa mwongozo.

2Timotheo 3:15 na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.

Kwa uwazi kabisa, wokovu unaozungumzwa hapa ni katika Kristo.

Wokovu kutoka katika nini?

Mathayo 1:21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao

Luka 1:77 wajulishe watu wake wokovu, Katika kusamehewa dhambi zao.

Mosi, kutoka katika maandiko hapo juu, inaweza kuonekana kwa uwazi kabisa kwamba wokovu ulio kwa imani katika Kristo Yesu unaongelea habari ya kuokolewa au kukombolewa kutoka katika dhambi na matokeo au madhara yake.

Pili, kwa kuwa Kristo ndiye aliyeokoa kutoka dhambini, hivyo Kristo ni Mwokozi. Hii ina onesha kwamba, ili kuwe na wokovu lazima kuwe na Mwokozi.

Mwokozi ni nani?

Neno “mwokozi” limetumiwa na waandishi kuongelea mtendaji; yule anayefanya kitendo cha kuokoa. Hivyo, ili uwe na wokovu lazima kuwe na mwokozi.

Ki-historia, neno mwokozi (soter) lilitumikwa kwa wana wa kifalme (princes) kabla ya nyakati za Kristo (kabla ya Kristo kuja). Lilikuwa linaongelea au kurejea kwa wale ambao wameshinda na kudhibiti maeneo waliyoyateka na kuwa imara kuzilinda nchi au ardhi zao. Mamlaka ya mfalme au mwana mfalme inategemea na jinsi gani anaweza kuilinda milki yake. Neno hili lilipatikana kutokea hapo.

Hivyo, kwa kuwa kitenzi cha neno wokovu kina maana ya kulinda kutoka hatari, kutoka madhara au uovu, hivyo basi mwokozi ni ambaye anafanya jukumu hilo au kazi hiyo. Analinda mbali na uovu, kutoka katika hatari na madhara ya dhambi.

1Timotheo 4:10 kwa maana twajitaabisha na kujitahidi kwa kusudi hili, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio

2Timotheo 1:10 na sasa inadhihirishwa kwa kufunuliwa kwake Mwokozi wetu Kristo Yesu; aliyebatili mauti, na kuufunua uzima na kutokuharibika, kwa ile Injili

Tito 1:3 akalifunua neno lake kwa majira yake katika ule ujumbe niliowekewa amana mimi kwa amri ya Mwokozi wetu Mungu

Tito 1:4 kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tuishirikiyo. Neema na iwe kwako na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu

Tito 2:10 wasiwe waibaji; bali wauonyeshe uaminifu mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote

Tito 2:13 ukilitazamia tumaini lenye 5haria na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;

Tito 3:4 Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa, alituokoa

Tito 3:6 ambaye alitumwagia kwa wingi, kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu Mwokozi ndiye afanyaye kitendo.

Hivyo, kuwa Mwokozi kwa Kristo ni ofisi. Pia, kama katika Luka 1:47 na Luka 2:11, Paulo hapa alikuwa anathibitisha uungu wa Yesu. Anamwita Mwokozi wetu kwa sababu mwokozi ni Mungu aliyefanyika mwanadamu. Alielezea kweli hii alipoandika barua ya kwanza kwa Timotheo.

1Timotheo 3:16 Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.

Kutokana na mistari hapo juu katika Nyaraka, Yesu ameelezewa kama Mwokozi wetu, (mwokozi wa mwili wake) na pia Mwokozi wa Ulimwengu.

Yohana 3:16-18 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. – 18 Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.

Iko wazi, jinsi wanadamu wanaokolewa kupitia Yeye, ni kwa imani katika Injili (ya Kristo)

Ushahidi mwingine juu ya hilo:

Marko 16:15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. 16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa

Warumi 10:8 Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo. 9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. 10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu,

Hivyo, mtu anapokea wokovu kwa imani katika Injili (ya Kristo). Kwa hiyo, wokovu utapokelewa kwa imani pekee katika mwokozi (soter).

Swali la kiakili la kuuliza katika msingi huu ni:

Ni wakati gani mtu anaokolewa?

Ili kuelewa ni wakati gani mtu anaokolewa, ni muhimu kwanza kujua ni namna gani mtu anaokolewa.

Maelezo ya Paulo kwa Warumi yanatupa mwongozo;

Warumi 10:8 Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo. 9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. 10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.

Katika mstari wa 8, anaeleza ujumbe unaohubiriwa kuwa ni ujumbe wa Imani. Hii ndio Injili. Katika mstari wa 9 alieleza zaidi jinsi gani mpokeaji wa Injili, kwa mwitikio wa ujumbe aliousikia; anakiri kwa kinywa chake na kuamini kwa moyo. Hiyo ndiyo sababu kutoka mstari wa 11 mpaka 13 alitamka namna hii;

Warumi 10:11 Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika. – 12 Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; 13 kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka.

Hivyo, mtu anaokolewa muda ule anapoamini Injili ya Kristo (katika moyo wake).

Imetolewa katika kitabu Cha Siku 30 za Mwamini Mpya.
Utakipata Bure hapa
View: https://t.me/kainosmedia/1122
 
Back
Top Bottom