Ni wakati gani mtu anaokoka?

Ni wakati gani mtu anaokoka?

Urban86

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2014
Posts
279
Reaction score
132
Maswali ya msingi kujiuliza

1. Ni mambo gani yanatakiwa kuaminiwa ili mtu kuokoka?
2. Umeokoka? Uliamini nini?
3. Unaweza kuelezea kwa maneno rahisi nini maana ya kuokoka?

Imani katika Kristo ni KUPOKEA kutoka kwa Kristo na sio KUMPA Yesu au kutoa kwa Yesu.

“Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;”
— Yohana 1:12 (SUV)

KUAMINI SIO KUTOA BALI KUPOKEA.

Katika wokovu mtu anapokea maisha/uzima kwa imani katika injili ya Yesu Kristo pekee.

“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”
— Yoh 3:16 (SUV)

Yeye(MUNGU Baba) alitoa uzima na sisi tunaupokea. Sisi ni kazi ya mikono yake tu.

Ef 2 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁸ Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;
⁹ wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
¹⁰ Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Wokovu hautokani na sisi, sio kwa kupenda kwetu, sio kwa kustahili kwetu, sio kwa matendo yetu bali kwa neema ya bure ya Mungu.

“Akasema, Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
— Yoh 6:65 (SUV)

Mtu ambaye bado hajaokoka hana kitu cha kutoa. Sote tulikuwa tumekufa katika dhambi zetu na makosa yetu, hatukuwa na maisha ya kutoa.

“Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;”
— Ef 2:1 (SUV)

Hii ndio maana ya wokovu --MUNGU ndiye mtoaji na sisi ni wapokeaji.

“Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?”
— Rum 8:32 (SUV)

Matendo yetu yote yalikuwa kupokea kile ambacho Mungu alitoa. Mwitikio wetu ulikuwa kuamini tu.
Hatukutoa maisha yetu ili tuokolewe. Badala yake tulipokea maisha yake na tukaokolewa.

Hivyo wokovu sio KUBADILISHANA MAISHA ILA MAISHA MAPYA KUTOKA MAUTINI KWENDA UZIMANI.

“Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.”
— Yoh 5:24 (SUV)

“Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.”
— Rum 8:2 (SUV)

Hivyo haiwezekani kwa mwamini kukosa kile Mungu alikwisha kutoa, kilichopo ni yeye(mwamini) kuja kwenye uhalisia wa kila kitu chema kilichoko ndani yake ndani ya Kristo.

IMANI KATIKA KRISTO

2Timotheo 3:15-16 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁵ na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.
¹⁶ Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

Wokovu ni kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.

“Paulo, mtumwa wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa aihubiri Injili ya Mungu;”
— Rum 1:1 (SUV)

“Sasa na atukuzwe yeye awezaye kuwafanya imara, sawasawa na injili yangu na kwa kuhubiriwa kwake Yesu Kristo, sawasawa na ufunuo wa ile siri iliyositirika tangu zamani za milele,”
— Rum 16:25 (SUV)

Kujua maandiko haina maana ya kuyakariri bali kuyaelewa kiasi cha kuweza kuyaelezea/ kuyafasiri kwa usahihi wake.
2Petro 1:16

Kuyaelewa maandiko matakatifu sio kipaji, au uwezo ambao mtu anazaliwa nao bali kwa kuyapata maarifa yaani kufundishwa, kuwa stadi/mahiri.

Ustadi/umahiri wa Timotheo ulionekana katika uwezo wake wa kufundisha maandiko matakatifu kwa usahihi.

Wokovu ambao ni kwa imani katika Kristo ni ujumbe wa maandiko matakatifu ukiwa umejikita katika utu wa Yesu Kristo.

Waamini hawatarajiwi kwa njia yoyote kuishi katika msingi wa dhahania, hisia au misemo ila katika msingi wa imani katika maandiko matakatifu.

Luka 24:25-27, 1Petr1:10-11, Rumi 1:1-4, Gal 3:6-8, Yohana 6:26-35 anza kwanza(1-25)

●Kumwamini Yeye ni kupokea uzima.
●Tofauti kati ya kupokea miujiza na kumpokea Yesu (mkate wa uzima)
●kumwamini Yeye ambaye Mungu alimtuma
●Yeye ni mkate wa uzima na yule amwaminiye Yeye hataona njaa kamwe.
●Alikuja toka mbinguni kufanya mapenzi ya Baba yake ambayo ni kuwapa uzima wale watakaomwamini.
●Aliyemwona Mwana na kumwamini anao uzima wa milele naye atamfufua siku ya mwisho.
●Atakaye mwamini Yeye anao uzima wa milele.

Yohana 6:60-66
●Imani ya uponyaji na miujiza sio sawa na imani kwa Kristo kwa wokovu. Mtu anaweza kutenda miujiza kwa jina la Yesu na asiwe mwamini.
Luka 10:1, 17, 9:49

Imani kwa Kristo kupata wokovu sio sawa na imani ya kupokea uponyaji na miujiza.

“Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.”
— Mat 7:21 (SUV)

Ni jinsi gani mtu anaingia katika ufalme wa mbinguni?
●Aliongea kuhusu kuingia mbinguni katika Yoh 3:3-5
●Kuzaliwa mara ya pili Yoh 3:16-17
●KUMWAMINI YEYE alirejea katika kuamini katika kufufuka kwake. Yoh 3:14,15,16-17
●Kuinuliwa ni ufufuo kutoka katika wafu

Mathayo 7:21
Hakusema "Yeye atakayebakia kufanya mapenzi ya Baba yangu" bali "Yeye afanye mapenzi ya Baba yangu"

Mathayo 7:22-23
Hakuwa anarejea juu ya kupoteza wokovu. (Angalia muktadha) bali kutokutii ambako ndiko kutokuamini
Mathayo 7:26, 7:24-25, 7:26-27

Yeye alikuwa akizungumzia wale ambao husikia maneno yake na wasiwe na imani kwa wokovu wake.

Watu wanaweza kupokea miujiza na hata kutoa mapepo kwa jina lake lakini wasiamini injili katika kufa na kufufuka kwake.

Yohana alimaanisha nini kwa "hawakumpokea?"

Yohana 1:12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

Hivyo, kumpokea kunamwamini Yeye- katika jina lake ni katika injili! Neno "kuamini" linamaanisha kuwa na imani ndani ya...

Angalia maneno "kama wengi waliompokea", sio "wengi waliopokea muujiza". Ndiyo sababu wengi waliopokea miujiza, uponyaji kutoka kwake, hawakupokea / kumwamini, kama ilivyokuwa katika Yohana 6.

Imani ya uponyaji au matendo ya nguvu/miujiza ni tofauti na imani katika Kristo iletayo uzima wa milele.

Kwamba mtu anaweza kuamini kupokea uponyaji lakini asimwamini Kristo atoaye uzima wa milele.

Sasa ni jinsi gani mtu anaokoka?

Mtume Paulo anaelezea katika Rumi 10: 8-17
Neno (ujumbe) wa imani (mstari wa 8) ni Injili (Mstari wa 16, 17), ambayo alikuwa amefafanua katika mstari wa 9 kama ufufuo wa Yesu kutoka kwa wafu.
ambayo ni nguvu ya Mungu kwa wokovu.

Hiyo tuu mtu anapoiamini anakuwa ameokoka/ kupata wokovu.

Kwa maneno mengine kama ujumbe aliohubiriwa mtu haumhusu(SIO) Yesu yaani kufufuka kwake kutoka kwa wafu ili kuhesabiwa haki kwetu, mpokeaji wa ujumbe huo mwingine HAJAOKOKA.

Hii haimjalishi mhubiri na msikiaji, kwa sababu injili pekee ndio ujumbe wenye nguvu ya kuweza kuokoa.

Imani katika Kristo ni imani katika injili ya Kristo; katika ufufuo wake. Hiyo ndiyo imani ya wokovu.
 
INJILI NI NINI?

Rumi 1:1-2 Paulo, mtumwa wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa aihubiri Injili ya Mungu;

"Injili ya Mungu" katika muktadha inarejea habari/ujumbe uliotangazwa katika Agano la kale. Habari hiyo ya ahadi ya Mungu ilinenwa na manabii wa Mungu katika maandiko matakatifu(Mwanzo hadi Malaki).

Mtume Paulo

kufufuka kwa Yesu kutoka kwa wafu.

Anailezea zaidi (Rumi 1:16) kwamba ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.

Nguvu ya Mungu (injili ya Yesu Kristo) katika muktadha ilikuwa katika mrejeo wa ufufuo ya Yesu kutoka katika wafu.

Hivyo injili ya Kristo ambayo ni uweza wa Mungu uuletao wokovu ni kuhusu Ufufuo wa Yesu kutoka kwa wafu. Habari hiyo iliahidiwa na Mungu kupitia manabii katika maandiko matakatifu.

Weka umakini mambo anayosema Mtume Paulo katika 1Kor 15:3-4 ...ya kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko; na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;

Paulo alisisitiza kwamba kweli za injili ya Kristo ni kulingana na maandiko matakatifu sawa na Yesu alivyonena(Luka 24:25-27) na mtume Petro (1Pet1:10-11) ikielezwa Injili ya Kristo itakuwa kweli za kuhusu mateso ya Yesu na utukufu utakaokuwako baada ya hayo.(kufa, kuzikwa na kufufuka) ambazo zilikuwepo katika unabii wa manabii.

Mtume Paulo anazidi kusisistiza tena katika 1Kor 15:12-19 kwamba Kristo kufufuka katika wafu ndio uhalisia wa imani yetu, uhakika wetu pia ya kwamba tumefufuka kutoka katika wafu.

Ni wazi kabisa injili ambayo Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wakahubiri ulimwenguni ni ufufuo wake kutoka kwa wafu. Marko 16:15 Hivyo injili ya Mungu ni kweli ya kuwa alimfufua Yesu kutoka kwa wafu.

Rumi 4:25 ambaye alitolewa kwa ajili ya makosa yetu, na kufufuliwa ili mpate kuhesabiwa haki.

Hivyo imani katika Kristo/Injili ni imani katika ufufuo. Na huu ndio ujumbe PEKEE uokoao. Hakuna ufufuo kama hakingekuwepo kifo chake, Mungu alichokifanya ilikuwa kumfufua kutoka kwa wafu na katika ufufuo huo tumepata UZIMA, KUHESABIWA HAKI, WOKOVU.

Hiki ndicho kilichoahidiwa zamani hizo kwa mababa zetu na manabii katika maandiko matakatifu.

Angalia jinsi paulo anavyosisitiza Jinsi gani mtu anaokoka katika barua zake Rumi 10:8-9, 1Kor 15:1-2, Efeso 2:8-9 Hivyo ndio namna wokovu unavyopokelewa... Imani katika injili imani katika ufufuo.

Sasa ikiwa injili ni ujumbe kuhusu ufufuo wa Yesu kwa ajili ya kuhesabiwa haki kwetu, wokovu hii inamaanisha kuwa Injili ya Kristo haiwezi kulenga watu mahitaji ya kimwili au vitu vya kimwili.

Kwa hiyo, kuhubiri mahubiri yaliyozingatia hali za watu, miujiza na uponyaji na sio juu ya utu wa Yesu (ufufuo wake) sio kuhubiri injili! Ikiwa ni injili ya Kristo, itamzingatia Yeye (ufufuo wake kutoka kwa wafu) peke yake.

Paulo alionya juu ya hili katika barua yake kwa Kanisa la Korintho 1Kor 2:1-5
Jambo la kwanza alilowaambia ni kwamba hakwenda awahubiri siri ya Mungu kwa ufasaha wa maneno, wala kwa hekima.

Kwa maneno mengine, wakati ujumbe hauzingatii Kristo pekee yake(ufufuo wake kutoka kwa wafu), ni ufasaha wa maneno. Alisisitiza jambo hilo hilo katika mstari wa 4 ... maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu.

Sababu ni hii
mstari 5 ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu.

Wakati ujumbe uliohubiriwa ni si kulenga Kristo (ufufuo wake kutoka wafu) imani ya mpokeaji haiko katika ufufuo wa Yesu (nguvu ya Mungu); katika injili ya Kristo, badala yake, ni katika ufasaha wa maneno wa mhubiri, maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu.

Alimaanisha nini kwa nguvu za Mungu?
1Kor 2:1-5. Paulo alikuwa akimaanisha ujumbe ambao aliwahubiria; injili ya Kristo; Yesu alisulubiwa na yeye alimfufua kutoka kwa wafu.
Ujumbe ni ndani yake wenyewe, nguvu ya Mungu ya kuokoa.

Hivyo, madhihirisho ya Roho na nguvu (Mstari wa 5) yalikuwa yanamaanisha kazi ya Roho, katika kuhubiri injili. Ndiyo sababu Paulo alisema... neno langu na kuhubiri kwangu...

Ujumbe wowote unaozingatia vitu vya kimwili, mahitaji ya kimwili na kihisia ya watu, miujiza, uponyaji, fedha, mali na kama hivyo, na sio juu ya ufufuo wa Yesu hauwezi kuokoa. Ni injili ya Kristo tu ndiyo ina uwezo wa kumwokoa mwanadamu!

Ni muhimu kutambua kwamba huu ulikuwa ujumbe uliohubiriwa na Mitume na wengine wote kupitia kitabu cha Matendo.

1. Mtume Petro

Mdo 2:29-37
Lengo la ujumbe wake lilikuwa ufufuo wa Yesu kutoka kwa wafu na kupaa kwake kwa mkono wa kulia wa Baba (Mstari wa 31, 32, na 33).
Mdo 3:12-15, 25-26
mst.15 ..."mkamwua yule Mkuu wa uzima, ambaye Mungu amemfufua katika wafu; na sisi tu mashahidi wake."
mst.18..."Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo."
Mdo 5:28-42
mst.30... "Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti."
Mdo 10:36-43
mst.43 ..."Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi."

2. Stefano
Mdo 7:52-56
Jambo kuu la ujumbe wake: Yesu alifufuka kutoka kwa wafu na kutukuzwa,
amesimama Mkono wa Kuume wa Mungu!

3. Filipo
Mdo 8:4-12
mst.12... "Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake."
Mdo 8:30-35 Yesu alikuwa lengo la ujumbe wa Filipo.

4. Paulo
Mdo 13:27-34, 37-38
● Katika mstari 27 hadi 29, Paulo alizungumza kuhusu kifo cha Yesu, na uhakika wa kwamba kilikuwa utimizo wa yote yaliyoandikwa kumhusu.

● Katika mstari 30, alisema waziwazi kwamba Mungu alimfufua katika wafu

● Katika mstari 33 & 34, alinena kwa mkazo juu ya ahadi waliyopewa baba zetu, na jinsi hiyo ilivyotimizwa kwa watoto wao kwa njia ya Mungu kumfufua Yesu katika wafu.

● Katika mstari 35, Alinukuu toka Zaburi 16:10 kuhusu ufufuo wa Yesu katika wafu

● Katika mstari 37, Paulo tena kwa mara ya nne, anakazia ufufuo wa Yesu kutoka kwa wafu.

● Katika mstari 38, Paulo alihubiri msamaha kutoka kwa Maandiko.

● Katika mstari 39, Aliweka tofauti kati ya kuhesabiwa haki kwa imani katika ufufuo na kutafuta kuhesabiwa haki kwa sheria/torati ya Musa.
Hivyo, Kuhesabiwa haki kwa imani na msamaha wa dhambi kulikuwepo wakati Musa alipotoa sheria/torati.

Mdo 17:22-32
mst.31"Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu."

Ni muhimu kutambua kwamba HAKUNA MTU aliyeokolewa katika kitabu cha Matendo bila kuhubiriwa kutoka katika Maandiko.
Kwa hiyo maandiko yanabaki kuwa msingi wa imani yetu! Hiyo ni, injili ya Kristo lazima iwe na ukweli ulioainishwa katika maandiko.

Dakika ambapo ukweli huu haupo, ujumbe huo sio tena wa Kristo.
Utakachokuwa nacho ni jumbe zinazohubiriwa kwa ufasaha wa usemi na hekima, ambazo HAZINA UWEZO wa kuokoa.

Pia, ni wazi, hakuna Mtume aliyehubiri injili nyingine yoyote tofauti na injili ya ukweli, kwa hivyo Nyaraka ziliandikwa kwa nuru ya ukweli huu.

1Pet1:10-11
Walitabiri kuhusu Mateso ya Kristo na Utukufu ambao unapaswa kufuata. Ilikuwa ni msukumo wa injili yao.

Mdo 17:10-11, 12
Waberoya walichunguza maandiko. Kwa maneno mengine, Paulo aliwahubiria kutoka katika Maandiko.
Walichunguza maandiko (kila siku) ili kuthibitisha ikiwa mambo aliyofundisha yalikuwa ya kweli.

Matokeo ya uchunguzi wa maandiko ambao walifanya kulingana na kile Paulo alifundisha kutoka kwenye maandiko - wengi wao waliamini ... WOKOVU!

Yesu na Mitume wote katika kitabu cha Matendo na katika nyaraka, walihubiri kutoka kwenye maandiko. Hivyo, kuhubiri mahubiri yenye mlengo wa "mahitaji ya mwili"; "injili ya fedha"; "miujiza" na "uponyaji" kama injili ya Kristo itazalisha tu waongofu wa uongo.

Injili sio kupokea miujiza, vinginevyo wote yalioponywa katika injili nne wangeokolewa moja kwa moja.

Wala si ushuhuda wa mahitaji ya yaliyotimizwa, kuoa/kuolewa, kupata kazi mpya, kupata mtoto, nyumba na mengine kama hayo.

Injili ni ujumbe; ujumbe huo una kweli maalum...Mungu alionyesha nguvu zake katika kumfufua Yesu kutoka kwa wafu!
 
Kuokoka( read carefully )yaani kuacha matatizo ya KIMWILI kama ugomvi, ngono za kiovu, ulafi; mambo kama hayo. Kuacha fitness ni essential part ya kuokoka, kuacha majungu.

Fikiria, watu wanatembea mji wote salama, wanarudi nyumbani wanauawa na ndugu zao.
 
Hakuna haja ya kuokoka cha muhimu ni kupambna na hisia hasi na kujizoeza kuwa na upendo tu
1677230765669.jpg
 
Maswali ya msingi kujiuliza

1. Ni mambo gani yanatakiwa kuaminiwa ili mtu kuokoka?
2. Umeokoka? Uliamini nini?
3. Unaweza kuelezea kwa maneno rahisi nini maana ya kuokoka?

Imani katika Kristo ni KUPOKEA kutoka kwa Kristo na sio KUMPA Yesu au kutoa kwa Yesu.

“Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;”
— Yohana 1:12 (SUV)

KUAMINI SIO KUTOA BALI KUPOKEA.

Katika wokovu mtu anapokea maisha/uzima kwa imani katika injili ya Yesu Kristo pekee.

“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”
— Yoh 3:16 (SUV)

Yeye(MUNGU Baba) alitoa uzima na sisi tunaupokea. Sisi ni kazi ya mikono yake tu.

Ef 2 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁸ Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;
⁹ wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
¹⁰ Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Wokovu hautokani na sisi, sio kwa kupenda kwetu, sio kwa kustahili kwetu, sio kwa matendo yetu bali kwa neema ya bure ya Mungu.

“Akasema, Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
— Yoh 6:65 (SUV)

Mtu ambaye bado hajaokoka hana kitu cha kutoa. Sote tulikuwa tumekufa katika dhambi zetu na makosa yetu, hatukuwa na maisha ya kutoa.

“Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;”
— Ef 2:1 (SUV)

Hii ndio maana ya wokovu --MUNGU ndiye mtoaji na sisi ni wapokeaji.

“Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?”
— Rum 8:32 (SUV)

Matendo yetu yote yalikuwa kupokea kile ambacho Mungu alitoa. Mwitikio wetu ulikuwa kuamini tu.
Hatukutoa maisha yetu ili tuokolewe. Badala yake tulipokea maisha yake na tukaokolewa.

Hivyo wokovu sio KUBADILISHANA MAISHA ILA MAISHA MAPYA KUTOKA MAUTINI KWENDA UZIMANI.

“Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.”
— Yoh 5:24 (SUV)

“Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.”
— Rum 8:2 (SUV)

Hivyo haiwezekani kwa mwamini kukosa kile Mungu alikwisha kutoa, kilichopo ni yeye(mwamini) kuja kwenye uhalisia wa kila kitu chema kilichoko ndani yake ndani ya Kristo.

IMANI KATIKA KRISTO

2Timotheo 3:15-16 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁵ na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.
¹⁶ Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

Wokovu ni kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.

“Paulo, mtumwa wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa aihubiri Injili ya Mungu;”
— Rum 1:1 (SUV)

“Sasa na atukuzwe yeye awezaye kuwafanya imara, sawasawa na injili yangu na kwa kuhubiriwa kwake Yesu Kristo, sawasawa na ufunuo wa ile siri iliyositirika tangu zamani za milele,”
— Rum 16:25 (SUV)

Kujua maandiko haina maana ya kuyakariri bali kuyaelewa kiasi cha kuweza kuyaelezea/ kuyafasiri kwa usahihi wake.
2Petro 1:16

Kuyaelewa maandiko matakatifu sio kipaji, au uwezo ambao mtu anazaliwa nao bali kwa kuyapata maarifa yaani kufundishwa, kuwa stadi/mahiri.

Ustadi/umahiri wa Timotheo ulionekana katika uwezo wake wa kufundisha maandiko matakatifu kwa usahihi.

Wokovu ambao ni kwa imani katika Kristo ni ujumbe wa maandiko matakatifu ukiwa umejikita katika utu wa Yesu Kristo.

Waamini hawatarajiwi kwa njia yoyote kuishi katika msingi wa dhahania, hisia au misemo ila katika msingi wa imani katika maandiko matakatifu.

Luka 24:25-27, 1Petr1:10-11, Rumi 1:1-4, Gal 3:6-8, Yohana 6:26-35 anza kwanza(1-25)

●Kumwamini Yeye ni kupokea uzima.
●Tofauti kati ya kupokea miujiza na kumpokea Yesu (mkate wa uzima)
●kumwamini Yeye ambaye Mungu alimtuma
●Yeye ni mkate wa uzima na yule amwaminiye Yeye hataona njaa kamwe.
●Alikuja toka mbinguni kufanya mapenzi ya Baba yake ambayo ni kuwapa uzima wale watakaomwamini.
●Aliyemwona Mwana na kumwamini anao uzima wa milele naye atamfufua siku ya mwisho.
●Atakaye mwamini Yeye anao uzima wa milele.

Yohana 6:60-66
●Imani ya uponyaji na miujiza sio sawa na imani kwa Kristo kwa wokovu. Mtu anaweza kutenda miujiza kwa jina la Yesu na asiwe mwamini.
Luka 10:1, 17, 9:49

Imani kwa Kristo kupata wokovu sio sawa na imani ya kupokea uponyaji na miujiza.

“Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.”
— Mat 7:21 (SUV)

Ni jinsi gani mtu anaingia katika ufalme wa mbinguni?
●Aliongea kuhusu kuingia mbinguni katika Yoh 3:3-5
●Kuzaliwa mara ya pili Yoh 3:16-17
●KUMWAMINI YEYE alirejea katika kuamini katika kufufuka kwake. Yoh 3:14,15,16-17
●Kuinuliwa ni ufufuo kutoka katika wafu

Mathayo 7:21
Hakusema "Yeye atakayebakia kufanya mapenzi ya Baba yangu" bali "Yeye afanye mapenzi ya Baba yangu"

Mathayo 7:22-23
Hakuwa anarejea juu ya kupoteza wokovu. (Angalia muktadha) bali kutokutii ambako ndiko kutokuamini
Mathayo 7:26, 7:24-25, 7:26-27

Yeye alikuwa akizungumzia wale ambao husikia maneno yake na wasiwe na imani kwa wokovu wake.

Watu wanaweza kupokea miujiza na hata kutoa mapepo kwa jina lake lakini wasiamini injili katika kufa na kufufuka kwake.

Yohana alimaanisha nini kwa "hawakumpokea?"

Yohana 1:12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

Hivyo, kumpokea kunamwamini Yeye- katika jina lake ni katika injili! Neno "kuamini" linamaanisha kuwa na imani ndani ya...

Angalia maneno "kama wengi waliompokea", sio "wengi waliopokea muujiza". Ndiyo sababu wengi waliopokea miujiza, uponyaji kutoka kwake, hawakupokea / kumwamini, kama ilivyokuwa katika Yohana 6.

Imani ya uponyaji au matendo ya nguvu/miujiza ni tofauti na imani katika Kristo iletayo uzima wa milele.

Kwamba mtu anaweza kuamini kupokea uponyaji lakini asimwamini Kristo atoaye uzima wa milele.

Sasa ni jinsi gani mtu anaokoka?

Mtume Paulo anaelezea katika Rumi 10: 8-17
Neno (ujumbe) wa imani (mstari wa 8) ni Injili (Mstari wa 16, 17), ambayo alikuwa amefafanua katika mstari wa 9 kama ufufuo wa Yesu kutoka kwa wafu.
ambayo ni nguvu ya Mungu kwa wokovu.

Hiyo tuu mtu anapoiamini anakuwa ameokoka/ kupata wokovu.

Kwa maneno mengine kama ujumbe aliohubiriwa mtu haumhusu(SIO) Yesu yaani kufufuka kwake kutoka kwa wafu ili kuhesabiwa haki kwetu, mpokeaji wa ujumbe huo mwingine HAJAOKOKA.

Hii haimjalishi mhubiri na msikiaji, kwa sababu injili pekee ndio ujumbe wenye nguvu ya kuweza kuokoa.

Imani katika Kristo ni imani katika injili ya Kristo; katika ufufuo wake. Hiyo ndiyo imani ya wokovu.
Kuna Kuongoka na Kuokoka...
 
Kuna Kuongoka na Kuokoka...
Kutoka kwenye tafsiri ipi hiyo ya Biblia? Leta hapa tuone? Usichukue maneno ya mtaani ukayaleta kwenye biblia.

Biblia tafsiri ya kiswahili haina neno kuongoka. Hata tafsiri za English wala lugha za asili.

Kama ilivyo maneno katika uwanja wa sheria, kidaktari, jeshi, engineering nk maneno katika nyanja hizo hayana maana za jumla. Ndivyo hivyo hivyo maneno ya kwenye biblia yanapata maana zake ndani ya muktadha wa biblia. Ukiyapa maana toka kwenye kamusi za kawaida au 'gugo'[emoji38] lazima uende chaka.

Hivyo neno "kuokoka" litapata maana yake kulingana na biblia na sio vinginevyo.

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
Kuokoka( read carefully )yaani kuacha matatizo ya KIMWILI kama ugomvi, ngono za kiovu, ulafi; mambo kama hayo. Kuacha fitness ni essential part ya kuokoka, kuacha majungu.

Fikiria, watu wanatembea mji wote salama, wanarudi nyumbani wanauawa na ndugu zao.
Haya ni maoni yako wewe kama wewe sio kama Neno la Mungu linavyosema. Ukiacha kuliamini neno la Mungu linavyosema utautafsiri wokovu kwa maoni yako, utajiokoa kwa maoni yako, utapata mwokozi wa maoni yako. Hata mbingu na pepo itakuwa kulingana na maoni yako.

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna haja ya kuokoka cha muhimu ni kupambna na hisia hasi na kujizoeza kuwa na upendo tuView attachment 2540277
(Mtu ambaye bado hajaokoka hana kitu cha kutoa. Sote tulikuwa tumekufa katika dhambi zetu na makosa yetu, hatukuwa na maisha ya kutoa.

“Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;”
— Ef 2:1 (SUV)

Hii ndio maana ya wokovu --MUNGU ndiye mtoaji na sisi ni wapokeaji.) Hiki kifungu hujakisoma au ndio hujakielewa?

Unaposema hakuna haja ya kuokoka maana yake unamwambia Mungu usoni "Mimi sina haja na wewe! Mimi naweza kijiokoa mwenyewe ili hali niko mfu kiroho, mimi naweza kutoa upendo ingali tunajua mfu hawezi kutoa kitu chochote"

Pasipo mtu kuamini injili yu hali ileile ya ufu wa kiroho. Hana uzima wa Mungu ndani yake. Kwa maneno mengine atapotea milele asipoamini Mungu alimtoa Yesu ateswe, afe na kufufuka kwa ajili yake ili awe na uzima wa milele ndani yake.

Unahitaji kuokoka. Hakuna option/alternative nyingine yote ya kukupa uzima wa Mungu zaidi ya kumpokea Yeye mtoa uzima.


Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
(Mtu ambaye bado hajaokoka hana kitu cha kutoa. Sote tulikuwa tumekufa katika dhambi zetu na makosa yetu, hatukuwa na maisha ya kutoa.

“Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;”
— Ef 2:1 (SUV)

Hii ndio maana ya wokovu --MUNGU ndiye mtoaji na sisi ni wapokeaji.) Hiki kifungu hujakisoma au ndio hujakielewa?

Unaposema hakuna haja ya kuokoka maana yake unamwambia Mungu usoni "Mimi sina haja na wewe! Mimi naweza kijiokoa mwenyewe ili hali niko mfu kiroho, mimi naweza kutoa upendo ingali tunajua mfu hawezi kutoa kitu chochote"

Pasipo mtu kuamini injili yu hali ileile ya ufu wa kiroho. Hana uzima wa Mungu ndani yake. Kwa maneno mengine atapotea milele asipoamini Mungu alimtoa Yesu ateswe, afe na kufufuka kwa ajili yake ili awe na uzima wa milele ndani yake.

Unahitaji kuokoka. Hakuna option/alternative nyingine yote ya kukupa uzima wa Mungu zaidi ya kumpokea Yeye mtoa uzima.


Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
Kuna din 4000 mungu yupi na njia ipi ni sahihi niifuate?
 
(Mtu ambaye bado hajaokoka hana kitu cha kutoa. Sote tulikuwa tumekufa katika dhambi zetu na makosa yetu, hatukuwa na maisha ya kutoa.

“Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;”
— Ef 2:1 (SUV)

Hii ndio maana ya wokovu --MUNGU ndiye mtoaji na sisi ni wapokeaji.) Hiki kifungu hujakisoma au ndio hujakielewa?

Unaposema hakuna haja ya kuokoka maana yake unamwambia Mungu usoni "Mimi sina haja na wewe! Mimi naweza kijiokoa mwenyewe ili hali niko mfu kiroho, mimi naweza kutoa upendo ingali tunajua mfu hawezi kutoa kitu chochote"

Pasipo mtu kuamini injili yu hali ileile ya ufu wa kiroho. Hana uzima wa Mungu ndani yake. Kwa maneno mengine atapotea milele asipoamini Mungu alimtoa Yesu ateswe, afe na kufufuka kwa ajili yake ili awe na uzima wa milele ndani yake.

Unahitaji kuokoka. Hakuna option/alternative nyingine yote ya kukupa uzima wa Mungu zaidi ya kumpokea Yeye mtoa uzima.


Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
Na kwa hiyo yesu ni mjnga aliposisitiza upendo?
 
Kuna din 4000 mungu yupi na njia ipi ni sahihi niifuate?
Tunaamini kuwa Mungu wetu ni mmoja naye ameelezewa na maandiko kama Baba na Mwana.

Tunaamini kuwa Mungu mmoja na wa Kweli amejifunua kikamilifu pasipo kujibakiza katika utu wa Yesu Kristo. Tunamjua Yeye kupitia Yesu Kristo pekee.

1Kor 8 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁵ Kwa maana ijapokuwa wako waitwao miungu, ama mbinguni ama duniani, kama vile walivyoko miungu mingi na mabwana wengi;
⁶ lakini kwetu sisi Mungu ni mmoja tu, aliye Baba, ambaye vitu vyote vimetoka kwake, nasi tunaishi kwake; yuko na Bwana mmoja Yesu Kristo, ambaye kwake vitu vyote vimekuwapo, na sisi kwa yeye huyo.

Njia ni Yesu Kristo pekee. Kumjua Yesu ndio kumjua Mungu. Sikiliza maneno yake na amini neno lake.

Yoh 14 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁶ Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
⁷ Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.


Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
Na kwa hiyo yesu ni mjnga aliposisitiza upendo?
Huwezi kutenganisha upendo na Yesu. Maana halisi ya upendo ni Yesu Kristo pekee. Nje yake kinachoitwa upendo sio upendo halisi.

“Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu.”
— 1Yoh 3:16 (SUV)

Katika Yesu ndio tumepata real definition ya upendo. Hivyo kumkataa Yesu na kujidai una upendo ni sawa na kujilisha upepo.

“Lakini yeye alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake.”
— 1Yoh 2:5 (SUV)

“Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”
— Yoh 15:13 (SUV)

Kumwamini ambako ndio kumpokea Yeye aliyekufa kwa ajili yetu tulipokuwa tungali wenye dhambi ndio standard yake ya upendo. Nje na hiyo hujaujua upendo.

Unamwamini Yesu?

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
Tunaamini kuwa Mungu wetu ni mmoja naye ameelezewa na maandiko kama Baba na Mwana.

Tunaamini kuwa Mungu mmoja na wa Kweli amejifunua kikamilifu pasipo kujibakiza katika utu wa Yesu Kristo. Tunamjua Yeye kupitia Yesu Kristo pekee.

1Kor 8 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁵ Kwa maana ijapokuwa wako waitwao miungu, ama mbinguni ama duniani, kama vile walivyoko miungu mingi na mabwana wengi;
⁶ lakini kwetu sisi Mungu ni mmoja tu, aliye Baba, ambaye vitu vyote vimetoka kwake, nasi tunaishi kwake; yuko na Bwana mmoja Yesu Kristo, ambaye kwake vitu vyote vimekuwapo, na sisi kwa yeye huyo.

Njia ni Yesu Kristo pekee. Kumjua Yesu ndio kumjua Mungu. Sikiliza maneno yake na amini neno lake.

Yoh 14 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁶ Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
⁷ Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.


Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
Je ungezaliwa Korea kusini ungeqmini hayo ?
 
Huwezi kutenganisha upendo na Yesu. Maana halisi ya upendo ni Yesu Kristo pekee. Nje yake kinachoitwa upendo sio upendo halisi.

“Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu.”
— 1Yoh 3:16 (SUV)

Katika Yesu ndio tumepata real definition ya upendo. Hivyo kumkataa Yesu na kujidai una upendo ni sawa na kujilisha upepo.

“Lakini yeye alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake.”
— 1Yoh 2:5 (SUV)

“Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”
— Yoh 15:13 (SUV)

Kumwamini ambako ndio kumpokea Yeye aliyekufa kwa ajili yetu tulipokuwa tungali wenye dhambi ndio standard yake ya upendo. Nje na hiyo hujaujua upendo.

Unamwamini Yesu?

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
Kuna jamii nyingi hazimjui yesu naupendo wanaufahamu , mkuu unasema hivyo tu kwasababu umezaliwa tz ukapata neema ya wakoloni kukuletea ukristo.
 
Je ungezaliwa Korea kusini ungeqmini hayo ?
Kama nihubiriwa haya haya ninayokueleza ningewaamini maana ndio kipimo cha Mungu cha upendo.

Je wewe unapima vipi upendo? Kama ni nje ya Kristo Yesu huo sio upendo wa viwango vya Mungu.

Unadhani Mungu atapima upendo wako nje ya vipimo na viwango vyake?

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
Kama nihubiriwa haya haya ninayokueleza ningewaamini maana ndio kipimo cha Mungu cha upendo.

Je wewe unapima vipi upendo? Kama ni nje ya Kristo Yesu huo sio upendo wa viwango vya Mungu.

Unadhani Mungu atapima upendo wako nje ya vipimo na viwango vyake?

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
Huo ujinga wakahadae nao kondoo sio mimi
 
Kuna jamii nyingi hazimjui yesu naupendo wanaufahamu , mkuu unasema hivyo tu kwasababu umezaliwa tz ukapata neema ya wakoloni kukuletea ukristo.
Yes jamii nyingi pamoja na wewe hawamjui Yesu Kristo na upendo wake ndio maana tunashare na kuhubiri injili kwa nguvu zote ili mpate kumfahamu kwamba sio wa kuletwa na wazungu bali ni Mungu aliyekuwako kabla ya kuumbwa ulimwengu na vyote vilifanyika kupitia Yeye.

Ni Mungu aliyejifunua kwa wanadamu kupitia utu wa Yesu Kristo. Sio imaginations au mastori ya kutungwa bali anaelezewa na kuhushudiwa kupitia maandiko matakatifu.

Yoh 1 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
² Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
³ Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
⁴ Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.
⁵ Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.
⁶ Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
⁷ Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye.
⁸ Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru.
⁹ Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu.
¹⁰ Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua.
¹¹ Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.
¹² Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

Unaamini maandiko matakatifu? Unaamini ujumbe wake? Ikiwa waamini yote waliyosema manabii juu yake, huwezi kuwa na ufahamu tena imani ya kikristo ni imani ya kuletwa na wakoloni.



Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom