KERENG'ENDE
JF-Expert Member
- Nov 14, 2010
- 398
- 31
wanajamvi hivi hii nayo ni maada ya kujadili
mtaumbuka muda si mrefu, hamjakata tamaa na kuwaonea watanzania huruma baada ya mpango mzima wa masalia kufichuka? kama mnataka mwenyekiti au katibu kutoka kigoma si muanzishe chama chenu cha kikabila mueleweke kabisa? mnasubiri nini angali mnadai kinara wenu zzk anamvuto kwa jamii? hii ni baadhi tu ya mipango haramu ya ccm ya kutika kuuwa upinzani nchini! wameshindwa na watashindwa tena!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Hivi kwanini hao watu kijiweni wasifuati kauli ya Zitto mwenyewe? "fuata misingi ya chama na sio watu sababu watu wanayumba, misingi haiyumbi".
It is about time wanachama waache kukigawa chama kwa misingi ya udini na ukanda na waanze kupigana the real struggle.
Leo kuna more attacks from cdm members against cdm leaders than there are attacks from ccm.
changia uzi huu kwa maslahi ya chama na si kwa maslahi ya mtu fulani.maana huku mtaani chama kimechafuka na tunatumia nguvu nyingi kukitetea.
Uko sawa lakini sidhani kama vijana wenzako wameshafanya lolote zaidi ya kujitafutia umaarufu wa kisiasa. Vijiwe vya aina hiyo Mkuu vipo vingi sana, watu hawafanyi kazi kutwa kuchambua siasa, unafikiri tutafika kokote kwa kutokufanya kazi? Pato la taifa halitoongezeka kwa kukaa kijiweni kuchambua siasa.Leo nilikuwepo katika kijiwe kimoja hapa Morogoro,hawajamaa ni marufu sana kwa kuichambua siasa ya Tanzania.Hoja kubwa ikawa ni umaarufu wa Zitto ambao wengi wanadai kwa sasa unazidi hata umaarufu wa chama,hivyo wadau wengi wakadhauri kua Zitto ni mtaji mkubwa kwa chama endapo wataamua kumtumia ktk uchaguzi mkuu wa 2015 kwa sababu zifuatazo.
1.Kuifuta propaganda ya udini iliyoanza kuenezwa kwa wa tz.
2.Kuifuta propaganda ya ukabila na ukanda inayoenea kwa kasi sana.
3.Zitto anakubalika sana maeneo mengi kutoksna na michango yake bungeni yenye maslahi kwa taifa.
4.Zitto kukosa kashfa zinazo mkabili.mfano wapo wanao shutumiwa kwa kuwa na kadi zaidi ya moja.hii ni ngumu kumuelewesha mwananchi wa kawaida.hivyo kwa zitto haitamkumba.
5.Watanzania sasa hasa vijana wanaimani kubwa na vijana kuliko wazee.hii ni kutokana na mapinduzi makubwa yaliyofanywa na vijana bungeni.
TUMUUNGE MKONO KIJANA HUYU MCHAPA KAZI ILI ATUSAIDIE KUINGIA IKULU 2015.
Anauzika au ananunulika?3,4,5 umepatia sana zitto anauzika sio kwa maana hamna mwenye haki ya kugombea urais lkn zzk ndo chaguo
afadhali umkweze Mbuzi kuliko mshirikina anaeweza kuua ukoo mzima hadi panya kwa kosa la mtu mmoja.ulitaka amkweze mbuzi au kenge...........
Kwa mtu yeyote aliye makini na anayefanya maamuzi kwa UTAFITI atagundua kua migogoro mingi ndani ya CDM chanzo ni ZITTO, ni migogoro michache sana ndani ya CDM ambayo Zitto hana mchango. Tafakari kwa akili huru utaliona hilo lipo dhahiri sana!kwa mtu yeyote makini anaefanya maamuz kwa UTAFITI
FIKRA
UKWELI&UJASIRI
asiyekuwa kibaraka atakubaliana na mada kuwa ZITTO ni chaguo sahihi na chaguo la wengi!!!
hata chadema,mbowe,slaa wanaliju hilo...!
Zitto aanzishe chama chake chadema hamfai
Masalia wanazidi kuja kwa rangi tofauti tofauti...
changia uzi huu kwa maslahi ya chama na si kwa maslahi ya mtu fulani.maana huku mtaani chama kimechafuka na tunatumia nguvu nyingi kukitetea.