kichenchele
JF-Expert Member
- Jun 28, 2010
- 539
- 176
Ndugu zangu wana JF, nawaombeni sana tujaribu kuwa watu wenye mtazamo wa kusaidiana na kuelimishana, ukweli kuna mada zinazoletwa humu ni nzuri na zenye tija na zipo nyingine ambazo kweli zinakuja hazina mashiko, sasa mimi nawaomba ndugu zangu tusaidiane ili mwisho wa siku tupate elimu japo kwa kifupi tu, maana nategemea watu wengi sana wanaaamini Jamii Forum ni mahala ambapo unaweza kuweka mada, tatizo au hata kuomba msaada uwe wa kisheria, kitabibu, kimasomo, kijamii n.k ukawa ni sehemu nzuri ya kuanzia kabla hujaanza kufuata taratibu nyingine zinazotakiwa. lakini kiukweli mtu unapokuwa unaweka mada yenye mantiki harafu badala ya watu kuchangia au kushauri juu ya nini kifanyike tunaleta utani na dharau na hata kutukanana bila sababu zozote za msingi, hali hii inasikitisha sana, nawaombeni wana JF wenzangu tushirikiane kwa nia njema tu ili hata wale tulio na ufahamu mdogo au tusio juwa juu ya mambo mengi yanayoletwa humu tuyaelewe na tuone watalaamu waliomo humu wanasema nini. Ni kweli kila mtu anajiunga JF kwa lengo tofauti na tumeachana kwa umri, elimu, kipato, ufahamu, uwezo wa kuchambua na kuelewa hoja, lakini hili haliwezi kutufanya tushindwe kusaidiana, ningependa kuiomba jamii iliyomo humu ndani ielewe kwamba inafika wakati hata adui yako akaja kuwa rafiki mzuri na rafiki yako mzuri akawa adui mkubwa. Panapoutani tutaniane, na palipo na hoja nzuri basi ni budi tusaidiane ndugu zangu, naomba kuto hoja, Mungu wabariki wana JF- Mungu Ibariki JF .Siku njema.